Naombeni msaada kuhusu risiti kwenye vituo vya polisi

kiraia

JF-Expert Member
Nov 20, 2007
1,716
999
Ndugu zangu wanaJF nimewahi kushikwa mara mbili na Polisi wa usalama barabarani mara ya kwanza kwenye mataa ya Maktaba na mara ya pili katika kituo cha karume, Niliposhikwa mara ya Kwanza nilipelekwa kituo cha Sarrender Bridge nikalipishwa faini ya 20,000 nilipouliza risiti nikapewa kopy ya Karatasi niende central polisi kwa ajili ya kuandikiwa risiti, na hata niliposhikwa mara ya pili pale Karume walifanya hivyo hivyo na kuniambia niende Msimbazi ndio naweza kupewa risiti kwa masharti ya kuacha funguo ya gari, swali langu ni kwa nini wanachukua pesa wakati hawana risiti? Je ni kweli kuwa hawana risiti au ni mchezo mchafu?
 
Ni swali zuri ndugu yangu, labda kwa upana zaidi tungejua sheria inasemaje pale unapokamatwa na trafiki na kutakiwa kulipa fine

1. Ni lazima ulipe hapo hapo
2.Vipi kuhusu funguo za gari, ni lazima uwa achie
Kuna kitu kinaitwa notification, inafanyaje kazi
Kwa kujua haya labda tutapata mwanga kwenye swala hili maana inaudhi sana pale unapokamatwa na hawa wala rushwa na wakataka uache gari, mwisho wanaishia kula hiyo hela.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom