Naombeni msaada please

Naombeni msaada please

Kwa kweli! Lakini ipo siku Mola ni mwaminifu milele
Amen: mkuu kuna wakati tunashindwa kujitafakari wenyewe ila tunatafakari ya wengne kijijini kuna fursa kubwa kuliko mjini maana unauwezo wa kuendesha maisha kwa garama ndogo na ukatengeneza mkwanja mrefu
 
Habari zenu wanajamii forum..ndugu zangu hali yangu ni mbaya kiuchumi nikiwa katika wakati huu mgumu wa kusubiri ajira ,nashindwa mpaka kupata mahitaji ya muhimu !.,nimekaa nikafikiria nikaona nianzishe biashara ndogo ya genge japo iweze kunisaidia kwa kipindi hiki kigumu lakini tatizo ni mtaji ,kitu pekee cha thamani nilicho nacho ni hii tecno M3 ambayo ndio naitegemea kupata habari mbalimbali na hata niiuze kupata mtaji pia hautatosha, kwa hiyo naomba mwenye kuguswa na hitaji langu anisaidie chochote hata mia ili niweze kupata mtaji niweze kujishkiza na hii biashara .

Mchanganuo:

-Nahitaji mtaji Wa sh.60,000 kwa ajili ya kuweka kibanda na kununulia bidhaa.

- Sehemu ninayotarajia kufungua genge ni nje ya nyumba ninayokaa ambapo ni kwa shangazi yangu.

-sehemu ninayoishi ni Vijibweni Kigamboni

Hitimisho;
-Najua kuna wengine watachukulia kama ni utapeli ,naheshimu mawazo na mitazamo yao ,lakini nawahakikishia kuwa hii ni shida imenibana mwenzenu na najaribu kuwashirikisheni mnisaidie kama si kwa hela hata kwa ushauri Mzuri utakao nifaa..Kwa atakaye guswa naomba ani PM .Ahsanteni.
Nenda kwenye makampuni ya ujenzi omba kazi ya usaidizi. Ukipata utaanzia hapo kuzichanga
 
Habari zenu wanajamii forum..ndugu zangu hali yangu ni mbaya kiuchumi nikiwa katika wakati huu mgumu wa kusubiri ajira ,nashindwa mpaka kupata mahitaji ya muhimu !.,nimekaa nikafikiria nikaona nianzishe biashara ndogo ya genge japo iweze kunisaidia kwa kipindi hiki kigumu lakini tatizo ni mtaji ,kitu pekee cha thamani nilicho nacho ni hii tecno M3 ambayo ndio naitegemea kupata habari mbalimbali na hata niiuze kupata mtaji pia hautatosha, kwa hiyo naomba mwenye kuguswa na hitaji langu anisaidie chochote hata mia ili niweze kupata mtaji niweze kujishkiza na hii biashara .

Mchanganuo:

-Nahitaji mtaji Wa sh.60,000 kwa ajili ya kuweka kibanda na kununulia bidhaa.

- Sehemu ninayotarajia kufungua genge ni nje ya nyumba ninayokaa ambapo ni kwa shangazi yangu.

-sehemu ninayoishi ni Vijibweni Kigamboni

Hitimisho;
-Najua kuna wengine watachukulia kama ni utapeli ,naheshimu mawazo na mitazamo yao ,lakini nawahakikishia kuwa hii ni shida imenibana mwenzenu na najaribu kuwashirikisheni mnisaidie kama si kwa hela hata kwa ushauri Mzuri utakao nifaa..Kwa atakaye guswa naomba ani PM .Ahsanteni.
60,000 ni kubwa mnao. Kwa mtaji wa Elfu tano unaweza kuishi.

Nunua unga wa ngano kilo mbili na mafuta na viungo vingine mnajua wenyewe. Anza kupika mandazi au kalimati au mafenesi yale yenye kitobo katikati.

Ongea na wenye maduka hata watatu uwe unapeleka Asubuhi jioni unaenda unachukua hela.

Haya na hilo huwezi watakuona hujasoma labda
 
Pole sana mkuu, ushauri wangu usirudie kosa 2020 siyo mbali okey?
 
Nashukuruni kwa ushauri ,,ila kumbukeni hali za vijijini kwetu hapafanani ,mimi kurudi kijijini kwa sasa sitaongeza chochote zaidi ya kuongeza burden tu !, kuna wengine wametoka vijiji vyenye ardhi nzuri na maeneo makubwa pia hali ya hewa nzuri na wengine tumetoka sehemu zenye tabu tupu ,.Najua wengi watabeza sababu hayajawapata..Japo hajatokea hata mmoja wa kunisaidia hata shilingi mia ila nawashukuru kwa maoni yenu,ndivyo tulivyo watanzania tulio wengi tunaongea na kurahisisha mambo tu ila kusaidiana kwa tangible things hakuna..Naomba mtaji mnisaidie wa 60000 tu ndugu zangu lakini mnasema tu easly nirudi kijijini na wakati nauli yenyewe ya kurudi kijijini kwetu ni zaidi ya huo mtaji.Asanteni Mungu awabariki
 
Nashukuruni kwa ushauri ,,ila kumbukeni hali za vijijini kwetu hapafanani ,mimi kurudi kijijini kwa sasa sitaongeza chochote zaidi ya kuongeza burden tu !, kuna wengine wametoka vijiji vyenye ardhi nzuri na maeneo makubwa pia hali ya hewa nzuri na wengine tumetoka sehemu zenye tabu tupu ,.Najua wengi watabeza sababu hayajawapata..Japo hajatokea hata mmoja wa kunisaidia hata shilingi mia ila nawashukuru kwa maoni yenu,ndivyo tulivyo watanzania tulio wengi tunaongea na kurahisisha mambo tu ila kusaidiana kwa tangible things hakuna..Naomba mtaji mnisaidie wa 60000 tu ndugu zangu lakini mnasema tu easly nirudi kijijini na wakati nauli yenyewe ya kurudi kijijini kwetu ni zaidi ya huo mtaji.Asanteni Mungu awabariki
tupe mrejesho mkuu
 
Asee mimi natafta mfanyakazi wa hotelini kama unaweza nichek kupitia hyo kaz taratibu utakua unatunza mtaji kwa malipo utayokua unapata nichek kwa taarfa zaid
 
Back
Top Bottom