EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
HALI ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), inazidi kuwa tete baada ya wenyeviti wa mikoa wa chama hicho tawala, kupitisha azimio la kutaka Waziri wa Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), atimuliwe uanachama kwa madai kuwa amemtukana, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Mbali na kutaka Sitta atimuliwe, baadhi ya wenyeviti hao wametaka Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, adhibitiwe kwa madai kuwa amekuwa akitoa matamko ya upotoshaji yanayoenda kinyume na maazimio ya NEC.
Wakati kundi la wenyeviti hao likimshambulia Sitta na Nape, kundi lingine lililoongozwa Mwenyekiti wa mkoa wa Mara, Makongoro Nyerere, liliibuka kumtetea Nape na Sitta, hali ambayo ilionyesha dhahiri kuwapo kwa makundi mawili yanayosigana ndani ya viongozi hao wa CCM mkoa.
Hali hiyo ilitokea jana katika kikao cha wenyeviti wa mikoa wa CCM, kilichofanyika katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti CCM Taifa, Pius Msekwa, kwa niaba ya Mwenyekiti, Jakaya Kikwete, zilisema kuwa jina la Sitta ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu, pamoja na Nape, lilitawala kikao hicho.
Kwa mujibu wa habari hizo, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, ndiye alianza kurusha mawe dhidi ya Sitta akidai kuwa Spika huyo wa zamani amemtukana Rais Kikwete na wajumbe wa Kamati Kuu (CC).
Akifafanua hoja yake, Mgeja alisema Sitta alimtukana Rais Kikwete na wajumbe wa CC, kupitia kipindi cha dakika 45, kinachorushwa na kituo kimoja cha TV, akilalamika kwamba waliweka kigezo cha jinsi kwa shinikizo la mafisadi kumuengua kwenye kinyang'anyiro cha uspika ambacho kilijenga mazingira kwa Mama Anna Makinda kupita kirahisi.
Chanzo chetu cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho, kilisema kuwa Mgeja alisema anashangazwa na ukimpya wa chama kutochukua hatua dhidi ya Sitta na kupendekeza kuwa afikishwe na kuhojiwa kwenye vikao vya chama na asipotoa maelezo ya kujitosheleza, atimuliwe.
Mbali ya kumvaa Sitta, Mgeja pia alimshambulia Nape kwamba amekuwa akitoa kauli za kupotosha dhidi ya mkakati wa kujivua gamba wa chama kwa kuwalenga watu asiowataka.
Ukimwacha Mgeja, baadhi ya wenyeviti wengine waliounga mkono hoja hiyo na majina ya mikoa yao kwenye mabano ni John Guninita (Dar es Salaam), Clement Mabina (Mwanza), Onesmo Ole Nangolo (Arusha), Nawab Mulla (Mbeya) na mwenyekiti wa mkoa wa Mtwara.
Kwa mujibu wa habari hizo, wenyeviti hao kama vile walipangwa, walimwangushia lawama nyingi Nape kuwa amekuwa akipotosha chama kuhusu dhana ya kujivua gamba kwani hakuna maazimio ya NEC yaliyotaja majina ya watu wanaopaswa kujiuzulu.
CHANZO: Tanzania Daima
Mbali na kutaka Sitta atimuliwe, baadhi ya wenyeviti hao wametaka Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, adhibitiwe kwa madai kuwa amekuwa akitoa matamko ya upotoshaji yanayoenda kinyume na maazimio ya NEC.
Wakati kundi la wenyeviti hao likimshambulia Sitta na Nape, kundi lingine lililoongozwa Mwenyekiti wa mkoa wa Mara, Makongoro Nyerere, liliibuka kumtetea Nape na Sitta, hali ambayo ilionyesha dhahiri kuwapo kwa makundi mawili yanayosigana ndani ya viongozi hao wa CCM mkoa.
Hali hiyo ilitokea jana katika kikao cha wenyeviti wa mikoa wa CCM, kilichofanyika katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti CCM Taifa, Pius Msekwa, kwa niaba ya Mwenyekiti, Jakaya Kikwete, zilisema kuwa jina la Sitta ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu, pamoja na Nape, lilitawala kikao hicho.
Kwa mujibu wa habari hizo, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, ndiye alianza kurusha mawe dhidi ya Sitta akidai kuwa Spika huyo wa zamani amemtukana Rais Kikwete na wajumbe wa Kamati Kuu (CC).
Akifafanua hoja yake, Mgeja alisema Sitta alimtukana Rais Kikwete na wajumbe wa CC, kupitia kipindi cha dakika 45, kinachorushwa na kituo kimoja cha TV, akilalamika kwamba waliweka kigezo cha jinsi kwa shinikizo la mafisadi kumuengua kwenye kinyang'anyiro cha uspika ambacho kilijenga mazingira kwa Mama Anna Makinda kupita kirahisi.
Chanzo chetu cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho, kilisema kuwa Mgeja alisema anashangazwa na ukimpya wa chama kutochukua hatua dhidi ya Sitta na kupendekeza kuwa afikishwe na kuhojiwa kwenye vikao vya chama na asipotoa maelezo ya kujitosheleza, atimuliwe.
Mbali ya kumvaa Sitta, Mgeja pia alimshambulia Nape kwamba amekuwa akitoa kauli za kupotosha dhidi ya mkakati wa kujivua gamba wa chama kwa kuwalenga watu asiowataka.
Ukimwacha Mgeja, baadhi ya wenyeviti wengine waliounga mkono hoja hiyo na majina ya mikoa yao kwenye mabano ni John Guninita (Dar es Salaam), Clement Mabina (Mwanza), Onesmo Ole Nangolo (Arusha), Nawab Mulla (Mbeya) na mwenyekiti wa mkoa wa Mtwara.
Kwa mujibu wa habari hizo, wenyeviti hao kama vile walipangwa, walimwangushia lawama nyingi Nape kuwa amekuwa akipotosha chama kuhusu dhana ya kujivua gamba kwani hakuna maazimio ya NEC yaliyotaja majina ya watu wanaopaswa kujiuzulu.
CHANZO: Tanzania Daima