Naombeni ushauri wenu kwenye hili

Leejay49

JF-Expert Member
Feb 10, 2023
12,847
39,719
Habari wana jf,

Niende moja kwa moja kwenye mada, toka mwaka 2020 kuna mwanaume nilikua nampenda sana in short hata mahusiano yetu ni mimi ambaye nlichochea anitongoze.

Nilikua najua mahali alipokua anafanya kazi kwahiyo ilikua rahisi kwangu kumwekea mitego mpaka aliponitongoza mwenyewe.

Mwanzo wakati tunaanza mahusiano alikua akinipenda na kunijali sana, kiukweli nilikua nampenda sana na sikuwahi hata siku moja kumdanganya wala kumsumbua kwa namna yoyote ile wala sikuwahi hata kumwomba au kutumia hela zake ni vile tu nilikua sitaki kuwa mzigo kwake.

Lakini ghafla tu akabadilika nikimpigia simu hupokei na ikitokea amepokea ananiambia subiri nitakupigia siku inaisha nikimsumbua sana anaweza akapokea na asiongee.

Nilikua naweza nikatuma sms ikajibiwa baada hata ya siku mbili au tatu, kwasababu ya mimi kuwa busy sana na kazi nilikua nashindwa kwenda kumuona ofisini kwake.

Nilivumilia ile hali kwa karibu mwezi mzima, nilivyopata tu likizo nikasema nimtafute tuongee nijue shida nini lakini kila nikiomba appointment napewa kalenda.

Aliniblock kawaida na WhatsApp nliumia sana, kuna siku nikafanya tu suprise kwenda nyumbani kwake usiku kwavile anaishi mwenyewe nikamkuta yupo na mwanamke na jinsi walivyokua wamevaa huwezi ukasema ni dada au ndugu yake.

Alinifukuza na kuniambia hanijui kabisa kiukweli nililia sana na niliumia sana, kama wiki hivi iliisha sikumtafuta na kuna mwanamke alikua kila siku ananitumia sms za matusi na kuniambia nikae mbali na mpenzi wake.

Japo niliumia lakini nikasema isiwe shida nkaamua nikae kimya na nika move on kabisa, toka yametokea hayo yote mwezi wa sita sasa lile tukio nishalisahau kabisa na nipo naendelea na kazi na mambo yangu mengine.

Nashangaa leo mtu anakuja ofisini na watu wengine wawili wanadai eti ni kaka zake wamekuja kuniomba msamaha eti hadi analia, kwa kuondoa aibu nliomba tu ruhusa nikatoka nao kwenda kuongea nao nje kidogo na ofisini.

Anasema nisipo mkubalia atakua anakuja kila siku kazini kwangu na atahakikisha ananichafulia cv yangu pale ofisini.

Kiukweli wamenidhalilisha sana kwasababu ofisini kila mtu ananiona mtu wa maana na ni mtu ambaye hata sijawahi kuwa na skendo zozote mbovu najiskia aibu hata boss nitamueleza nini, nimemkatalia lakini haelewi.

Naombeni msaada wenu wakuu natakiwa kufanya nini maana sielewi huyu mtu amepanga kunifanyia kitu gani.

Natanguliza shukrani πŸ™
 
habari wana jf
niende moja kwa moja kwenye mada, toka mwaka 2020 kuna mwanaume nlikua nampenda sana in short ata mahusiano
Ulikosea sana kumtega ili akutongozee

Alikuwa hakupendi

Cha kukushauri ni mwelezee bosi wako full scenario ili mambo yasije kuvurugika mbeleni ila ila ila ila ila ila usikae kumrudia huyu mwanaume utajijengea kaburi lako

Yangu ni hayo tu 😁😁😁😁
 
Kuna watu wengine ni wapuuzi kuliko hata upuuzi wenyewe, akosee yeye alafu aje na vimasharti uchwara, huyo jamaa ni mpuuzi kuwahi kutokea sijui ulitoka wapi na mtu mpuuzi kiasi hicho, mshukuru Mungu kukuengua mikononi mwa huyo jamaa.

Ukirudiana nae utakua unakosea sana.
 
Huyo kisheti wakati unajilengesha, alikuwa na mauhusiano tayari.

Bahati mbaya watu si wa kweli, huenda sasa wameshamwagana anataka kuja kujipoza kwako.

Mkatae katakata, mchukulie RB tu asikuharibie kazi.

Ndiyo kitu pekee anataka kukufanyia, ukose kazi uanze kuhangaika na maisha.
 
😊 usihuzunike, hiyo ni fursa, fungus YouTube Channel, akiwa anakuja ofisini mrecord rusha kwenye channel yako, na jina la hiyo Series nakupa, the real life of a stranded stupid guy.
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ Daaah aseeee unanivunja mbavu 😁😁😁
 
Yaani mtego mdogo huo unachanganyikiwa,ukishasoma huu ujumbe inuka uende polisi kamshtaki waambie hivi
"kuna kaka anakujaga hapa ofisini anauza madawa ya kulevya ananilazimisha niwe msambazaji hapa ofisini kwetu"
Ananiambia nikikataa watanifanyia mbaya,naombeni mnusuru maisha yangu...halafu unalia kidogo.
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ Daaah aseeee unanivunja mbavu 😁😁😁
πŸ˜€πŸ˜€ #Thinkabaurit
I will be your first and loyal subscriber.

Pumbavu zake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom