Nape avuna aibu SAUT Mwanza (picha)

Nape avuna aibu SAUT Mwanza (picha)

Ndugu, Waache waendelee kujidanganya huku wakifarijiana na propaganda za kibavicha. CCM imeishamaliza kazi yake SAUT tawi la Mwanza na sasa inasonga mbele.

Hawa vijana wanachofanya ni kuuguza majeraha ya kisiasa kwa kufarijiana katika mlengo wa kilaghai.

Maneno matupu hayavunji mfupa.

CCM ilithubutu, ikaweza na sasa inatenda.

Ni hekima tu ya viongozi wa cdm amani inaendekea kuwepo. Tunajua mlisha amua kutumia nguvu badala ya hoja; kupiga badala ya kujibu nini umeulizwa....matamko yenu yapo ktk black books za wapigania haki za binadamu. Si muda mlefu mtajibu hayo the Hague, mfano ni Hutto Wiliam wa Kenya.
 
Ccm bila kulindwa na dola haiwezi kuendelea kutawala kamwe! Wakuu wa wilaya, wakuu wa miko, na hata wakurugenzi wote mbele ya ccm hawakohoi! Ccm ni chama dola!
 
Viwanja vingi Tanzania ni mali ya ccm. Unalalamika mlinyimwa kiwanja na ccm wakapewa!!! Mpaka leo cdm hawajenga
hata Makao Makuu ya chama, unataka tuwape kiwanja ili muwadanganye raia??? Tafuteni vya kwenu. Kule Arusha kuna
sehemu cdm walikuwa wanapenda kukutana (NMC) na kuanzisha vujo ule uwanja serikali ya ccm iliwapa raia wafanyie biashara,mpaka leo cdm hawana sehemu ya kukutania tena.

Sasa wewe unalalamika nini?? Wenzio wa Arusha mpaka leo hawajui wafanye nini kwakuwa ccm ilichukua mali yake, fanya
utafiti dogo usikimbilie kuandika tu. USHAURI ni bora ujitahidi umalizie masomo yako kuliko kushindana na ccm na watu
wake ambao wamekuzidi elimu,,CCM ipo kila siku utachoka na utapoteza muda wako na kibaya zaidi utapoteza future yako.

ww tuambie baada ya mwaka 1992 CCM haijawahi kujenga uwanja wowote inamiliki viwanja ilivyopora na endapo watapoteza dola viwanja itabidi virudi kwa wananchi kupitia halmashauri.
 
kumbe muanzisha mada ndio alie pata kipigo? Ushauri wa bure kijana, fata elimu na achana na siasa lasivyo utashinda vijiweni mchana kutwa unaota jua.
 
kumbe mkutano ulidoda namna hiyo ? Sasa wale waliokuwa wanatuongopea kwamba NAPE APOKEWA KISHUJAA walikuwa na maana gani ? Ukiona wahudhuriaji wote wamevaa sare , basi jua huo mkutano ni magumashi tu !

sauti wanajitambua hawawez kwenda kumshangaa mbwa akibweka hovyo, eti wao wakimwona anavyobwatuka wao ndio wanaona nikishindo, akili fupi
 
Ni hekima tu ya viongozi wa cdm amani inaendekea kuwepo. Tunajua mlisha amua kutumia nguvu badala ya hoja; kupiga badala ya kujibu nini umeulizwa....matamko yenu yapo ktk black books za wapigania haki za binadamu. Si muda mlefu mtajibu hayo the Hague, mfano ni Hutto Wiliam wa Kenya.
Ndugu, viongozi wa CHADEMA wana hekima gani?.

Nani alikuambia amani ya Taifa letu inashikiliwa na viongozi wa CHADEMA.

Eti tutajibu the Hague. Ndivyo ulivyodanganywa na hawa wanasiasa walaghai unaodai kama siyo hekima yao, kwa sasa kungekuwa na hakuna amani.

Andiko lako linadhihirisha umelaghaika kweli kweli. Pole sana!.
 
Kuleta mabadiliko ktk jamii inahutaji kujitolea,pole sana kijana husiogope wala kukatishwa tamaa na hayo yaliyo kupata.
 
Aibu iko wapi wakati mevuna wanachama wengi kiasi kile ikiwemo rais wa wanafunzi na rais mstaafu wa wanafunzi?
 
Ndugu, viongozi wa CHADEMA wana hekima gani?.

Nani alikuambia amani ya Taifa letu inashikiliwa na viongozi wa CHADEMA.

