Katika maisha yangu haya ya miongo minne kasoro niliyoishi, na muongo mmj na nusu hv katika kuwajua wanawake, kuna mambo mengi sana niliyojifunza. Lakini kubwa kuliko nililojifunza na kulielewa vyema ni kuhusu mwanamke kutokuwa na ustahamilivu/Subra/Uvumilivu pindi mume/bwana wake anapokuwa amepata changamoto ya kipesa.
Wengi wanasema kuwa katika mahusiano/ndoa , isije ikatokea hata kwa bahati mbaya mwanamke akamzidi mwanamume kipato, hasa wanawake wetu wa ngozi nyeusi (African ladies to be precisely). Mara nyingi imekuwa ikileta shida sana.
Kwa asili wanasema mwanamke mi mtu wa kuhudumiwa/kupewa (don't get me wrong), na mwanamme ni mtu wa kutoa.
Sasa inapotokea circumstances mambo yakawa vice versa, basi mambo huwa kama alivyosema mtoa mada au hata pengine zaidi.
Ukitaka uthibitishe kauli niliyotoa hapo juu, angalia mfano huu: unakuta mwanaume anakazi au biashara nzr, wkt huo mwanamke anakaa home au ana kazi ya kawaida na kipato cha kawaida tu. Mwanaume atahudumia na kuitunza familia, atajenga nyumba ya kuishi, atanunua gari, atalipia watoto ada, ataitoa familia out, n.k (yote haya yakifanyika huku mke/mwanamke akipata special treatment klk pengine hata watoto au mama mzazi wa mwanaume).
Sasa itokee siku mwanaume kafukuzwa kazi au biashara imebuma, na mwanamke anaendelea na kijikazi chake cha mshahara wa laki 7, aisee dharau zitaanzia hapo, kukasirika kusikokuwa na sababu, maneno kibao kuwa majukumu ameachiwa yeye tu, manun'guniko kuwa mwanaume hafanyi chochote, unakuta hata mzigo hakupi, na mmb mengine kama hayo. Hii siyo kwa kila mwanamke lkn wengi wao, hasa hawa wa mjini ndy wako hvy.
Sasa tukirudi kwenye mada mezani, mtoa mada unatakiwa uelewe kuwa mwanaume asipokuwa na pesa mfukoni anakosa confidence, hajiamini, anachanyikiwa, n.k!
Lakini la muhimu kujua ni kuwa mwanaume ni ngumu na inaleta sana ukakasi kumuomba mwanamke pesa mara kwa mara hata kama ni mkeo, kwa asili iko hvy. Ukiona mwaname yuko comfortable kuomba omba pesa kwa mwanamke huyo ni Marioo na ma Marioo wengi huwa wanafanywa michezo mibaya.
NINI CHA KUFANYA?
Kaa chini na mwenzako, mjadili suala hili na mengine kama yapo, zungumza nae, ikiwezekana uwe unampa mwanaume/mume wako mamlaka na pesa zako, hii itasaidia sana kumrudisha mchezoni na kuleta amani ndani. Mpe yeye ashike awe anatoa kulingana na mahitaji yenu. Ikiwezekana pangeni bajeti kbs kisha awe anatoa yeye hy pesa. Kama unaona ni ngumu, basi mpe kiasi fln akae nacho mfukoni kilinde mfuko wake, usisubiri akuombe. Najua kwa wanawake wengi hili itakuwa ni ngumu, lkn niamini nacholwambia, itasaidia sana kuokoa ndoa yenu.
Pia jaribu, kuwa na kauli nzr kwa mumeo, kaeni chini na mlijadili hili kwa unyenyekevu mkubwa, naamini mtafikia muafaka kuwa karibu na Muumba wako, mshirikishe kwa kila kitu chako, appreciate, vile vyote vzr alivyokufanyia wewe personally km mke. Mwisho pesa muhimu kwenye mahusiano/ndoa lkn haijawahi kuwa kila kitu, kuna muda wanandoa wanahitaji Amani na upendo zaidi kuliko masuala ya kipesa.
Adios!