Leejay49
JF-Expert Member
- Feb 10, 2023
- 12,958
- 39,959
Habari wana jf,
Niende moja kwa moja kwenye mada, toka mwaka 2020 kuna mwanaume nilikua nampenda sana in short hata mahusiano yetu ni mimi ambaye nlichochea anitongoze.
Nilikua najua mahali alipokua anafanya kazi kwahiyo ilikua rahisi kwangu kumwekea mitego mpaka aliponitongoza mwenyewe.
Mwanzo wakati tunaanza mahusiano alikua akinipenda na kunijali sana, kiukweli nilikua nampenda sana na sikuwahi hata siku moja kumdanganya wala kumsumbua kwa namna yoyote ile wala sikuwahi hata kumwomba au kutumia hela zake ni vile tu nilikua sitaki kuwa mzigo kwake.
Lakini ghafla tu akabadilika nikimpigia simu hupokei na ikitokea amepokea ananiambia subiri nitakupigia siku inaisha nikimsumbua sana anaweza akapokea na asiongee.
Nilikua naweza nikatuma sms ikajibiwa baada hata ya siku mbili au tatu, kwasababu ya mimi kuwa busy sana na kazi nilikua nashindwa kwenda kumuona ofisini kwake.
Nilivumilia ile hali kwa karibu mwezi mzima, nilivyopata tu likizo nikasema nimtafute tuongee nijue shida nini lakini kila nikiomba appointment napewa kalenda.
Aliniblock kawaida na WhatsApp nliumia sana, kuna siku nikafanya tu suprise kwenda nyumbani kwake usiku kwavile anaishi mwenyewe nikamkuta yupo na mwanamke na jinsi walivyokua wamevaa huwezi ukasema ni dada au ndugu yake.
Alinifukuza na kuniambia hanijui kabisa kiukweli nililia sana na niliumia sana, kama wiki hivi iliisha sikumtafuta na kuna mwanamke alikua kila siku ananitumia sms za matusi na kuniambia nikae mbali na mpenzi wake.
Japo niliumia lakini nikasema isiwe shida nkaamua nikae kimya na nika move on kabisa, toka yametokea hayo yote mwezi wa sita sasa lile tukio nishalisahau kabisa na nipo naendelea na kazi na mambo yangu mengine.
Nashangaa leo mtu anakuja ofisini na watu wengine wawili wanadai eti ni kaka zake wamekuja kuniomba msamaha eti hadi analia, kwa kuondoa aibu nliomba tu ruhusa nikatoka nao kwenda kuongea nao nje kidogo na ofisini.
Anasema nisipo mkubalia atakua anakuja kila siku kazini kwangu na atahakikisha ananichafulia cv yangu pale ofisini.
Kiukweli wamenidhalilisha sana kwasababu ofisini kila mtu ananiona mtu wa maana na ni mtu ambaye hata sijawahi kuwa na skendo zozote mbovu najiskia aibu hata boss nitamueleza nini, nimemkatalia lakini haelewi.
Naombeni msaada wenu wakuu natakiwa kufanya nini maana sielewi huyu mtu amepanga kunifanyia kitu gani.
Natanguliza shukrani π
Niende moja kwa moja kwenye mada, toka mwaka 2020 kuna mwanaume nilikua nampenda sana in short hata mahusiano yetu ni mimi ambaye nlichochea anitongoze.
Nilikua najua mahali alipokua anafanya kazi kwahiyo ilikua rahisi kwangu kumwekea mitego mpaka aliponitongoza mwenyewe.
Mwanzo wakati tunaanza mahusiano alikua akinipenda na kunijali sana, kiukweli nilikua nampenda sana na sikuwahi hata siku moja kumdanganya wala kumsumbua kwa namna yoyote ile wala sikuwahi hata kumwomba au kutumia hela zake ni vile tu nilikua sitaki kuwa mzigo kwake.
Lakini ghafla tu akabadilika nikimpigia simu hupokei na ikitokea amepokea ananiambia subiri nitakupigia siku inaisha nikimsumbua sana anaweza akapokea na asiongee.
Nilikua naweza nikatuma sms ikajibiwa baada hata ya siku mbili au tatu, kwasababu ya mimi kuwa busy sana na kazi nilikua nashindwa kwenda kumuona ofisini kwake.
Nilivumilia ile hali kwa karibu mwezi mzima, nilivyopata tu likizo nikasema nimtafute tuongee nijue shida nini lakini kila nikiomba appointment napewa kalenda.
Aliniblock kawaida na WhatsApp nliumia sana, kuna siku nikafanya tu suprise kwenda nyumbani kwake usiku kwavile anaishi mwenyewe nikamkuta yupo na mwanamke na jinsi walivyokua wamevaa huwezi ukasema ni dada au ndugu yake.
Alinifukuza na kuniambia hanijui kabisa kiukweli nililia sana na niliumia sana, kama wiki hivi iliisha sikumtafuta na kuna mwanamke alikua kila siku ananitumia sms za matusi na kuniambia nikae mbali na mpenzi wake.
Japo niliumia lakini nikasema isiwe shida nkaamua nikae kimya na nika move on kabisa, toka yametokea hayo yote mwezi wa sita sasa lile tukio nishalisahau kabisa na nipo naendelea na kazi na mambo yangu mengine.
Nashangaa leo mtu anakuja ofisini na watu wengine wawili wanadai eti ni kaka zake wamekuja kuniomba msamaha eti hadi analia, kwa kuondoa aibu nliomba tu ruhusa nikatoka nao kwenda kuongea nao nje kidogo na ofisini.
Anasema nisipo mkubalia atakua anakuja kila siku kazini kwangu na atahakikisha ananichafulia cv yangu pale ofisini.
Kiukweli wamenidhalilisha sana kwasababu ofisini kila mtu ananiona mtu wa maana na ni mtu ambaye hata sijawahi kuwa na skendo zozote mbovu najiskia aibu hata boss nitamueleza nini, nimemkatalia lakini haelewi.
Naombeni msaada wenu wakuu natakiwa kufanya nini maana sielewi huyu mtu amepanga kunifanyia kitu gani.
Natanguliza shukrani π