Eti tutajibu the Hague. Ndivyo ulivyodanganywa na hawa wanasiasa walaghai unaodai kama siyo hekima yao, kwa sasa kungekuwa na hakuna amani.

Andiko lako linadhihirisha umelaghaika kweli kweli. Pole sana!.

We ndo umelaghaika au labda ni Nape kwa ID tofauti. Wanaokwenda THE HAGUE huwa wanaamua wo wenyewe? Kuna siku ntavujisha waraka fulani hapa kuhusu haki za binadamu, kama hutatetemeka! Wakati unakuja ndg jiandae.
 
We ndo umelaghaika au labda ni Nape kwa ID tofauti. Wanaokwenda THE HAGUE huwa wanaamua wo wenyewe? Kuna siku ntavujisha waraka fulani hapa kuhusu haki za binadamu, kama hutatetemeka! Wakati unakuja ndg jiandae.
BAVICHA at its best.

Unamtisha nyani?. Akili yako ni sawa na akili ya viongozi wako wa CHADEMA wanaodai wana mkanda wa video wa mauwaji ya raia Arusha lakini wakiambiwa watoe hata photo na kuionyesha kwenye jamii eti wanadai wataonyesha tu pale tume ya kimahakama itakapoundwa.

Na wewe unaleta hapa akili hiyo hiyo ya kusema kuna siku utaweka hapa waraka kuhusu haki za binadamu. Kwani ukiweka kwa sasa nani atakufahamu wakati hata ID yako ni unverified user. This is fun!.

Tatizo wazee wa CHADEMA wamewapeni kazi ya propaganda lakini uwezo wenu uko chini sana katika kupembua masuala mbali mbali.
 
Atumia asilimia 90 ya hotuba yake kuwashambulia dr Slaa,Lissu ,CDM na UKAWA,
mkutano wake wasogezwa mbele ili kuwasubiria watu wafike uwanjani
Magari yasomba watu kutoka nje ya SAUT baada ya wanafunzi wa SAUT kutojitokeza uwanjani hapo
Awafanisha upinzani na vichaa,asema yeye alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi bora 3 waliofaulu kati ya 100 Bukumbi primary

Katibu wa itikadi na uenezi taifa wa CCM jana alijikuta anavuna aibu ya mwaka pale alipojikuta anahutubia watu waachache tofauti na gharama zilizotumika na malengo ya mkutano huo,kwani kwa mujibu wa taarifa za awali zilizotolewa na uongozi wa CCM tawi la SAUT Mwanza,walisema wamemwandalia mkutano huo kwa ajili ya kuja kuongea na wasomi wa chuo kikuu cha mtakatifu Agustino (SAUT) tawi la Mwanza pamoja na kuwa mgeni rasmi katika mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa CCM chuoni hapo,awali mkutano huo ulikuwa uanze saa 8 kamili za mchana lakini ulilazimika kuchelewa kuanza na kusogezwa mbele mpaka saa kumi na dakika 27 jioni kutokana na kukosa watu,kwani mpaka kufikia saa 9 za mchana watu walikuwa wachache sana hali iliyowalazimu CCM SAUT kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa kuanza kuratibu zoezi la kuhamasisha watu wasombwe na magari kutoka kwenye matawi mengine yaliyoko mjini Mwanza.

Mara baada ya magari kadhaa kusomba watu,iliwalazimu pia kukodisha vikundi vya maigizo na mziki wa asili kuja kutoa burudani ili kuwavuta wananchi wafike uwanjani hapo,zoezi ambalo kimsingi nalo lilikwama kwa kushindwa kuzaa matunda hali iliyopelekea katibu huyo mwenezi wa CCM kuanza kuhutubia hivohivyo kwa watu wachache,ikumbukwe kuwa awali zilivuja taarifa ya Nape kupitia serikali ya wanafunzi chuoni hapo kuchinja ng'ombe 3 na mbuzi 10 usiku wa kuamkia siku ya mkutano huo,

