Wasioaminika wanapotaka waaminike kwenye mambo yasiyoaminika

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,057
Siku zote, historia yako, ndiyo hutoa imani kwa watu wengine.

Hivi ni tangu lini anayejulikana ni mwizi na fisadi, mtu akasema amemwona anaiba, taarifa ikatolewa kwa jamii inayomzunguka, mwizi huyo akasema siyo yeye aliyeiba, halafu jamii ikaiamini kauli yake ya kukanusha bila vielelezo? Kiuhalisia, ni rahisi kuaminika raia aliyetoa taarifa ya wizi uliofanywa na mwizi mzoefu, hata bila ya vielelezo kuliko mwizi mzoefu kujitetea bila ya vielelezo.

Amesikika msemaji wa Bunge akieleza kuwa kauli ya Mbowe kuwa wabunge wale batili, wevi wa kura, Rais Samia amewaongezea mshahara toka shilingi milioni 13 hadi milioni 18, siyo ya kweli. Lakini hakuweza hata kusema ukweli ni upi. Wala hakutoa kielelezo chochote kuuonesha uwongo wa Mbowe.

Lakini tunajua kuwa Bunge, CCM na Serikali, wote wana historia mbaya ya uwongo, ufisadi na wizi. Na vithibitisho ni vingi.

Hawa watu waliojazana bungeni ni wezi wa kura na wezi waporaji wa mamlaka ya wananchi katika kuwapata viongozi.

Baadhi yao wamejazana Bungeni bila kupata kura ya mtu yeyote bali kwa kutangazwa tu na vibaraka wao wa wizi wa kura kuwa ndio washindi.

Viongozi wa chama hiki ndio wanaoongoza serikali ya watu waongo walioweza kufikia hatua mpaka ya kutamka Hayati Magufuli alikuwa anachapa kazi ikulu, wameongea naye kwa simu na anawasalimia sana wananchi, wakati Hayati alikuwa dakika za mwisho za kuyaaga maisha ya Duniani.

Walioiba kura, walioiba maamuzi ya wananchi, hawawezi kushindwa kuiba pesa za umma kwa kupitia njia mbalimbali, ikiwemo hiyo ya kujirundikia mshahara wa sh 18m na posho ya sh milioni 8, total 26m.

Lakini ukiona watu wachache wanafanya uchafu kama huu, ujue umma ndio uliobweteka.

Siku wananchi watakapoweza kunena kwa kauli na dhamira kuwa sisi wananchi ndio wenye maamuzi ya mwisho, ndipo hawa waovu watakapokoma kuyatenda mambo ya ajabu ya kuzinufanisha nafsi zao kwa gharama ya umma wa Watanzania.
 
Mnapenda Sana kupika uongo na uzushi pasipo ushahidi wa aina yoyote ile. Mbowe alifanya kutafuta sifa tu kwa watu kwa kuzungumza vitu vya uongo na uzushi. Nenda kamwambie akupatie ushahidi ili uje uweke hapa jukwaani na siyo kupiga porojo na mihemuko tu.msifikiri Watanzania ni wajinga wa kumeza na kukariri kila kitu bila kuchuja.inawezekana mbowe alijuwa anaongea na wanachama wake wa CHADEMA ambao amezoea kuwadanganya,kuwaswaga kama makondoo na kuwachukulia hawana akili kama manyumbu.
 
Mnapenda Sana kupika uongo na uzushi pasipo ushahidi wa aina yoyote ile. Mbowe alifanya kutafuta sifa tu kwa watu kwa kuzungumza vitu vya uongo na uzushi. Nenda kamwambie akupatie ushahidi ili uje uweke hapa jukwaani na siyo kupiga porojo na mihemuko tu.msifikiri Watanzania ni wajinga wa kumeza na kukariri kila kitu bila kuchuja.inawezekana mbowe alijuwa anaongea na wanachama wake wa CHADEMA ambao amezoea kuwadanganya,kuwaswaga kama makondoo na kuwachukulia hawana akili kama manyumbu.

