Nape akimbia nguvu ya Mnyika Ubungo

Nape akimbia nguvu ya Mnyika Ubungo

2hery

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2011
Posts
4,700
Reaction score
4,639
Habari wana jamvi,

Wakati joto la uchaguzi mkuu likiendelea kupamba moto imefahamika kuwa jimbo la ubungo wagombea wengi wameanza kuogopa nguvu ya JJ Mnyika ambapo sasa wameamua kutafuta majimbo mengine.

Mmoja wa wanasiasa ambae amekimbia moto wa Mnyika ni bwana Nape Nnauye ambae ameenda kujiandikisha kupiga kura Jimbo la Mtama Mkoani lindi,itakumbukwa kuwa mwaka 2010 kwenye kura za maoni za CCM Nape alishiriki kuomba ridhaa ya chama chake kupitia Ubungo na kushindwa na Shamsa Mwangunga.

Heko Mnyika juhudi zako kwa jimbo la Ubungo zimeoneka na chama tawala kimejianda kuwa chama pinzani.Naaomba UKAWA wazidishe kutoa elimu ya uraia hasa umuhimu wa kupiga kura hasa maeneo ya vijijini kama Mtama ili hata kile walichobakiwa nacho kipotee kabisa.

Nape na kadi yake Mtama

8.jpg

 
Majimbo ya mijini yanahitaji wachapa kazi na si wababaishaji.
 
Mwache akimbilie huko walikolala usingizi wa pono; siku wanakuja kustuka CCM walishajimilikisha rasilimali zao zote ikiwa ni pamoja na ardhi. Nape ni binadamu wa kushindana hoja na Mnyika!?
 
Hii inathibitisha @Nape anatumika na Membe na familia ya Magogoni kumwandama na kumtukana Lowasa kwa kuwa ni kikwazo kwa Membe na mali za nyumba kuu so wanataka Membe aje kuwa turubai lao!!!

cc MwanaDiwani TandaleOne
 
Last edited by a moderator:
Kwani Nape ni mwenyeji wa Mtama au Wanamtama wamekosa mbadala wa Membe na hivyo kumkodisha Mnauye?
 
Nape baba yake anatokea wilaya ya Busokelo na mama yake Singida. Wapi na wapi na Mtama kama sio kulipana fadhila za kumchafua mamvi...
 
Mwenye macho haambiwi tazama, kazi mnyika inaonekana. Mwanasiasa mwenye jina akijaribu kugombea ubungo, inakula kwake!
 
Nape kwake huu mwaka mbaya...akishinda lowassa analiwa kichwa, ikishinda ukawa the same... aisee kila kitu na mwisho wake
 
Nape baba yake anatokea wilaya ya Busokelo na mama yake Singida. Wapi na wapi na Mtama kama sio kulipana fadhila za kumchafua mamvi...

ni kweli kabisa alikulia kijiji cha Mwanga kule Iramba. huko anameenda kuachiwa jimbo na membe.
 
nape amekimbilia kwa ndugu zangu wa lindi ili akagombee ubunge. wana mtama kuweni makini sana.kumbukeni masuala ya gesi yetu.
 
Nape anataka kuwa mbunge wa gesi,ukawa elekezeni nguvu huko mtama tumwage vima
 
Halafu mbona sisi tuliandikishwa na NIDA hatukupewa vitambulisho hapo hapo...!? au mashine za NIDA nitofauti na mashine za BVR za Tume ya uchaguzi
 
Kuna mnyetishaji wangu kutoka chanzo makini mitaa ya Lumumba ameniambia CCM baada ya kuona jimbo la Ubungo limekuwa gumu mno, wameamuwa kumsimamisha msemaji mmoja wa timu fulani Tz yenye rangi kama ya chama ili kupata followers wa timu hiyo.
Siku ya kufa nyani miti yote huteleza.
 
Mwache akimbilie huko walikolala usingizi wa pono; siku wanakuja kustuka CCM walishajimilikisha rasilimali zao zote ikiwa ni pamoja na ardhi. Nape ni binadamu wa kushindana hoja na Mnyika!?

Acha kudharau na kukashifu binaadamu wenzako. Nyie wa kaskazini mna ubaguzi sana na dharau kwa watu wa kusini.
 
Kuna mnyetishaji wangu kutoka chanzo makini mitaa ya Lumumba ameniambia CCM baada ya kuona jimbo la Ubungo limekuwa gumu mno, wameamuwa kumsimamisha msemaji mmoja wa timu fulani Tz yenye rangi kama ya chama ili kupata followers wa timu hiyo.
Siku ya kufa nyani miti yote huteleza.

Mkuu Ubungo ni sehemu ngumu kwa mtu kuingia kichwa kichwa.Unapimwa kwa hoja na sio maneno mengi.
 
Sasa 'Joka la mdimu' akitoswa kwenye nafasi ya urais si watatoana macho na huyu bwamdogo?
 
Back
Top Bottom