Naombeni ushauri

Naombeni ushauri

Kuna mpenzi wangu ambaye nampenda sana ambaye nina km mwaka1 hivi nipo nae anatabia poa tu lakini hivi karibuni kama 3week nikimpigia simu kama sa 5-6 nambiwa inatumika.

Then nikipiga zaid inakuwa haipatikani nikawa mpole kusuluisha yakaisha sasa tangu hapo anipigii simu hadi nimpigie, anitumii text had nimtumie.

Nahitaji ushari wenu nimfanye nini, nitumie njia gani naitaj furaha katika pendo langu.

Get ready for a broken heart.....
 
Kuna mpenzi wangu ambaye nampenda sana ambaye nina km mwaka1 hivi nipo nae anatabia poa tu lakini hivi karibuni kama 3week nikimpigia simu kama sa 5-6 nambiwa inatumika.

Then nikipiga zaid inakuwa haipatikani nikawa mpole kusuluisha yakaisha sasa tangu hapo anipigii simu hadi nimpigie, anitumii text had nimtumie.

Nahitaji ushari wenu nimfanye nini, nitumie njia gani naitaj furaha katika pendo langu.

Ukiona hivyo ujue kipele kimepata mkunaji mzuri. Wewe ni mwananfunzi tu.
 
profilepic150098_1.gif
 
du aya mapenzi balaa, kweli mapenzi nilize kama mashabiki wa brazil
 
Hapana kwanini??
Kuna njia nyingi nzuri na sahihi ambazo unaweza kuzitumia kwa mtu na kumfanya akueleze ukweli au ajifeel guilt kwa anachokufanyia kama ni kibaya lakini sio kutumia nguvu na ubabe .Na pia kila mtu ana uhuru na simu yake labda kuna makubaliano mmewekeana kuhusus simu. lakini kama sio noo mkuu kumpokonya simu sio suluhu
 
Pole mdogo wangu, hapo kuna mambo mengi yaliyowafikisha hapo. Sijui we ni jinsia gani hivyo nashindwa kuamua. Ila kama wewe ni mwanaume inawezekana ulimzoesha kwamba mawasiliano lazima wewe upige uulizie kama hajambo. Pia inawezekana huyo binti alikusubiria muda mrefu ueleze malengo ya kuwa naye ukawa kimya unamtumia kama toilet paper wakati umri wake unasogea na anahitaji kuwa na familia. Hiyo ni kusema kwamba matokeo unayoona sasa chanzo chake ni wewe. Unachopaswa kufanya sasa ni kuomba muda wake mkakae mahali mzungumze malengo ya mahusiano yenu na nini kinachomkera kwako na wewe umweleze mambo gani usiyopebda kwake. Usizungumze nayo hayo siku ya kumtafuna tu maana hamtazungumza kwa kina. Usithubutu kunyang'anya simu yake maana huyo si mkeo na hata angekuwa mkeo si vizuri kuingilia uhuru binafsi wa mtu. Kuna mambo lazima yabakie personal. Jifunze kujiepusha na mambo ambayo hutaweza kuyakabili moyoni siku ukiyafahamu. Pia ukikutana naye muelezane kwamba kujuliana hali ni wajibu wa kila mmoja wenu na pia mpeane moyo kwamba ujana mlionao leo unaisha punde mtakuwa wazee kwahiyo muwe makini na kila jambo mnalofanya na pia msijidanfanye kwamba mnapinda raha ya ujana.
 
perhaps ametingwa jaribu kumpa space mtafute pale utapokua na hitaji ambalo hakuna mtatuzi mwingine salaaam sijui kukumis kama yuko ocupied havina maana kwa sasa, kama sababu ni yuko ocupied itaisha with time atakutafuta kama ana sababu nyingine hatarudi hop utakua umejiadjust kuachana taratibu hiki kipindi unachompa space
 
nikwel unayosema kiongoz .mi ni mwanaume na nimejaribu kumweleza x kwa x na anaomba msamaha namsa mehe.ila cha kuskitisha had nimtext ndo ajibu.nimejaribu kumuuliza.hoja anataka amridhishe father wake kitabia zaid.nimejaribu x kwa x.lakin wap .nifanyaje
 
Back
Top Bottom