Nape Nnauye: Alipotoka, alipo na aendapo

Mwaka 2002,August,nikiwa najisomea nyumbani,majira ya kumi na moja jioni,huku nikifuatilia matokeo ya kura ya Uchaguzi Mkuu wa ndani wa CCM,nilistuka kusikia Nape, akiwa na miaka 24 wakati huo,wakati huo akisoma Chuo Cha Kivukoni,akitajwa kuongoza katika kinyanganyiro cha kutafuta Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM,kupitia kundi la Vijana la watu kumi.

Nilistuka si kwa sababu kijana huyo hakuwa akifaa kuweza kushinda.Nilistuka kwa sababu sikuwahi kumsikia akizungumzia nia yake hiyo hadharani wala kuonyesha mapenzi na masuala ya siasa.

Wakati wote kijana huyo alikuwa akijihusisha zaidi na masuala ya dini katika kanisa lake la wakati huo la Free Pentecostal Church of Tanzania,FPCT,kanisa la Singida Mjini.Mara kwa mara, alikuwa akipata nafasi ya kuhubiri pale kanisani,licha ya umri wake mdogo wakati huo.

Upo ujumbe wa Jumapili moja,ambao hadi leo umenasa katiaka akili yangu ambao kijana huyu alipata kuufundisha pale kanisani mwanzonni mwa mwaka 2002 alioupa jina la 'Jiandae Kufanikiwa'.Kama vile Obama aliyeanza kuonyesha kipaji chake cha uongozi kanisani kwake alikokuwa akisali kama Community Organiser,ndivyo ilivyokuwa pia kwa Nape.

Baadaye,mwaka 2004 kamanda Nape,aligombea Uenyekiti wa UVCCM na kura hazikutosha.Kama kamanda asiyekata tamaa ,mwaka 2008 aliwania nafasi hiyo tena , na sote tunajua kilichotokea.Kama mpiganaji asiyechoka ,mwaka 2010 aliomba ridhaa ya kuteuliwa na CCM kugombea Ubunge jimbo la Ubungo lakini hakutimiza ndoto yake hiyo.

Baadaye mwaka 2010, aliteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya ya MASASI kabla ya kuteuliwa kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama.
Katika CCM, kutokana na hila ,ghiliba,mizengwe na uhuni, mara zote Nape alizogombea ameambulia patupu isipokuwa ,kutokana na sababau wanazofahamu vyema wateuzi,Nape hajawahi kusahaulikahata mara moja.

Manenno na kauli zake za hivi karibuni zinaashiria kuwa kwake yeye UONGO,GHILIBA zinaweza kuruhusiwa iwapo tu zinafanywa katika ulingo wa siasa.Na sidhani kama Mungu wa Mbinguni ana adhabu tofauti kwa uongo unaotendwa katika siasa na ule unaofanywa katika maeneo mengine.

CCM inaelekea sasa mwisho wake.Nini hatma ya kisiasa ya Nape.Mimi sijui, huenda yupo miongoni mwetu anayejua.
Nimesema kweli yote kadiri ninavyoijua,na kamwe uongo na fitna kwangu ni mwiko maana ni DHAMBI.

HONGERA NAPE KWA KUJIELEZA,KUMBE UNAJITAMBUA VIZUrI
 
Nape namjua uzuri enzi hizo akiishi National Housing, Unyankindi Singida kwa Mjomba ake (ndio kwanza alikuwa katoka kufeli kidato cha IV Nsumba) Kilichomfikisha hapo alipo ni Ubini wa "Nnauye" lakini KAMWE SI UWEZO WAKE BINAFSI. Yeye kama yeye ni DHAIFU kuliko hata udhaifu wenyewe. Angalia anavyojichanganya: Anajifanya kumnanga Lowassa kuwa Fisadi, wakati huo huo anasimama naye jukwaani kumnadi mgombea wa CCM Arumeru. Kwa kifupi usimpomsikia kwa makini utafikiri anachukua UFISADI kumbe anachokifanya ni kutafuta cheap popularity. He's just good for nothing. Tembea ukurasa wake wa Facebook uone anayoyajadili. Tofauti kabisa na akina Makamba, Zitto, Mnyika etc
 
Nimefuatilia baadhi ya posts,nimebaini kuwa yawezekana sikueleweka vyema.Baadhi ya watu wamediriki kudhani kuwa mimi ni Nape.Sehemu ya mwisho ya post yangu inaonyesha wazi mtazamo wangu dhidi ya Nape.Labda kwa uwazi zaidi,niseme kuwa simuungi mkono Nape! mimi si Nape.Na kwa kuwa kamanda yupo jamvini anaweza kuthibitisha ukweli ama uongo wa niliyoandika.
Post yangu ililenga kufanya uchambuzi objectively kuonyesha pande mbili za Nape:Nape kama mtumishi wa Mungu mkweli na muadilifu na Nape kama mwanasiasa wa CCM ambaye uongo ni jadi, propaganda,ghiliba na porojo kwake ni jambo la kawaida sasa.
 
Mkuu FortJeasus.
Kwanza kabisa, futa maandiko/kauli yako ya kusema kwamba nape ni KAMANDA, yeye si kamanda ila ni GAMBA.
Pili, kwa kuwa amechagua chama cha dhuruma, chama cha majambazi, wezi, mafisadi na wanyonya damu, kwa hakika mwisho wa Nepi hauwezi kuwa mzuri.
Tatu, Nepi ni mnafiki sana, tena sana, kama walivyo kina Sitta & co., kwa sababu uozo wa ccm wanaujua na unaonekana, kama wangekuwa na nia njema wangetoka huko.
 
Mkuu FortJeasus.
Kwanza kabisa, futa maandiko/kauli yako ya kusema kwamba nape ni KAMANDA, yeye si kamanda ila ni GAMBA.
Pili, kwa kuwa amechagua chama cha dhuruma, chama cha majambazi, wezi, mafisadi na wanyonya damu, kwa hakika mwisho wa Nepi hauwezi kuwa mzuri.
Tatu, Nepi ni mnafiki sana, tena sana, kama walivyo kina Sitta & co., kwa sababu uozo wa ccm wanaujua na unaonekana, kama wangekuwa na nia njema wangetoka huko.

MD25,nimpokea ushauri wako kama ulivyo...baada ya kuutafakari na kuupima kwa umakini nimeamua kwa hiari yangu kumwondolea Nape hadhi ya ukamanda.Popote kwenye maandiko yangu nimefuta neno kamanda na napendekeza neno Ndugu litumike kama mbadala wake.Bado ni binadamu mwenzetu na kama Kambarage alivyotufunza,binadamu wote ni ndugu
zangu.Poleni sana makamanda wenzangu popote mlipo kwa usumbufu uliojitokeza.
 
Back
Top Bottom