Naomba ushauri wenu WanJF

RedDevil

JF-Expert Member
Apr 30, 2009
2,367
1,519
WanaJF, nimeona niwashirikishe kuhusu hili linalonisumbua muda kidogo kwani muda unaelekea ukingoni sasa. Mimi mwanaJF mwenzenu nimefanya application nyingi kwa ajili ya admission vyuo mbalimbali vya nje lakini application nyingi zinishis njiani ikiwa na maanisha huwa nashindwa kuzimalizia kutokana na gharama ama kushindwa kukamilisha malipo ya application fees. Nimejitahidi kufuatilia namna ya kulipa lakini kwa njia ya ama credit card au bank draft lakini shida ni kuwa nashindwa kutokana na kuongezeka kwa gharama. Kama kuna mtu au mwanaJF yeyote anaweza kunipa njia au kunishauri namna yeyote rahisi ya kufanya hayo malipo nitashukuru. Ahsanteni, naomba kuwasilisha hoja.
 
... huwa nashindwa kuzimalizia kutokana na gharama ama kushindwa kukamilisha malipo ya application fees.
...Nimejitahidi kufuatilia namna ya kulipa lakini kwa njia ya ama credit card au bank draft lakini shida ni kuwa nashindwa kutokana na kuongezeka kwa gharama.
... Kama kuna mtu au mwanaJF yeyote anaweza kunipa njia au kunishauri namna yeyote rahisi ya kufanya hayo malipo nitashukuru.
Umenichanganya kidogo nikashindwa kuelewa swali ni lipi. Je, tatizo ni kiwango kikubwa cha ada au namna (njia) ya ulipaji? Au ni vyote viwili? Kama ni kiwango kikubwa cha ada ya masomo, kwa nini usisome hapa hapa Tz? Iwapo bado lengo lako ni kusoma nje, basi apply nchi za Asia Mashariki, inaelekea ada zao si kubwa sana kulinganisha na Europe/USA kwani kuna wanafunzi wengi tu wa kiTanzania na Kiafrika kwa ujumla wanaosoma huko, na binafsi nilipokuwa Malaysia nilikuwa nakutana nao wengi tu.
 
Pole sana ndugu. Ila inaonesha tatizo lako kubwa ni pesa. Hilo ni tatizo sugu na common kwa wengi wetu,ndio maana wengi tumesoma hapa nyumbani,waliotoka wengi utakuta wamepata scholarship,otherwise ada ya vyuo vya nje+accommodation+kujikim+medical expense? Ni ngumu sana aisee. Endelea kuzichanga ila kama vipi apply chuo cha hapa home uanze maana time is running kama ulivyosema. Wanaoenda nje wengi utakuta wengi wao either wana hali nzuri kipesa au wamepata scholarship. Waliolazimisha ndio hao wanaohangaika sana mpaka huruma, na akina dada tena ndio kabisa tunaweza tukaanzisha mada mpya hapa. Good luck lakini!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom