Manjagata
JF-Expert Member
- Mar 7, 2012
- 16,541
- 18,648
Kwa kweli tuvumilie tu maana jiwe lenyewe karibia linakata moto! Nchi yetu nzuri sana jamani basi wapumbavu wachache wanaofanya ionekane kama jehanamu lakini ni nchi nzuri sana iliyojaa fursa. Nimefika huku Loliondo kwa kweli nimeshangazwa na uzuri wa ardhi ya huku kwa kweli kama mtu wewe ni mpambanaji ni sehemu moja nzuri kwa Kilimo! Shida niliyoiona ni ubovu wa barabara, Jiwe kuwatenga sana hawa raia! Unajiuliza kwanini aliamua kwenda kumwaga ile hela kule baharini wakati bado kuna wilaya zina barabara mbovu kiasi hiki?Mkuu baki huko huko kwa ushauri wangu, japo Tz tatizo kubwa ni Jiwe lakini bado kuna unafuu na usalama wa kutosha. Epuka sana kuishi ugenini.