Tatizo wewe huna weledi wa aina yoyote.

Zipo kanuni za Bunge za kuwahoji na kuwawajibisha watu wanaotoa taarifa za uwongo kuhusu Bunge na wabunge. Kama Mbowe ni mwongo, unadhani ni kwa nini Mbowe hajaitwa kuhojiwa na Bunge kama kanuni zinavyoelekeza?

Wewe tunakutambua. Hututarajii kauli yoyote inayoashiria utimamu wa akili au ukweli wa nafsi toka kwako. Endelea kusifia hilp Bunge na wabunge majambazi ya uporoji wa mamlaka ya wananchi. Tunafahamu kuwa hayo majizi ya maamuzi na mamlaka ya umma, yana majitu maovu mengine huku nje ambayo kazi yao ni kuyasifia hayo majizi ya haki za wananchi.

Wewe endelea kusimama na watu waovu, na sisi wengine hatutachoka kuusema ukweli kuwa Bunge limejaza majitu maovu, maporaji ya mamlaka ya wananchi. Mengine yalitangazwa tu kuwa ni wabunge, lakini hawakuwahi kupata hata kura moja, na mahakama kuu ilitoa hukumu kuwa majitu hayo ni batili kuwepo bungeni, lakini bado yameng'ang'ania.
 
Tatizo wewe huna weledi wa aina yoyote.

Zipo kanuni za Bunge za kuwahoji na kuwawajibisha watu wanaotoa taarifa za uwongo kuhusu Bunge na wabunge. Kama Mbowe ni mwongo, unadhani ni kwa nini Mbowe hajaitwa kuhojiwa na Bunge kama kanuni zinavyoelekeza?

Wewe tunakutambua. Hututarajii kauli yoyote inayoashiria utimamu wa akili au ukweli wa nafsi toka kwako. Endelea kusifia hilp Bunge na wabunge majambazi ya uporoji wa mamlaka ya wananchi. Tunafahamu kuwa hayo majizi ya maamuzi na mamlaka ya umma, yana majitu maovu mengine huku nje ambayo kazi yao ni kuyasifia hayo majizi ya haki za wananchi.

Wewe endelea kusimama na watu waovu, na sisi wengine hatutachoka kuusema ukweli kuwa Bunge limejaza majitu maovu, maporaji ya mamlaka ya wananchi. Mengine yalitangazwa tu kuwa ni wabunge, lakini hawakuwahi kupata hata kura moja, na mahakama kuu ilitoa hukumu kuwa majitu hayo ni batili kuwepo bungeni, lakini bado yameng'ang'ania.
Acheni porojo ,narudia tena acheni uzushi.kama una ushahidi weka hapa jukwaani na siyo kuzusha vitu vya uongo kutafuta umaarufu wa kijinga na kishamba hasa baada ya kuona chama Chenu kimepuuzwa na watanzania.kutokana na kukosa sera na ajenda zenye kugusa maisha ya watu.
 
Tatizo wewe huna weledi wa aina yoyote.

Zipo kanuni za Bunge za kuwahoji na kuwawajibisha watu wanaotoa taarifa za uwongo kuhusu Bunge na wabunge. Kama Mbowe ni mwongo, unadhani ni kwa nini Mbowe hajaitwa kuhojiwa na Bunge kama kanuni zinavyoelekeza?

Wewe tunakutambua. Hututarajii kauli yoyote inayoashiria utimamu wa akili au ukweli wa nafsi toka kwako. Endelea kusifia hilp Bunge na wabunge majambazi ya uporoji wa mamlaka ya wananchi. Tunafahamu kuwa hayo majizi ya maamuzi na mamlaka ya umma, yana majitu maovu mengine huku nje ambayo kazi yao ni kuyasifia hayo majizi ya haki za wananchi.

