Naona kama Wanawake wengi hawapiki chakula cha waume zao

Huyo sasa siyo mke ni mzigo, yani mke mama wa Nyumbani halafu anashindwa kumpikia mumewe kwa misingi ipi.
 
Mkuu unahudumia familia lakini au na wewe ndio wale wale wa maisha kusaidiana, kutaka Mkeo akusaidie majukumu yako ya kutafuta pesa na kuhudumia familia.
 
Huyo sasa siyo mke ni mzigo, yani mke mama wa Nyumbani halafu anashindwa kumpikia mumewe kwa misingi ipi.
Wanawake wengi ninyi ni mizigo kwenye mahusiano, maana iyo ni nature yenu, hata simlaumu huyo ndugu yangu Karma
 
Mkuu unahudumia familia lakini au na wewe ndio wale wale wa maisha kusaidiana, kutaka Mkeo akusaidie majukumu yako ya kutafuta pesa na kuhudumia familia.
Sijajua kwa wengine hao wanaume unao wazungumzia wewe, mimi wajibu wangu kwa mke wangu na watoto wangu naujua na nitamuoa yule nimtakae mimi na atakayekizi vigezo vyangu FULL STOP,hao wengine 50/50,wabeijing watawapata wenzao wakuumizana nao vichwa kwani kupanga ni kuchagua.
 
Wanaume wengi hatuna mda wa kusubiri chakula nyumbani,unakuta upo kwenye mishe nyingi au kazi za ofisini ,msosi wa nyumbani utakupotezea mda tu ,chai ya kusubiri,lunch mpaka iive tayari saa nane ,mwanamke anaweza kuanzia kupika kuanzia saa tano huko yeye anaonja jikoni we mwanaume mpaka usubiri msosi uive huna ham tena
 
Wengine unakuta wanaishi nyumba moja lakini hawana mawasiliano kila mtu na chumba chake.
 
Kaka ukioa na ukapata watoto usisahau feedback
 
Wengi hawapendi vyakula vya home, ukute mke hajui kupika vizuri, ili kuepusha ugomvi usio na lazima anakula kwanza nje kisha home anadonoa donoa tu
Nikigundua hili wa kwangu nitamuambia ajifunze mapishi kupitia youtube
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…