Kuna wakati kweli tunahitajika tuyaangalie mambo kwa mapana yake
Kuna wakati watu hujiingiza kwenye changamoto nyingi sana kwa kujidai kukana kuwa watoto wao nao hufikia mahali wakawa na mahitaji kama vile marafiki,kutoka out n.k
Mambo hayo yalipelekea kujiingiza kwenye malumbano na na ugomvi na watoto wao kwasababu ya kujaribu kukana ukweli kuwa watoto wao nao ni binadamu kama wengine
Kwenye suala hili nako ni hivi pia
Wasichana wa ndani maarufu kama House Girls nao ni binadamu kama wengine
Wana marafiki,ndugu na wapenzi,sasa kama kweli tunawaona kama binadamu ambao wanahitaji kuwa na matumizi ya kibinadamu,shilingi 1000 inawezaje kutosha kwa wiki nzima?
Mi nadhani ni bora kutokumpa kabisa kuliko kumpa hela kidogo kama hiyo huku ukijua kabisa hana kipato kingine na akikitumia unakuja kulalamika,angalau ni bora uwe unampa kila baada ya siku 2 unampa hiyo "buku" maana kiukweli sijui ulitaka aitumie vipi kwa hiyo wiki nzima
Kama unajua nae ana watu ambao anahitajika kuwasiliana nao kama binadamu na hana kipato kingine kabisa ni bora ukajifikiria kama hiyo hela unayompa kama inatosha au laa
Nii dhana ya kuwaona hawa kama vile hawana mahitaji ya kibinadamu ndio inayopelekea malalamiko ya aina hii
Muongezee hela ya vocha au acha kabisa kumpa!