wewe mwenyewe hujatulia sijui ndio fisadi maana hata jina la baba Nape hujui kuliandika: Nnauye sio kama ulivyoandika wewe.
Pili ujumbe wako hauna maana hata tone. kaa utulie kama umefulia utajiju
Wapendwa wana JF ufuatao ni ujumbe wangu kwa Nape Mnawiye kufuatia mashambulizi yake kwa CDM akijaribu kukwepa ahadi zake za kuwapa Mapacha watatu siku 90. Naomba nyongeza na mtazamo wenu katika hili maana itamsaidia jamaa kujua kama anachapia au amewini bingo.
Nape.....! Nape.....! Nape.....! Nape.....!
Tangu ulipoteuliwa katika Kamati Kuu Mpya ya chama chako cha Magamba umekuwa msemaji/mropokaji sana na umesababisha baadhi ya watanzania kudhania JK anakuunga mkono kuwashambulia mafisadi wenzenu usiokubaliana nao. (wenye kuelewa tunajua ulikuwa unakurupuka tu maana hakuna siku JK atashirikiana na wewe against RA au EL).
Baada ya kuonywa na mabosi wako dhidi ya uropokaji sasa unataka kujaribu kuwashambulia Chadema ukidhania itabadilisha mitazamo ya wanajamii waliochoka na chama chenu na kurejesha kijiheshima kidogo ulichostahili. Hapo umepotea zaidi maana kinachotukera ni ufisadi wenu mkubwa ambao unasababisha asilimia 100 ya matatizo yote yanaoyoweza kudhibitiwa na binadamu katika nchi yetu. Pengine huna akili ya kuelewa hilo lakini ukweli ni kwamba hata ile rushwa ndogo ya serikali za mitaa inasababishwa na rushwa kubwa ambazo zinamnyima mwenyekiti wenu moral authority kukemea maovu mengine yote katika jamii.
Mimi naamini hata hiyo nafasi ulipewa kwa sababu walidhania ufisadi wako binafsi umejificha kidogo katika jamii kuliko wengine na ingeweza ku-buy time wakati mafisadi wakuu wanajipanga kuweka kibaraka wao mwingine ikulu kupitia chama chenu ifikapo mwaka 2015. Mungu atuepushe na dhahama hiyo. Ndiyo maana tunawaunga mkono Chadema si kwa kuwa wewe unawasilfu au la bali kwa kuwa wanaweza kutusaidia kutuepusha na fisadi mwingine hapo Magogoni.
Ukichunguza vizuri utagundua hata ukuu wa wilaya ulipepa ili utulie maana wakubwa waliona umezidi kelele. Chama chako na viongozi wake wote mnajijua mlivyooza na unyoka wenu, ndiyo maana mnatoa mifano ya kujivua magamba. Nyoka ndiyo wanaojivua magamba na si wanasiasa. Wanasiasa wanawajibika na kusafisasha vyama vyao.
Nakushauri utafute approach nyingine ya kupata umaarufu maana, ufisadi wa Slaa (hata kama upo kweli) si ajenda ktk Tanzania hii mliyoifilisi kwa matumizi yenu mabaya na kutusababishia maisha magumu wakati baba zenu na viongozi wenu wakiendelea kutajirika kwa ufisadi.
Acha kumfuatilia Nape wafuatilie Viongozi wako wa Chadema,pilipili usio ila inakuwashia nini? Nani kakwambia mafisadi wameachwa?
Kila mtu ndg. yangu anao uhuru wa kutoa maoni yake lakini maoni ya mtu mwenye BUSARA utayajua na Maoni ya mtu aliyetoka MIREMBE pale Dodoma nayo utayajua. Mwenyezi Mungu akusamehe kwa kutumia vibaya uhuru wako wa kutoa MAONI. RUSHWA inasemwa hata kweta kwenye vitabu vitakatifu. Kama watu wako wamefisadi kubali ufisadi wao si kudai si ajenda.
