Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 876
Sijui bwana
Alisema wazee wanasubiri kufa akajisahau yeye ni mwanadamu ambaye awezi kuona kesho, sasa kavunjika na wazee bado wanapeta....
Pole zake, na akome kutukana wakunga wakati uzazi ungalipo hujafa hujaumbika, alikuwa akifanza nini?
Pole zake, ila huo mwili haoufai kwa kijana anaejitambua.
Huwezi kunenepeana kama mtu asiekuwa na majukumu.
Kijana wa kileo?
Tena muenezi wa chama tawala?
No.
yaniniiNampa pole.
....
katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) Taifa Nape Nnauye apatwa na majanga mkoani Iringa baada ya kuanguka na kuteguka mkono wake wa kulia wakati wa mchezo wa kirafiki kati ya timu ya msafara wa Kinana na Veteran mjini Iringa.
Tukio hilo limetokea mapema asubuhi ya leo na hivyo kulazimika kukimbizwa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa kwa matibabu zaidi.
![]()
![]()
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa
Mwembetogwa mjini hapa Nape ambae alikuwa amefungwa mkono wake alisema amepatwa na tatizo hilo leo asubuhi baada ya kuanguka uwanjani japo mbali ya kuanguka alisema hajaweza kuacha kupanda jukwaani kuwaeleza wananchi wa Iringa mjini juu ya mbunge wao mchungaji Peter Msigwa( Chadema)
Kwani alisema ni lazima mbunge Msigwa aondoke katika jimbo hilo baada ya kushindwa kuwatumikia vema wananchi wa jimbo hilo na kuendelea kuwaletea mabalaa mbali mbali .
Nape pia ametumia nafasi hiyo kutaja ahadi lukuki za mbunge Msigwa ambazo alipata kuwaahidi wananchi pasipo kuzitekeleza katika jimbo hilo.
note: Ukipambana na Chadema unapambana na Mungu !!!
" If Obama wants me to allow Gay Marriage in Zimbabwe I should marry him first to show good example"-Robert Mugabe.kWA POST HII I CAN RATE you,Labda huyu ndio Mungu wako.Mungu gani huyo kwenye Masanduku ya kura kila Uchaguzi kura hazitoshi, Mungu gani anaedai kuibiwa kura baada ya kushindwa " kuzilinda" aliepa kuandamana mpaka Bunge liahirishwe lakini akashindwa, Acheni kufananisha washerati wa akina Mukya na jina la Muumba wako na wangu