Tangu ilipokuwa imetolewa ratiba ya kutangaza nia ya urais nimekuwa nikimsikiliza kila mtangaza nia ya urais laikini kuna mambo kadhaa mimi binafsi sija ya elewa.Nitayaeleza machache kama ifuatavyo.
1.Wapo waliojinadi kukomesha RUSHWA na UFISADI, lakini hawajatuambia kama mafisadi Tanzania wapo au hawapo;kama ni wapo ni akina nani? na kwa nini mpaka leo hawajukuliwa hatua? kwa sababu baadhi ya hao watangaza nia mawaziri au nyadhifa nyingine serikalini au ni wastaafu ambapo walikuwa na nafasi ya kumsaidia rais kukomesha hiyo hali.
2.Kwa wale walioko kwenye nyazifa zao bado au wanafanya hivyo kumuhujumu rais wao aonekane ameshindwa? au wametunza hayo matatizo kwa makusudi ili iwe ndiyo gia ya kuomba urais?
3.Baadhi yao tunawaona kule bungeni kwa nguvu zote wakitetea UFISADI leo wanakuja na wimbo huo huo kuutaka urais;hivi wanatufanya watanzania ni watu tusiyo na fikra?
4.Baadhi ya wataka nia ni Mawaziri waandamizi na wastaafu ambapo mikataba yote mibovu inayolinyonya taifa imefanyika wao wakiwa madarakani;sisi tutawaaminije kuwapa nchi tena kwa mara ya pili?
5.Baadhi ya watia nia tunaona kabisa huku mikoani jinsi wanavyotumia fedha nyingi kukodi watu,lakini wanadai ni za marafiki zao,hao marafiki zao malipo yao ni nini baada ya kupata urais? je, hao marafiki ni wa ndani au wa nje?
6.Baadhi yao wamemshauri vibaya kabisa rais kiasi cha kutumia pesa nyingi katika katiba na katiba haijapatikana;je hao ndiyo wanafaa kupewa urais?
7.Wapo wanaojinadi watafanya maamuzi magumu wakipewa urais;lakini hawasemi ni aina gani ya uamuzi mgumu amabao wataufanya kama katika viwanda,elimu,ulinzi,kilimo,mi undombinu nk; na wengine bado wako kwenye nafasi hizo lakini hawawahi hata kushauri rais afanye hivyo; je leo ndiyo wataweza wakipewa urais?
MAONI YANGU:
Watanzania sasa wanataka rais anayeweza kushughulikia maswala yanayo mgusa mwananchi moja kwa moja siyo porojo.
1.Mfumo wa elimu ni mbaya kabisa hauandai mhitimu kujiajiri
2.Ardhi ni kilio cha watu kila kukicha,wanyonge wanaporwa ardhi viongozi wakok kimya
3.Mazao ya wakulima yanaoza majumbani
5.Afya mbaya.watu binafsi maduka yao yana dawa,serikali hakuna
6.Barabara za halmashauri zetu ni mbaya na kama zina jengwa ni kwa chini ya viwango
7.Kodi watu hawalipi,wameachiwa watumishi,serikali iko kimya
8.Maji safi na salama hakuna.maeneo mengine mto mkubwa upo chini ya km 50 na makazi ya watu lakini watu hawana maji ya bomba,
Haya ni machache tu lakini watia nia haya hata hawasemi.
Mungu ibariki TANZANIA