Yaelekea wewe umetumwa na huyo mjomba wako NAPE. Sasa nakuhabarisha kuwa, mwisho wenu umeshafika, tieni maji msije nyolewa kichwa kikiwa kikavu.
wewe mwenyewe hujatulia sijui ndio fisadi maana hata jina la baba Nape hujui kuliandika: Nnauye sio kama ulivyoandika wewe.
Pili ujumbe wako hauna maana hata tone. kaa utulie kama umefulia utajiju
Kila mtu ndg. yangu anao uhuru wa kutoa maoni yake lakini maoni ya mtu mwenye BUSARA utayajua na Maoni ya mtu aliyetoka MIREMBE pale Dodoma nayo utayajua. Mwenyezi Mungu akusamehe kwa kutumia vibaya uhuru wako wa kutoa MAONI. RUSHWA inasemwa hata kweta kwenye vitabu vitakatifu. Kama watu wako wamefisadi kubali ufisadi wao si kudai si ajenda.
Nyinyi na wanamagamba wenzenu wote ni wafinyu wa kuelewa kama huyo Nape wenu mmekosa la kusema sasa mnaropoka tu mkidhani watanzania wajinga kama nyinyi. Hivi hamuoni tofauti kati ya mshahara na ufisadi nyinyi maboga kweli nyinyi wenyewe mnakiri kuwa Dr. Slaa anaplipwa mshahara wa kiasi hicho mnachokitaja nyie. Lakini Dr. anapozungumzia EPA au Richimond haihusiani kabisa na mishahara ya watu hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi ufisadi ni kuhujumu taifa kwa kuchota pesa zisizo halali!! Sasa kama Dr. analipwa na chama na chama kimeridhia malipo hayo huo sio ufisadi!! Hiyo inaonyesha kuwa chama kinaridhika na kazi za Dr.!! Hiyo pesa haichukuliwi kiwizi!! ni pesa iliyoidhinishwa na kamati halali za chama! Sasa ndo kusema hamjui tofauti kati ya ufisadi na mshahara? nyinyi kweli mazumbukuku!!!Nape hapambani na Dr Slaa. Anapambana na hoja za Dr Slaa. Mpeni nafasi. Baadhi yetu tunayasubiri majibu toka kwa Dr Slaa. Ni kweli analipwa kama David Beckham kule LA Galaxy?
si kutumwa na mjomba au shangazi mvuni!!. Utashi ni jambo zuri. Utashi ndio unaomtenganisha binadamu na wanyama wengine. Binadamu anapopungua utashi hugeuka na kufanana na wanyama. Hivi kosa la nape ni kuyasema mapungufu ya dr. Slaa na mbowe???? Je mwataka kutuambia hao ni watakatifu???? Mnataka wana jf waamini utakatifu huo muutakao????? Vitisho ni vizuri kwa mtu asiye jiamini kwani vinampa kaujasiri. Ha ha ha ha !!! Naikumbuka hadithi ya fisi na mkono wa binadamu.
wewe mwenyewe hujatulia sijui ndio fisadi maana hata jina la baba nape hujui kuliandika: Nnauye sio kama ulivyoandika wewe.
Pili ujumbe wako hauna maana hata tone. Kaa utulie kama umefulia utajiju
Si kutumwa na Mjomba au Shangazi Mvuni!!. UTASHI NI JAMBO ZURI. Utashi ndio unaomtenganisha BINADAMU na WANYAMA wengine. Binadamu anapopungua utashi hugeuka na kufanana na wanyama. Hivi kosa la Nape ni kuyasema mapungufu ya Dr. Slaa na Mbowe???? Je mwataka kutuambia hao ni watakatifu???? mnataka wana JF waamini UTAKATIFU huo muutakao????? Vitisho ni vizuri kwa mtu asiye jiamini kwani vinampa kaujasiri. Ha ha ha ha !!! Naikumbuka hadithi ya FISI na MKONO WA BINADAMU.