Wewe endelea kusimama na watu waovu, na sisi wengine hatutachoka kuusema ukweli kuwa Bunge limejaza majitu maovu, maporaji ya mamlaka ya wananchi. Mengine yalitangazwa tu kuwa ni wabunge, lakini hawakuwahi kupata hata kura moja, na mahakama kuu ilitoa hukumu kuwa majitu hayo ni batili kuwepo bungeni, lakini bado yameng'ang'ania.
Unampigia mbuzi gita
 
Mnapenda Sana kupika uongo na uzushi pasipo ushahidi wa aina yoyote ile. Mbowe alifanya kutafuta sifa tu kwa watu kwa kuzungumza vitu vya uongo na uzushi. Nenda kamwambie akupatie ushahidi ili uje uweke hapa jukwaani na siyo kupiga porojo na mihemuko tu.msifikiri Watanzania ni wajinga wa kumeza na kukariri kila kitu bila kuchuja.inawezekana mbowe alijuwa anaongea na wanachama wake wa CHADEMA ambao amezoea kuwadanganya,kuwaswaga kama makondoo na kuwachukulia hawana akili kama manyumbu.
Lucas,

Tutumie mfano mdogo tu wa kutumia akili ya kawaida.
Kila raia wa Tanzania na mlipa kodi anawajibika kuhakikisha kodi yake na pesa nyingine ya uma inatumika vizuri.
Pesa za uma ni mali ya wananchi na siyo ya serikali au viongozi (wengi ambao ni chawa, wajinga au waovu hupotosha kuwa ni ya Rais). Hata Rais mwenyewe hajawahi kusema pesa za uma ni zake.
Sasa wewe kama mmiliki mwenye akili wa pesa hizo, ukipata taarifa kuwa zimeibwa au zinatumiwa vibaya, utachofanya ni kuitisha ripoti ya matumizi au unambishia mtoa taarifa?
Chama Cha Mapinduzi na taifa kwa ujumla (vikiwemo vyama vya upinzani) tunahitaji watu wenye akili kujenga hoja zenye mantiki na siyo kubishana kipumbavu.
Chama, serikali na bunge siyo magenge ya wahuni yanayohitaji utetezi wa uongo uongo au uhuni bila kutumia akili.
Kama taasisi hizo zikifanya makosa (ambayo ni ya kibinadamu), ufafanuzi na marekebisho hufanywa kwa weledi.
Hii ni kwa faida ya wote, kuanzia kizazi hiki na vijavyo.
 
Tanzania Kuna kusanyiko la wajinga lenye jina la "Bunge".Ndani kumejaa vilaza na mazuzu wasio jua hata majukumu Yao.

Wenye Akili timamu,wasipo jishughulisha na mambo ya msingi katika taifa lao,mwisho hutawaliwa na wajinga.
 
Acheni porojo ,narudia tena acheni uzushi.kama una ushahidi weka hapa jukwaani na siyo kuzusha vitu vya uongo kutafuta umaarufu wa kijinga na kishamba hasa baada ya kuona chama Chenu kimepuuzwa na watanzania.kutokana na kukosa sera na ajenda zenye kugusa maisha ya watu.

Wewe ndiyo maana kila mwenye akili amekuweka kwenye kundi la hamnazo. Mwombe msemaji wa Bunge akuletee vielelezo vya kuonesha wabunge bado wanalipwa 13m ya awali.
 
Tanzania Kuna kusanyiko la wajinga lenye jina la "Bunge".Ndani kumejaa vilaza na mazuzu wasio jua hata majukumu Yao.

Wenye Akili timamu,wasipo jishughulisha na mambo ya msingi katika taifa lao,mwisho hutawaliwa na wajinga.

Ndiyo kinachotokea Tanzania. Watu ama wenye uwezo mdogo wa akili au wasio na akili kabisa wanawatawala wenye akili.
 
Back
Top Bottom