Naomben msaada wa mawazo

Naomben msaada wa mawazo

maimatha

Senior Member
Joined
Mar 2, 2013
Posts
129
Reaction score
162
Naomben mnisaidie nifanyeje?
Mimi Ni mama wa mtoto 1 ana 5yrs
Nimeolewa ila mtoto nilizaa na mwanaume mwingine kabla sijaolewa yupo nyumban,
Sasa moyo unaniuma kwel mtoto kumuacha kwa mama nimeshindwa kuzoea maana niliishi na mtoto wangu kabla
Niliteseka maana nyumban mzee alinitimua mwanaume alinikataa pamoja na kunitolea mahar kisa nilikua Sina kazi akapata mchumba mwalimu wakati tupo kwenye process za ndoa

Akawa kaniacha...niliteseka na mtoto wangu mpaka last year nilivyoolewa nikamuacha nyumban ...moyo unaniuma mtoto wangu nilimpenda mno mpaka nawaza kuacha hi ndoa aisee
Familia inadai nisimchukue Kwanza mpaka nizae na huyu mwanaume siwezi leta mtoto wangu wakati sijazaa na huyu mume mpya
Na uzazi ndio umegoma sasa sijui nafanyaje Mimi!!!!

Jaman mabint nawashauri msizae nje ya ndoa jaman changamoto ni nyingi Sana, hasa Kama unampango wa kuja kuolewa badae
 
Jiulize haya maswali...una miaka mingapi ya kuishi hapa duniani? na kwa nini mtu mmoja akunyime furaha unayoitaka?kama unataka kuishi na mtoto wako,piga chini ndoa jipange kiuchumi utatue changamoto zako.Jitahidi kila siku iwe ni siku ya furaha kwako...kuishi ni bahati pia,tumia pumzi yako bila kumkwaza mwingine na bila kujikwaza wewe.
 
Jiulize haya maswali...una miaka mingapi ya kuishi hapa duniani? na kwa nini mtu mmoja akunyime furaha unayoitaka?kama unataka kuishi na mtoto wako,piga chini ndoa jipange kiuchumi utatue changamoto zako.Jitahidi kila siku iwe ni siku ya furaha kwako...kuishi ni bahati pia,tumia pumzi yako bila kumkwaza mwingine na bila kujikwaza wewe.
Comment nzuri sana mkuu
 
Acha uvivu wa kufikiri wewe mwanamke unachanganyikiwa nn wakati mtoto yupo salama, una uhakika utakuwa na huyo mtoto wako kila mahali utakapo kwenda?

Msogeze mtoto uone utakavyoanza upya onhooo! Ww vunga tu ukihitaji kumuona mwanao siutakwenda kumsalimia tu. Fikiria nje ya box.
 
Pole sana kiongozi..kila mtu ni msikivu na anaroho ya Huruma..usifiche hisia zako.
Kaa na mumeo mueelze kila kitu unavyojisikia juu ya mtoto. Fanya kila njia katika kumshawishi...atakuelewa.
Wanawake hashindwi kitu toka kwa mwanaume sema hamjiamini tu.
Pole mkuu
 
  • Thanks
Reactions: THT
Vitu vingine vinaumiza kichwa kizembe zembe sana,,,, kwamba bora niache ndoa kisa mtoto wangu kabaki nyumbani na ninampenda sana mtoto wangu kwani huyo mwanaume umeshamwambia kuhusu mwanao aje hapo kwako akakataa!!!!????

Hivi huyo mumeo na ndugu zake hawajui yakwamba umeshazaa!??? Kama wanajua hofu yako nini,,, tulia kwa mumeo mwanamke mbona mnatupatia shida sana mtaani au hako kakazi kako ndiyo kanakupatia kiburi..
 
Kwani mumeo kaoa na mtoto huyo mwanao mpeleke kwa baba yake akalelewe huko yan utake kuvunja ndoa kisa mtt tena yuko kwenye mikono salama nyumban kwenu inamana hata wazazi wako huwaamini wakulelee mwanao
 
Jaman mabint nawashauri msizae nje ya ndoa jaman changamoto ni nyingi Sana, hasa Kama unampango wa kuja kuolewa badae
waufanyie kazi sana huu wosia.

ongea vizuri na mumeo tu wanaume sisi ni waelewa sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom