ANTHONY MICHAEL
Member
- Aug 27, 2013
- 26
- 11
Habari za majukumu wana-MMU.
Kwa ufupi nipo kwenye mahusiano na binti takribani miezi 5 sasa. Mwanzo mapenzi yalikua mazuri na tulipendana sana na nilijitahidi kutimiza kile alichohitaji kadri ya uwezo wangu. Japo kuna kipindi mawasiliano yalipungua kwake ikawa nisipo mtafuta mimi yeye hanitafuti hata tukikubaliana Jambo fulani yeye hatimizi mpaka ikafika kipindi tukawa na mgogoro. Ila nilijaribu kukaa naye chini na kuzungumza hatimaye tukawa sawa.
Sasa wiki iliyopita alikua hapatikani hewani takribani siku 3 mfululizo siku alipo nipigia tukaongea na kumuuliza akasema simu yake kioo kilivunjika na akawa ameniomba pesa ya matengenezo na kiukweli sikuwa nayo na ikumbukwe siku 4 nyuma kuna pesa nilikua nimempa kwa ajili ya kujikimu mahitaji yake madogo madogo.
Mpaka naandika hapa sasa ni zaidi ya wiki sina mawasiliano naye ikiwa na maana simu yake haipo hewani mpaka leo hadi nashindwa kuelewa maana hata alipokua anakaa aliondoka Kwa muda akaenda Kwa shangazi yake ili nilikua nalijua. Hivi ina maana mpaka leo simu yake haijatengemaa? Na inawezekana Kwa mtu unayempenda kukaa bila mawasiliano Kwa zaidi ya wiki kweli?
Hapa hata sielewi maana hata marafiki zake hawana mawasiliano naye kwa muda. Hivi kuna mapenzi kweli hapa? Maana sijui Hali yake na nini kimemsibu mbali na tatizo la simu.
Naombeni ushauri wenu wadau. Asante
Kwa ufupi nipo kwenye mahusiano na binti takribani miezi 5 sasa. Mwanzo mapenzi yalikua mazuri na tulipendana sana na nilijitahidi kutimiza kile alichohitaji kadri ya uwezo wangu. Japo kuna kipindi mawasiliano yalipungua kwake ikawa nisipo mtafuta mimi yeye hanitafuti hata tukikubaliana Jambo fulani yeye hatimizi mpaka ikafika kipindi tukawa na mgogoro. Ila nilijaribu kukaa naye chini na kuzungumza hatimaye tukawa sawa.
Sasa wiki iliyopita alikua hapatikani hewani takribani siku 3 mfululizo siku alipo nipigia tukaongea na kumuuliza akasema simu yake kioo kilivunjika na akawa ameniomba pesa ya matengenezo na kiukweli sikuwa nayo na ikumbukwe siku 4 nyuma kuna pesa nilikua nimempa kwa ajili ya kujikimu mahitaji yake madogo madogo.
Mpaka naandika hapa sasa ni zaidi ya wiki sina mawasiliano naye ikiwa na maana simu yake haipo hewani mpaka leo hadi nashindwa kuelewa maana hata alipokua anakaa aliondoka Kwa muda akaenda Kwa shangazi yake ili nilikua nalijua. Hivi ina maana mpaka leo simu yake haijatengemaa? Na inawezekana Kwa mtu unayempenda kukaa bila mawasiliano Kwa zaidi ya wiki kweli?
Hapa hata sielewi maana hata marafiki zake hawana mawasiliano naye kwa muda. Hivi kuna mapenzi kweli hapa? Maana sijui Hali yake na nini kimemsibu mbali na tatizo la simu.
Naombeni ushauri wenu wadau. Asante

