Huyu bwana nashauri aache kuji-strain kwa kukaa anatafuta tafuta maneno ya ku-release kwenye media kwa sababu bado yanakuwa si tiba sahihi ya pressure aliyonayo kifuani kwake. Anatakiwa akae chini na kutafakari halafu achukue hatua ambayo itakua ni ya manufaa si kwake tu bali na kwa wengine pia. Kukaa anaiponda Serikali wakati aliwahi kula kiapo, si hekima sana. Na kwa taarifa tu ni kwamba unapokula kiapo, unajifunga kuwa hata kama kutakuwa na mabaya ambayo wewe utayaona, hutakiwi kuyasema wewe kama wewe, ila unaweza ukamweleza mtu mwingine akayasema kwa niaba yako, na pasipo watu kujua kuwa anayasema kwa niaba yako! Ana maumivu makali sana kicfuani na wakati mwingine kuumia kwa kiwango hii hakufai sana kwa mtu ambaye ni mwanasiasa, kwa sababu kwenye siasa kuna mambo mengi mno!