Bwana Nnauye alijikuta akitumia zaidi ya asilimia 90 kuwashambulia na kuwaongelea wapinzani hasa Dr Slaa,Lissu ,CHADEMA na UKAWA,hali iliyowakera wasomi wachache waliofika mkutanoni hapo na baadhi ya raia wakazi wa maeneo jirani na chuo,wakiongea kwa masharti ya kutotajwa majina wasomi na raia hao walihoji faida ya mkutano ule kwa wanafunzi na raia wanaoishi maeneo jirani na chuo hicho kwamba hawakuona tija ya mkutano ule kwani walitegemea kma kiongozi wa chama tawala angeongelea masuala mbalimbali ya kitaluma yanayowakabili wanafunzi na mfumo wa elimu kwa ujumla,huku kukiwa na taarifa kwamba kuna baadhi ya maeneo ya chuo hicho hayana huduma ya maji takribani mwezi 1 sasa,walisema hawakwenda pale kuambiwa habari za dr Slaa wala UKAWA,bali walikwenda pale kusikiliza sera na majibu ya kero zao zinazowakabili,nao raia waliokuwa wakitoa maoni baada ya mkutano walisema walishangazwa na namna Nape alivyotumia mda mrefu kuwaongelea wapinzani huku akiacha kuzungumzia kero yao ya mda mrefu ya migogoro ya ardhi eneo la Luchelele ambapo vigogo kadhaa wa CCM na serikali wamejimilikisha mapande makubwa ya ardhi huku wakiwafukuza wakazi wazawa wa eneo hilo.

AWAFANANISHA WAPINZANI NA VICHAA

Wakati akiendelea kuhutubia,mara mara alisikika akiwaita wapinzani ni vichaa huku akiunga mkono wapinzani kunyimwa uwanja huo kufanyia mkutano wa siasa kwa madai kwamba hawana sera zaidi ya kutaka kuwaambukiza wasomia pia aliendelea kusema CCM ni chama dora wanauwezo wa kufanya lolote kwa wakati wowote huku akisema serikali yote kwa mfano ipo pale,miongoni mwa viongozi wa serikali waliokuwepo pale huku wamevaa mavazi rasmi ya chama cha Mapinduzi ,bwana Nape aliendelea kuwapolomoshea wapinzani matusi na kashfa kwa kusema "kale kababu kameshajichokea,kameshakuwa kalemavu wa mkono kapumzike ili sisi vidume tupige kazi"

VURUGU ZA ZUKA /MWANAFUNZI WA SAUT AKAMATWA
Mwanafunzi wa mwaka wa 3 anaesomea masomo ya mawasiliano ya umma chuoni hapo Nicholaus Kilunga,alijikuta akipigwa na walinzi wa CCM na wanaCCM na baadae kukamatwa na polisi kwa kosa la kumtaka Nape azungumzie ufisadi wa bilioni 200 za IPTL kupitia kwenye account ya Escro,mwanafunzi huyo alishikiliwa kwa zaidi ya saa moja hatua iliyopelekea wanachama wa CDM SAUT kuanza kukusanyika kwa wingi kushinikiza mwenzao huyo aachiwe huru kwani hakuwa na kosa lolote,dalili za kutokea vurugu mkutanoni hapo zilianza kuonekana mapema hasa pale Nape alipokuwa akimponda dr Slaa kwamba anakuja kuwadanganya watu kwa maneno ya "people's "huku wanafunzi waliokuwa mkutanoni hapo kuitikia "powerr"hali iliyowakera CCM.

KAULI YA RAIS WA SAUT YAZUA UTATA NA KUWAGAWA WANAFUNZI
Katika hatua nyingine leo chuoni hapa kumezuka sintofahamu na kuongeza hali ya uhasama na sintofahamu kufuatia kauli aliyoitoa rais wa serikali ya wanafunzi wa chuo hicho mkutanoni jana ndugu Philibert Saimo,pale alipokaribishwa awasalimie wageni na watu waliofika kwenye mkutano huo,huku akiambatana na makamu wake wa rais,waziri mkuu,spika wa bunge la wanafunzi chuoni hapo na waziri wa michezo alitamka maneno haya"Nimeamua kujiunga na CCM,kwa wale wote ambao hawataki kuongozwa na rais ambaye ni mwanachama wa CCM,wale wasio wa CCM na wale wanaoipinga CCM chuoni mjiandae kuhama chuo"kauli ambayo imezusha sintofahamu chuoni hapa hasa ikizingatiwa kwamba kiongozi wa serikali ya wanafunzi hapaswi kujihusisha na vikundi vyenye mlengo wa kidini,kikabila na kisiasa huku ibara ya 53 ya sheria zinazoongoza vyuo vikuu ikikataza siasa kufanyika vyuoni,wanafunzi wengi wameutaka uongozi wa chuo hicho umchukulie hatua kwani hakuchaguliwa na wanaCCM pekee wala kuchaguliwa awahudumie CCM pekee,wakiendelea kusema kwa wale wasiokuwa na vyama vya siasa ama wale wanafunzi wafuasi wa vyama vya upinzani hawatakuwa huru kwenda kupata huduma kwenye serikali hiyo,
Na alipotafutwa na kuhojiwa juu ya kauli yake hiyo,rais wa chuo hicho bwana Saimon alisema yeye anahaki ya kujiunga na chama chochote cha kisiasa,na kwamba pamoja yeye kuwamwanaCCM atahudumia watu wote bila kujari vyama vyao,katika mkutano huo jumla ya wanachama 2 walijiunga na CCM wakitokea CDM nao ni rais wa mwaka jana chuoni hapo bwana Dovakamwene Mcheshi na huyu rais wa sasa Philibert Saimon.
View attachment 163826View attachment 163826View attachment 163828View attachment 163831View attachment 163832View attachment 163859











