Naomben msaada wa mawazo

Naomben msaada wa mawazo

Naiona ndoa hii ikielekea ukingoni.

Anakuja mtoto, mahaba mengi yatakuwa kwa mtoto, mtoto nae ataanza kuuliza, mbona siku zote baba haukuwepo!? Mtamdanganya ili atulie.

Mara utaanza kummisi baba mtoto kwamba angekuwepo, mngemlea vyema mwanenu. Naona kila dalili ya mawasiliano na mzazi mwenzio yakurudi kwa spidi ya hatari.
 
Mbona Kama ushamaliza hapo kwenye conclusion unataka Ushauri upi tena
 
Nimeyapenda maamuzi ya jamaa alie kuacha sababu huna kazi......kuishi na mwanamke asiye na kazi Ni mzigo sana
Mungu muache tu aitwe Mungu nilifight nilienda chuo kwa hasira huku mtoto ananyonya....imagine unalala night vitanda vya wagonjwa nalaza mtoto hapo ...Mungu akanisaidia mwaka Jana nikapata ajira....
Mkewe alikua na cheti feki katumbuliwa...Mungu muache tu
 
  • Thanks
Reactions: THT
Ushauri wangu mzalie kwanza huyo mwanaume ndio ujue baadae utafanyaje, ila nawe awali kabla ya ndoa kwann ulimficha kumwambia kama una mtoto?
 
Naomben mnisaidie nifanyeje?
Mimi Ni mama wa mtoto 1 ana 5yrs
Nimeolewa ila mtoto nilizaa na mwanaume mwingine kabla sijaolewa yupo nyumban,
Sasa moyo unaniuma kwel mtoto kumuacha kwa mama nimeshindwa kuzoea maana niliishi na mtoto wangu kabla
Niliteseka maana nyumban mzee alinitimua mwanaume alinikataa pamoja na kunitolea mahar kisa nilikua Sina kazi akapata mchumba mwalimu wakati tupo kwenye process za ndoa

Akawa kaniacha...niliteseka na mtoto wangu mpaka last year nilivyoolewa nikamuacha nyumban ...moyo unaniuma mtoto wangu nilimpenda mno mpaka nawaza kuacha hi ndoa aisee
Familia inadai nisimchukue Kwanza mpaka nizae na huyu mwanaume siwezi leta mtoto wangu wakati sijazaa na huyu mume mpya
Na uzazi ndio umegoma sasa sijui nafanyaje Mimi!!!!

Jaman mabint nawashauri msizae nje ya ndoa jaman changamoto ni nyingi Sana, hasa Kama unampango wa kuja kuolewa badae
Ongea na Mumeo kama hana tatzo muombe umchukue, btw wanaume huwa sio shida sana kama mlivyo nyie.
Mie nikimpenda mwanamke hata kama anao wanne aje nao, shida ipo wapi? Unamjua nani atakayekuzika
 
Ukweli ni kuwa mwanaume kuishi na mtoto wa mwanaume mwenzie ilhali yeye hana mtoto ni ngumu sana! Kama wapo wanaoweza ni wachache. Bora uzae kwanza mtoto akishakua ndio itakuwa afadhali kukaa nae.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom