Naombeni msada: Nahitaji kuonana na Rais Samia

Naombeni msada: Nahitaji kuonana na Rais Samia

Ni muhimu sana mkuu,pia ni confidential sana.
Hivi kwanini Tunadhani Raisi ndie wa Kumpelekea Habari za Siri.. Sometimes unaweza Peleka Habari za Ufisadi kwake kumbe Yeye mwenyewe yupo kwenye Kundi Hilo.. Unakuwa umeenda Kujikaanga Mwenyewe..

Sometimes Ni Vyema Ukajua Kwanza Unapambana na Kina Nani kabla Hujaanzisha Vita ili ujue Unakabiliana Nao Vipi
 
Umesema ni siri sawa ila tuambie walau dondoo jambo linahusu nini
Je ni ishu ya uhujumu uchumi na matumizi mabaya ya ofisi umeyagundua?
Je ni wewe umetendewa jinai hivyo unahitaji haki yako ambayo unahisi level za chini hutasaidiwa?
Je ni ushauri wa masuala ya kiuchumi?


Funguka mkuu walau intro
Sijafanyiwa kosa, na Wala hakuna ufisadi wowote, but there is something very critical and important for the betterment our survival.
 
Baada ya kuomba utaratibu wa kuonana na Mhe: Daktari Samia Suluhu Hassan na Waziri mkuu, Wana jf wengi wamenidhihaki na kushidwa kunionesha namna au utaratibu ulivyo.

Hivyo basi nimeona ni vema ujumbe niliotaka kufikisha kwa Rais na Waziri mkuu nataka niuweke kwenye hard copy Kisha niutume ikulu kupitia posta.

Japo kuwa document hiyo ni kubwa sana, it's like a report, naamini njia hii itakuwa Sahihi kufikisha ujumbe huu muhimu sana.

Ujumbe wangu sio madai, Wala sio kwamba nadai haki yangu hapana.


Kwa Mungu wa taifa langu Amen
 
Wastege of time. Hilo li document hawata lisoma. Wataliweka kwenye dustbin.
 
Mi Ndo napokeaga hapa lazima niusome niuscan nilete pdf humu au nikupe email ya office ya rais? Ya chief minister?
 
Mheshimiwa huwa anapitia pitia humu, ungeandika tu hata watu wake wa karibu watamwambia
 
Weka huo ujume hapa mkuu, kwani haukusikia Samia alivyo sema kwamba hua anaperuzi pia kwenye mtandao wa jamiiforums..!!🤔
Alafu mihanisi ID yake ni ile inayo anza na......
 
Wakuu habarini,

Niende kwenye mada moja Kwa Moja, Wakuu naomba msaada nahitaji kuonana na Rais Samia Suluhu Hassan na jambo muhimu sana natamani ni mwambie physically. Ikishindikana basi nionane na waziri mkuu ndugu Kassimu Majaliwa Kassimu.

Lakini sifahamu utaratibu na namna ya kuonana na hao wakuu

Naombeni muongozo.

===

Hata Lucas mwashambwa naye hakukupa mwongozo wa kumfikia?
 
Wakuu habarini,

Niende kwenye mada moja Kwa Moja, Wakuu naomba msaada nahitaji kuonana na Rais Samia Suluhu Hassan na jambo muhimu sana natamani ni mwambie physically. Ikishindikana basi nionane na waziri mkuu ndugu Kassimu Majaliwa Kassimu.

Lakini sifahamu utaratibu na namna ya kuonana na hao wakuu

Naombeni muongozo.

===
Zaburi 146:3
[3]Msiwatumainie wakuu,
Wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake.
Put not your trust in princes, nor in the son of man, in whom there is no help.
 
Sijafanyiwa kosa, na Wala hakuna ufisadi wowote, but there is something very critical and important for the betterment our survival.
Kwa msaada wangu nadhani mwezi huu ndani ya siku kadhaa hizi Stendi ya Makumbusho inaamia mwenge pale na anaekujafanya ufunguzi ni Mama hiyo nenda kachunguze pale mwenge Stendi inapofunguliwa tukio itakuwa lini then siku ya ufunguzi nenda beba bango lako payuka kwa nguvu kadri uwezavyo akusikie nadhani kwa njia hiyo unaweza kuongea nae sasa maan atataka kujua una shida nae
 
Nenda magogoni au Chamwino pale ukifika ruka ukuta, ingia ndani nyoosha moja kwa moja mpaka mjengoni. Akikuongelesha mtu usimjibu chochote wewe focus na mishe yako tu
 
Wakuu habarini,

Niende kwenye mada moja Kwa Moja, Wakuu naomba msaada nahitaji kuonana na Rais Samia Suluhu Hassan na jambo muhimu sana natamani ni mwambie physically. Ikishindikana basi nionane na waziri mkuu ndugu Kassimu Majaliwa Kassimu.

Lakini sifahamu utaratibu na namna ya kuonana na hao wakuu

Naombeni muongozo.

===
professional ethics hii account yako nyingine huku kwani hapa hukufanikiwa??
 
Back
Top Bottom