Nape avuna aibu SAUT Mwanza (picha)

Nape avuna aibu SAUT Mwanza (picha)

Wanafunzi wabaya nyie, licha ya kula ming'ombe na mijimbuzi mwisho wa siku mnalala CHADEMA!!

Pole ndugu yangu Nnauye, ndio siasa hiyo hata hao kiduchu watafikisha ujumbe kwa wenzao.

yes mkuu nyama zililiwa bt watu wakaendelea kujisomea majumbani mwao kujiandaa na UE
 
Huwa natafakari CCM imejikwaa wapi mpaka kuwa na viongozi kama Nape na Mwigulu! Chama kikongwe Afrika chawezaje kuongozwa na watu hawa? Hivi Nape anawezaje jujenga hoja za kisiasa akiwa kama katibu mwenezi katika wakati ambao vyama vya upinzani vina vijana wenye upeo mkubwa wa masuala ya kisiasa. Nawazungumzia Julius Mtatilo, John Mnyika, Ismail Jusa na wengine wengi.... kuna wakati huwa nahisi aliefanya uteuzi wa Nape na Mwigulu alikuwa na njama za kukiangamiza chama hiki kikongwe... kuna hasara nyingi CCM inapata kwa kuendelea kuwa na viongozi hawa wasio na uwezo wa kujenga hoja zaidi ya kutoa matusi na vitisho kwa vyama vya upinzani...kuwa na viongozi ambao wanahusishwa na matukio yenye sura ya kigaidi ni kukihujumu chama! CCM yenye wanachama kama Mzee Warioba,Mzee Butiku,Salim Ahmed Salim,Cleopa Msuya, Edward Lowasa, Mzee Mwinyi,Ben Mkapa,pius Msekwa,Samwel Sita,Dr Shein na wengineo wengi kuongozwa na kina Nape Nauye na Mwigulu Nchemba ni kukihujumu chama! Nina amini kila wanakopita hawa vijana badala ya kuwavutia watu,huwa wanawaudhi watu. Itahitajika kazi ya ziada kuijenga upya CCM.
 
Viva kwa vijana wa SAUT mliojiunga na ccm. Tutawalinda popote pale mtakapokuwepo,
ccm ndio wenye serikali tutakuwa na nyie mpaka mtakapo maliza chuo. Mlinifurahisha sana na Mh Nape ana
matumaini makubwa na nyie.

Huna tofauti na zuzu!
 
Kwa Kipigo ulichopata lazima povu likutoke sana...hiyo ndio ccm mkuu!! Na bado
Kweli kabisa hiyo ndio ccm mabibgwa wa kuteka na kupiga subirien kihama chenu mafirahuni makubwa nyie moto wa chadema hamuuwezi endeleen kuwavia hao hao UDP and co.
 
mkuu nicholaus kilunga big up sana ume onyesha uzalendo mkubwa sana.usife moyo haya ni mapambano ya kumtoa mkoloni mweusi siku si nyingi tutafika nchi ya ahadi.
hawa magamba wanajiona nani..nape kashindwa jibu swali wanaamua pigana na kupiga watu.sasa ndio wamechokoza..hawajui kuwa sasa hivi pale pembamba pa kamba pako very tense na tayari sauti zakukatika zimeshaanza sikika.
 
Last edited by a moderator:
Kwa Kipigo ulichopata lazima povu likutoke sana...hiyo ndio ccm mkuu!! Na bado
Ndugu, Waache waendelee kujidanganya huku wakifarijiana na propaganda za kibavicha. CCM imeishamaliza kazi yake SAUT tawi la Mwanza na sasa inasonga mbele.

Hawa vijana wanachofanya ni kuuguza majeraha ya kisiasa kwa kufarijiana katika mlengo wa kilaghai.

Maneno matupu hayavunji mfupa.

CCM ilithubutu, ikaweza na sasa inatenda.
 
Viva kwa vijana wa SAUT mliojiunga na ccm. Tutawalinda popote pale mtakapokuwepo,
ccm ndio wenye serikali tutakuwa na nyie mpaka mtakapo maliza chuo. Mlinifurahisha sana na Mh Nape ana
matumaini makubwa na nyie.

Nawapa pole kwa kuvua utu na kuvaa unyani.
 
Kwi kwi kwi kwi kwi lol!!! Akawaombe wenye mabilioni yao kule uswiss wamkatie kidogo ili katika ziara zao kuzunguka nchi waangushe ng'ombe watatu, mbuzi watatu, kondoo watatu na kuku kama 200 hivi na mpunga gunia 10.

kuhusu madai ya kuchinja ng'ombe Nape alisema angekuwa na uwezo zaidi angegawa ng'ombe zaidi
 
Ni aibu kubwa kwa kijana Nape Nauye kuchumuia tumbo kwa maslahi binafsi...hizi njaa ni mbaya sana
 
CCm ni manyang'au na ni chama cha kimagumasi hasa baada ya wahuni (Nepi) kupewa uongozi na bado kinajifia hiki kikundi cha wevi na majangili
 
hizi ni dalili za kukata tamaa kimaisha, kufanya fujo ya makusudi kwenye halaiki ili upigwe ukamatwe upate kisingizio cha kushindwa shule. akina moses machali na ezekiel wenje hawakuwa wajinga wajinga kama hawa.
 
Viwanja vingi Tanzania ni mali ya ccm. Unalalamika mlinyimwa kiwanja na ccm wakapewa!!! Mpaka leo cdm hawajenga
hata Makao Makuu ya chama, unataka tuwape kiwanja ili muwadanganye raia??? Tafuteni vya kwenu. Kule Arusha kuna
sehemu cdm walikuwa wanapenda kukutana (NMC) na kuanzisha vujo ule uwanja serikali ya ccm iliwapa raia wafanyie biashara,mpaka leo cdm hawana sehemu ya kukutania tena.

Sasa wewe unalalamika nini?? Wenzio wa Arusha mpaka leo hawajui wafanye nini kwakuwa ccm ilichukua mali yake, fanya
utafiti dogo usikimbilie kuandika tu. USHAURI ni bora ujitahidi umalizie masomo yako kuliko kushindana na ccm na watu
wake ambao wamekuzidi elimu,,CCM ipo kila siku utachoka na utapoteza muda wako na kibaya zaidi utapoteza future yako.

Hujui hata unachoongea wewe.
CCM wana kiwanja au Mali IPI?
Yooote ni Mali ya wananchi, kama wangekuwa wanajiweza ilitakiwa iwe kwamba ktk mfumo wa vyama vingi kila chama kianze from the ground root. Mali zoote mnazosema ni za CCM sii kweli hizo ni Mali za wanachi ambazo zilichangiwa na wananchi wenyewe kipindi cha mwalimu wakati wa CCM yajenga nchi chini ya mfumo wa chama kimoja.
Kunielewa hapa itakuwa ngumu kwa sababu sidhani kama utaelewa dogo
 
Jana Nape alikuja hapa akadanganya bila aibu eti wanafunzi 400 walijiunga Ccm. Nikamuuliza inawezekanaje wakati waliohudhuria hawafiki 400? Sasa picha hizo hapo, Nape arudi atwambie kama watu hao wanafika 400!

Viongozi wa chama tawala wasipoona shida kudanganya ni hatari! Ndiyo maana wananchi hawajui ni lini wawaamini, ni wakati gani mnafanya propaganda na lini mnasema ukweli! Ninyi si saizi ya kuongoza Ccm na sijui kama kuna mtu mnamvutia kuingia kwenye chama zaidi ya watu kukimbia!
 
Back
Top Bottom