Hii mijibwa tu!! iko siku watajificha chooni!! subirini wapuuzi wakubwa!!
 
Huyo rais aliyejipendekeza kuhamia CCM mpige chini hana mvuto tena wa kukiongoza chuo km SAUT. Anajipendekeza akidhani baadae anaweza kupata ulaji hakuna jingine. Lakini akaulize rais wa wanachuo wa mwaka 2006/2007. Anaitwa Revocatus Kassimba tulivyomshikisha adabu baada ya kujipendekeza kwa wakina masha, na aulize huyu bwana yuko wapi mpk sasa km sio kuishia kuwa afisa habari wa mkuu wa mkoa huko ruvuma na anakaa mtaa wa wahuni wa mfaranyaki.
 
asema yeye alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi bora 3 waliofaulu kati ya 100 Bukumbi primary
Hivi kufaulu kwa Nape kwenda shule za kata ilikuwa ni achievement kubwa sana maishani mwake tena miaka ya 90?? Ningemuelewa kidogo kama ingekuwa miaka ya 70 au 80 (Mtoto akifaulu anafanyiwa party) kabla secondary school za kata hazijaanza!!
 
Huyo rais aliyejipendekeza kuhamia CCM mpige chini hana mvuto tena wa kukiongoza chuo km SAUT. Anajipendekeza akidhani baadae anaweza kupata ulaji hakuna jingine. Lakini akaulize rais wa wanachuo wa mwaka 2006/2007. Anaitwa Revocatus Kassimba tulivyomshikisha adabu baada ya kujipendekeza kwa wakina masha, na aulize huyu bwana yuko wapi mpk sasa km sio kuishia kuwa afisa habari wa mkuu wa mkoa huko ruvuma na anakaa mtaa wa wahuni wa mfaranyaki.


Hata huyu tuanaangalia katiba ya chuo,standing order na student by law vinasemaje ili awajibishwe
 
Ndugu, viongozi wa CHADEMA wana hekima gani?.

Nani alikuambia amani ya Taifa letu inashikiliwa na viongozi wa CHADEMA.

Eti tutajibu the Hague. Ndivyo ulivyodanganywa na hawa wanasiasa walaghai unaodai kama siyo hekima yao, kwa sasa kungekuwa na hakuna amani.

Andiko lako linadhihirisha umelaghaika kweli kweli. Pole sana!.


Katibu mwenezi umepanic baada ya kusikia mahakama itakuhusu?hata ikichukua miaka 100 wahalifu wa kivita,mauaji ya haraiki,mateso na vifo vya watu wasio na idadi mtatafutwa na kuhukumiwa hata kma mtakuwa tayari vibabu,so endelea kujifariji
 
Tunatambua kuwa alilipwa milioni tano kwaajili ya kampeni za kuwania urais wa chuo hicho, baada ya kushinda akapewa milioni saba ili ahame chama, na kisha ameahidiwa uafisa elimu wilaya kulingana na masomo anayosomea,

Shukrani kwa Chadema Saut baada ya kubaini kijana ameasi chama walimfukuza uanachama yeye na vibaraka wake wengine.

Hivyo Nape Nnauye kaja kuchukua makapi.
 
Last edited by a moderator:
Njaa ishapiga hodi hadi kwa wasomi, hii ni balaa kwa ustawi wa taifa.
 
Ndugu, Waache waendelee kujidanganya huku wakifarijiana na propaganda za kibavicha. CCM imeishamaliza kazi yake SAUT tawi la Mwanza na sasa inasonga mbele.

Hawa vijana wanachofanya ni kuuguza majeraha ya kisiasa kwa kufarijiana katika mlengo wa kilaghai.

Maneno matupu hayavunji mfupa.

CCM ilithubutu, ikaweza na sasa inatenda.


maneno yenu tumeyazoea sana bt kamwe huwezi kuzuia ukweli,kwani ukweli ni kama boya hata ulizamishe vipi litaibuka tu
 
Back
Top Bottom