Nape kuwataja wanaoharibu CCM

List ni hii 1. Mfumo wote wa magamba na serikali yao umeoza 2. ?
 
Lazima aseme ni cdm hana jipya!
 
Huu mchezo wa kuogopana huu, siku zina kwenda hakuna utekelezaji, chama kinapoteza imani siku hadi siku. Mwenyekiti aalea makundi chama kinakufa hivihivi anaona kwa macho!
DHAIFU KWELI NI DHAIFU!!!

hata membe naye anasema atawataja wanaombomoa,
halafy=u wanasema ccm ni moja,
moto hauwaki? ila sisi tunaona moshi!
 
Ngonjera za Nape bana.........tabu kweli kweli viongozi wa CCM!
 
Nani asie mjue nape kwamba ni mropokaji asie weza fanya anachokisema Nape amekuwa kama Mbwa anae bweka asie weza kung'ata kwa kukosa meno, amalize gogoro lake la kujimegea maposho ya chama chake eti kwa kufanya mikutano ya ahadi limekuwa deni maana hazitekelezeki
 

Anahangaika na nini alishatwambia hawamsumbui maana ni oil chafu.
 

Hii tabia ya kutishia kutaja majina haya na yale inabidi sasa viongozi wa CCM waiache mara moja kama kweli wana nia ya kuzidi kutupa imani sisi wanachama wa CCM mitaani. Siasa za CCM zinaanza kuwa za kitoto sasa. Kama vikao vya ndani vinashindwa kutatua migogoro hiyo, msituletee wanachama migogoro yenu kwani sisi tunawachukulia nyinyi kama viongozi wa kutupeleka the promised land. Kama mmeshindwa kupata suluhisho kupitia taratibu husika, media haitawasaidia bali mtazidi kuweka bayana kwamba uongozi umewashinda. kama imefikia hali hiyo, pisheni wengine wenye uwezo watuongoze, wapo wengi tu.
 
Kikwete, Pinda, Mkapa, Mukama na Msekwa na magamba wengine katika nafasi za juu za uongozi.
 

Hana jipya,

kabla ya kuwataja wenzake aanze na yeye binafsi kwani ameshindwa kutekeleza sera ya kujivua gamba iliyoasisiwa na chama chake. ameshindwa kuwavua uanachama mafisadi, ameshindwa kukomesha siasa za maji taka alizosema Razizi ect
 
sasa mara wengne wanasema wanasubir kuoteshwa urais ambapo dunian najua urais ni dhamira ya dhati si ndoto mhhhhhhhhhh>,mara kutajana kwan nani hajui nape ana kundi lake,linalopambana na kund strong ndasn ya ccm linalojulikana ata nje ya chama wa kwanza ajitaje yeye 1.nape 2.ndoto 3..............amalizie
 

Makinda kashatekeleza hili kwani BUNGENi huruhusiwi kutaja majina ya watuhumiwa wala kuhoji.
 
This time atawapa siku ngapi wajiondoe? Manake last time aliwapa watu siku 90, zikaisha, hawakuondoka, hadi leo bado wamo.
 
Tumechoka kusikia tutawataja majina. Kwa sasa naona vitisho umekuwa mtaji mzuri wa kisiasa kupata wafuasi na mashabiki wengi. Ni vizuri kufuata nyayo kwa wengine ambao hutaja kwa uwazi bila kubabaika.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…