Nape na posho za Wabunge

Nape na posho za Wabunge

Aanze Nape kujivua gamba la uroho wa madaraka ndio wafuate mapacha wa3...CCJ oyeeeeeee
 
Zitto unatushangaza sana kuhusu suala lako la Posho yako kupelekwa KDI. Kama wewe unadhamira njema na si kutafuta umaarufu na ghiliba kwa Watanzania kwa nini usingepeleka hoja binafsi ya kubadili sheria bungeni ili muifute? Sheria huvunjwa kwa kupeleka Mswada bungeni sasa kijana unategemea kweli utaivunja kwa kumwandikia spika barua au kwa kuongea mitaani na barabarani. Zitto kuwa makini katika hili watu wanaokuheshimu na kukuona wewe kama mtu makini wanakudharau.
 
Mkuu upo wapi wewe? hoja ya KDI imeshafungwa Zitto ameshakataa kabisa kuchukua hiyo "posho ya kukaa" kuanzia tarehe 8/6/2011.. Kusanyeni hizo posho kwa ajili ya kofia, fulana na mabango 2015.
 
NAPE ni limbukeni wa fikra anawaza kwa makasi,akili kaziacha kabatini
 
We gamba unawaza kwa kutumia makamasi,akili umeiweka kabatini,ZITTO na CHADEMA wameshasema posho hawazitaki tena,
 
wewe ni gamba, hlf jaribu kuwa na utamaduni wa kusoma habari
 
Hata kama una mashaka na dhamira yake, alichokifanya kinaweka pembeni kidogo ubinafsi uliojaa mioyo ya wana siasa wenu. Kama hauiamini dhamira ya Zitoo amini kazi zake zilizo wazi using'ang'anie dhamira usiyoona. Yesu alisema kama hamniamini mimi ziaminini kazi zangu- hiyo tu inatosha!
 
soma barua ambayo zito amejibiwa na bunge,kushindikana kwakile alichokitaka cha kubadilisha akaunti no yake toka ile yabinafs kuingiziwa posho na kuomba ile ya taasisi yake ya kigoma.zito unaanza kufulia mipango yako ya kujitaftia umaarufu kuwa nayo makini
 
safi sana vijana inaelekea mnaanza kuwa na akili kidogo. sasa nataka muendelee kujadili kama kweli wanauchungu na hizo pesa kwa nini wawe na uchungu na hizi na wasiwe na uchungu na milioni 7 isiyotozwa kodi wanayomlipa Slaa. Acheni kuwa makasuku hapa hakuna nia yeyote njema zaidi ya kutaka umaarufu. lakini kwa miaka hii yote mitano iliyopita alipokea. Amekumbuka nini mwaka huu? I know Zitto vizuri toka nikiwa naye UDSM. He is the same hajabadilika ila kwa ninyi msiomfahamu endeleeni kula chaka.
 
soma barua ambayo zito amejibiwa na bunge,kushindikana kwakile alichokitaka cha kubadilisha akaunti no yake toka ile yabinafs kuingiziwa posho na kuomba ile ya taasisi yake ya kigoma.zito unaanza kufulia mipango yako ya kujitaftia umaarufu kuwa nayo makini
Zitto alitaka afikishe ujumbe kwamba posho zitumike kwa maendeleo na si kuharibu mabinti wa UDOM!
 
Mimi ningependa kuzungumzia suala ninaloliita political discourse: inaelekea wabongo wasiojali masilahi ya wananchi waliowengi (pangu pakavu) wameanzisha political discourse ya 'kujitafutia umaarufu' kwa kila anayeonesha kutetea maslahi ya walio wengi. Sioni ubaya wo wote kwa mwanasiasa au mwanaharakati 'kujitafutia umaarafu' alimradi 'umaarufu' huo utamkomboa mwananchi wa kawaida kupata haki zake - angaa zile za msingi. Zitto & Co msikatishwe tamaa na hii lugha mpya ya 'kujitafutia umaarufu'. Kaza buti jitafutie umaarufu na Muumba atawaongezea.:cool2:
 
kichapo2015
Join Date : 10th June 2011
Posts : 14
Thanks 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power : 0

Another Nape's disciple,
u will know them by their actions.
 
serikali ya ccm kuondoa ubishi imkomoe zitto kwa kusema hiyo posho isiende KDI bali posho ya zitto na wabunge wengine wote iondolewe na kupekwa hazina ili nyie mnaomsakama zitto mtulie.
 
wanafiki wakubwa! wanatutoa kwenye ishu za msingi sasa tuna kazi ya kujadili posho zao.kwanini wasingekataa kabla ya uchaguzi?hawakufanya hivyo cse zilikuwa muhimu sana kuwahonga wapiga kura ili warudi tena mjengoni.leo badala ya kujadili hoja za msingi wanaanza kulumbana na spika kuhusu posho.hypocrites!!
 
