Naombeni ushauri wa kumuacha mume wa mtu

Naombeni ushauri wa kumuacha mume wa mtu

Chinene

Member
Joined
Nov 30, 2010
Posts
17
Reaction score
2
Ninaishi na mume wa mtu mwaka mmoja sasa na ananipa chochote ninachotaka na ananipenda sana na kunijali tatizo mimi natumia nguvu za giza kumpumbaza ili nimfaidi tu mpaka nitakapopata mchumba wa kunioa.

Nina rafiki wa kiume ambaye nilimweleza kila kitu na akakubali kuwa na mimi kwa hali yoyote ile na ananipenda sana nami nampenda maana hakika ni handsome wa nguvu ila tu uchumi haujakaa vizuri na huwa namsaidia shida ndogo ndogo maana nimetulia kwa mtu mwenye kila kitu yani namfananisha na Mungu wangu wa Duniani ila tatizo ni moja tu.

Huyu mume wa mtu kanizidi umri na huwa haniridhishi vizuri ila napretend tu ili aone nampenda sana na sina mwingine. Huyu handsome wangu ananifurahisha sana mpaka huwa naomba Mungu huyu mume asafiri niweze kuchepuka vizuri au wakati mwingine natumia siku ya Jumapili nikiaga naenda kwa ndugu, rafiki au salon, namalizana nae fasta fasta.

Nishaurini nifanyeje maana nikimpoteza handsome wangu nikabaki na huyu mzee yeye akizeeka mie nitakuwa bado mbichi sintaweza kutulia nyumbani. Sikutaka kubeba mimba haraka nikamwambie tule happy kwanza kumbe mimi nabuy time kuangalia muelekeo na kuisoma familia vizuri. Nikiwa kazini nawaza sana lakini ndugu zangu na mama yangu wananipa moyo niendelee tu.

Naombeni mnishauri maana naogopa kuja kujutia maamuzi yangu niko njia panda
 
Si umetumia nguvu za Giza kumpumbaza, tumia nguvu hizo hizo umfukuze arudi kwa familia yake. Kwani hamjamchuna tu vya kutosha ili wewe na Huyo handsome wako mjitegemee wenyewe na maisha yenu? Mrudishe mume wa watu kwa familia yake, Mwisho wa ubaya Ni AIBU
 
shit happen for the reason, sasa hizo sababu zisijekufanya ujutie mazima achana na mume wa mtu. Kila kitu kinalipwa hapa hapa duniani wewe umemteka kwa madawa mwenzako anaumia tuu kwenye ndoa yake sasa kwako itakuja kuwa twice stuka acha kabisa.
 
Wanawake siku zote ni wa ajabu sana! I always Trust no woman in this wild world!

haa haa kwa kweli sasa BigBro nina mashaka na mwanamke wa kumpa moyo wangu na kumweka ndani, kwa njia hii hakuna tena kwenye jamii walah sasa inatisha.
 
Huyo handsome wako na wewe wote mmekutana mna akili fupi!!
Handsome anakubali uliwe kwa ajili ya Pesa?!! Nakupa ukweli ulivyo sasa
Wewe unamchuna pesa huyo mume wa mtu lakini humpendi na wewe unachunwa na huyo handsome wako na wala hakupendi
Usitegemee hata siku moja kama huyo handsome wako atakuowa....anakuchuna kama wewe unavyochunwa
 
Achana na huyo Mme wa Mtu endelea na maisha yako tena Umejaliwa kuwa na kazi
 
Aisee dada, hivyo vitu vya duniani hapa ni vya mpito tu. Hata hao ndugu zako wanaokupa support kuendelea kuharibu ndoa ya mwanamke mwenzako hawako sahihi. Na wewe kutumia nguvu za giza si sahihi, cha msingi tafadhari achana na huyo mume wa mtu, na ubaki na huyo HB wako ambae wewe unaridhika nae. Malipo yote ni hapa duniani, please STOP IT.
 
Chinene

mwandiko unaonesha we ni wa kiume unajaribu utunzi wa AYAN MOSENYA
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom