Nape: Lowassa kapoteza sifa ya kugombea


mkuu nape kwanza kheri ya mwaka mpya 2014, binafsi nimesikia magazetini sijaipata habari yote.
halafu ili tukuone wewe siyo mnafiki tuambie siku 90 ulizompa lowasa, chenge, kikwete zinaisha lini?
ni kweli nape kabla hujahongwa ukuu wa wilaya ulikuwa msema ukweli lakini baada ya hapo na kupewa ukatibu mwenezi ukawa mtukanaji hata hapa huchelewi kuikana hii ID..
 

Hapo umeongea mkuu wangu. Ndio maana nikasema CCM wamebaki watu wachache sana wanaoweza kusimamia misingi ya Chama na wewe ni mmojawapo.
 

Asante kwa ufafanuzi.
Lakini pamoja na hayo, inaonyesha kuna watu wanafanya hayo ambayo taratibu za chama haziruhusu na wewe unawafahamu kwa majina.
Kwanini unakua muoga au mnafiki tena kwa kushindwa kukemea kwa kuwalenga wahusika?, au unakemea kwa kuacha room ya kujitetea kwa kusema "mimi sikutaja jina?"
Pia tunaomba ujibu hoja ya siku 90 ulizotoaga, unaongeleaje kuwa ni miaka 900?!
 
japo haya maneno yako general,ukichunguza kwa umakini mlengwa anafahamika.
 
...nape lea ndoa yako kwanza,huyo jamaa sio saizi yako...
 
Reactions: Sal
Nape haogopi hata wazee..!! Lowasa ni mzee, mheshimiwa, mchapakazi, tajiri, sio mchoyo, ni mfadhili wa ndani, mwenye kuthamini watu, mtoaji wa zaka, sadaka na michango makanisani, mwezeshaji wa vijana, n.k.

jinsia yako tafadhali!!!

napredict ni KE
 
Kundi kubwa lipi? Watu 2500 waliokubali kununuliwa unawahesabu kuwa ni kundi kubwa kati ya watanzania milioni 45?
 

siasa za vijembe we ni bingwa,punguza kutumika Nape!!!!!!!
 
Nape kama wewe ni mwanamabadiliko si uhame CCM? kuendelea kutoa matamko ambayo kiukweli hayasikiliziki na yatapuuzwa na wenye CCM.
zile harakati zako za CCK na watu wako ziliishia wapi? vp kuhusu tembo wetu mbona huliongelei? acha uchumia tumbo.
 
...nape lea ndoa yako kwanza,huyo jamaa sio saizi yako...

Nape yupo sahihi nampongeza sana, haiwezekani mtu/watu wakitaka kugombea wagawe pesa kama vile wanaviwanda vya kudurusu pesa, mtu alikuwa mtumishi wa umma leo hii anaendesha harambee za mabilioni si awapelekee watu wa jimbo lake waondokane na shida za maji na chakula! Au awajengee malambo ili mifugo yao iache kuzurura hovyo
 
Nape, we sema sema tu, wakiingia madarakani hao, sijui utajificha wapi
 
Ukweli unabaki pale pale kuwa Nape ni jasiri sana na anajua anafanya nini. Wachumia tumbo wengi wa umri wake hawawezi kufanya wala kuthubutu kufikiria kama Nape. Kwa hiyo mpeni moyo kijana mwenzenu. Wazee wanajua uwezo wake na ndiyo maana wamemwamini. Nape hizi kelele za wasiojua zisikukatishe tamaa bali zizidi kukupa nguvu ya kukaza buti. All the best and Happy New Year!
 
Nape huwa siyo mnafiki. Huyu kijana hazina ya CCM.


ni kweli huyo bwana ni afisa habari wa chama na kila anachozungumza, kama ilivyo kwa wasemaji wa taasisi wengi, ni consensus ya taasisi yake vinginevyo tungesikia katibu mkuu kinana akimkaripia au hata mwenyekiti wake lakini hatuoni ukanushaji wowote wa hilo.
pia tumezoea kusikia kwamba kukemea ufisadi, ikiwa ni pamoja na uvunjaji wa kanuni za chama, ni kitu ambacho el hawezi hata siku moja,wengi tunasema hawezi kufanya hivyo
 
Awamu ijayo ni zamu yetu kaskazini hata mfanyeje
 
Amekutuma umsemee au umejituma? Maana maCCM hamkawii kuomba buku saba kisa umemteta Lowasha kwenye mtandao!
 
Nape Nnauye ni Kijana aliyekosa hekima, toka pale alipowatukana kina Mzee Warioba... Nilijua kichwani hamnazo.

Crashwise nnni nin kina kushangaza kutoka kwa Nape???? hana hekima na elimu yake ni ya kubabaisha, anafanya siasa za mazoea, hajui athari za mchezo anaoucheza!!!! Unafiki ni dhambi kubwa duniani na hata Mbinguni, mnafiki kamwe hawezi kushinda... Hakuna mtu asiyetoa rushwa CCM, kuna wanaonga vyeo na Nape anajua mana naye ni mpokea na mtoaji hongo hii, ila yeye hukaa na kumlaumu Lowassa tu, kwa chuki binafsi, akiamini ndo alisababisha akaenguliwa uenyekiti UVCCM bila kujua ndo hao hao wanaompa kula leo.. hakuna wa ku mstop Lowassa CCM, kama uchafu hakuna aliye msafi hata mwenyekiti mwenyewe tena yeye ndo balaa... si maneno mtaani twasikia!!!!

Kama Lowassa fisadi mbona vua gamba ilikufilia mbali na rushwa ni kosa la jinai kama Nape anaushahidi kwanin asiende mahakamani au kwenye kamati ya maadili ya chama??? huyu jamaa ni chumia tumbo kama wengine kwake bora leo ya kesho nitayajua hukohuko.. Badilika Nape..
 
Reactions: Sal
Nape Jaman yuko sawa huyu lowassa atatuua jiulizen hz juhud zote na nguvu zote nzann????
 
Nape haogopi hata wazee..!! Lowasa ni mzee, mheshimiwa, mchapakazi, tajiri, sio mchoyo, ni mfadhili wa ndani, mwenye kuthamini watu, mtoaji wa zaka, sadaka na michango makanisani, mwezeshaji wa vijana, n.k.

Sema tu MTOA RUSHWA tutakuelewa! njaa zitawaua vijana kama nyinyi mnaowaza makombo ya mafisadi.fanyeni kazi mjitegemee kiuchumi ni kifikra kuliko sasa mnavyoishi kwa kutegemea kuhongwa! mtapelekwa mombasa one day...
 
Nape haogopi hata wazee..!! Lowasa ni mzee, mheshimiwa, mchapakazi, tajiri, sio mchoyo, ni mfadhili wa ndani, mwenye kuthamini watu, mtoaji wa zaka, sadaka na michango makanisani, mwezeshaji wa vijana, n.k.

Hahaha sifa za kijinga...kwa hela za nani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…