Achebe, Ulitaka akatae ln?ndo kakataa sasa iv...kupigia kelele posho hawajaanza leo na alichofanya ni maelekezo aliyopewa na viongoz wa bunge..kumbuka ndugai alivowaambia 'kama wabunge wa upinzan hawatak posho waache kuzichukua tuone' ndo ivo kaacha sasa
 
Zitto unatushangaza sana kuhusu suala lako la Posho yako kupelekwa KDI. Kama wewe unadhamira njema na si kutafuta umaarufu na ghiliba kwa Watanzania kwa nini usingepeleka hoja binafsi ya kubadili sheria bungeni ili muifute? Sheria huvunjwa kwa kupeleka Mswada bungeni sasa kijana unategemea kweli utaivunja kwa kumwandikia spika barua au kwa kuongea mitaani na barabarani. Zitto kuwa makini katika hili watu wanaokuheshimu na kukuona wewe kama mtu makini wanakudharau.
Mkuu nadhani tatizo la Watanzania siku zote ni ktk maswala ya siasa. Tuna ujinga fulani ambao hauwezi kuelezeka kirahisi bila kuhoji dhamira za watu.

Labda nikukumbushe tu kwamba swala la posho za vikao halikuanza jana wakati Zitto anahoji posho hizi, lipo bungeni na limekuwepo kwa muda isipokuwa viongozi wetu hawataki kusikia kabisa kuondolewa kwa posho. na hakuna ujanja mwingine wowote wa kuwabana viongozi isipokuwa kwa mmoja wao kuwapa mtihani ambao hawataukubali ili mradi swala zima la posho lipate kuzungumziwa.

Sisi kama wananchi tunachotakiwa kujiuliza ni kwa nini wabunge wetu wanaotuwalikisha hawataki posho hizi ziondolewe! Kwa nini haramu hii inazidi kutukuzwa bungeni badala ya wao kama wawakilishi wa wananchi kufuata na kutumikia maagizo ya wananchi na sio kutafuta vijisababu vya kupinga dhamira ya Zitto ili mradi Zitto mwenyewe ndiye awe sababu.

Sijui kama unamkumbuka Babu wa Loliondo, yeye alikuwa akitoza Tsh 500 tu kwa dawa ya ponya yake lakini wapo watu waliompa ama kutaka kumpa fedha zaidi akawaambia wapeleke kanisani, sasa ukianza kujiuliza kwa nini anataka hizo fedha zaidi ziende kanisani kwa fikra kwamba yeye ni mchungaji hivyo anataka kujinufaisha kwa kupitia huko unakuwa unapotosha maana kwani hoja nzima ni kwamba Uganga wake unagharimu Tsh. 500 tu.
Na wala haikuishia hapo tu kuna watu walihoji vikombe, masufuria, mahema na hata nyumba alokuwa akihudumia mchungaji wakamwona tapelii tu wakati hawa hawa watu wana magonjwa makubwa yanayohitaji sana msaada wake na wala isingewagharimu hata kama dawa hiyo haitawaponya lakini inawapa unafuu fulani..

Hii ndio tabia ya Wadanganyika, tabbia ambayo siku zote hulalamikia hata vitu ambavyo malengo yake ni kuwaponya wao wkani Zitto anachokifanya hapa lengo lake haswa ni kuhakikisha Posho hizi zinaondolewa na fedha hizo zipelekwa (re allocated) ktk matumizi mengine ya msingi..

Jamani ebu irudieni kuisoma Bajeti utaona kwamba tunapanga matumizi ya trillioni 13 na kati ya hizo karibu trillioni moja imetengwa kwa posho tu, fedha ambazo zingeweza kabisa kuondoa matatizo mengi ya mishahara ya walimu, madaktari au hata kuboresha shule na hospital zetu lakini viongozi wetu wamegoma kabisa kuondoa hizi posho ambazo kusema kweli wao wenyewe wanasema hupokea zaidi ya mishahara yao..

Dhamira ya Zitto ni kuhamasisha wabunge wazikatae hizi posho lakini imeshindikana hivyo swala kubwa kwetu iwe kuuliza hawa wabunge kwa nini wamekataa kuondoa Posho hizi hali sisi wananchi tunaambiwa tujifunge mkanda hali ya uchumi ni mbaya na nakumbuka Ngeleja aliwahi kusema kila mtu atakula kwa jasho lake!
 
Utashangaa kwa nini wabunge wanang'aka zikiguswa posho zao, wanakuwa wakali kama wembe, kwa nini?
Ukweli ni kwamba utamu wa siasa ni ubinafsi, hasa siasa za kibongo. Ndiyo maana professionals wameacha kazi zao walizosomea na kuanza ubinafsi kupitia siasa. Hawaoni huruma kuwapa walimu mshahara unaolingana na posho zao, hawaoni noma raia kuishi kwa mlo mmoja huku wao wakijilimbikizia mali, ukienda uswisi wamejaza mabenki kwa akiba mabilioni kadhaa huku raia wakitaabika kwao kitu cha mhimu ni " mimi nineemeke kwanza kabla ya watu walionichagua" by the way huu ndio utamu wa siasa- UBINAFSI
Ndiyo maana wabunge wa ccm wamechukizwa na kitendo cha akina zitto kukataa posho, sababu zozote wanazotaja ni za uongo, ni ujanja ujanja tu ili ubinafsi wao wauendeleze. Hii vita ya kupinga posho ni ngumu kwani wako tayari hat kufa wakiipinga maana hiyo ndiyo sababu iliyowapeleka bungeni na siyo kuwawakilisha wananchi au kuisimamia serikali. Ndiyo maana wako tayari kukubaliana na ujinga unaofanywa na serikali ilmradi mwisho wa siku wapate posho zao. Kweli utamu wa siasa ni UBINAFSI!
 
Back
Top Bottom