Naomba ushauri: Nimezaa na dada yangu

7 5 mm

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2014
Posts
352
Reaction score
203
Habar ya mda huu wadau,

Moja kwa moja niende kwenye maada. Mkasa huu umenikumba nikiwa nafanya kazi mkoa flani kanda ya kati. Katika eneo ambalo nilikuwa naishi ni karibu na sehemu ambayo baba yangu alikuwa anafanyia kazi kabla ya kustaafu na kurudi nyumbani kwake namaanisha mkoa alikozaliwa yeye ambao upo kusini nyanda za juu.

Wakati baba anastaafu na kurudi mkoa aliozaliwa mimi na nikabaki mkoa huo huo aliokuwa anafanya kazi sikuweza kuhama naye kwasababu nilikuwa nafanya kazi kwenye kampuni moja ya mawasiliano .

Katika kipindi alichokuwa anafanya kazi kumbe alizaa nje ya ndoa na mwanamke mmoja lakini baba hakuweza kumhudumia yule mtoto kitendo ambacho kilimfanya mama mtoto asimweke karibu na baba.

Hata yeye baba hakuwahi kutuambia kuwa aliwahi kuzaa nje ya ndoa. Katka kipindi chote hicho mama huyo na mwanaye walikuwa wakiishi mbali kidogo na wilaya yetu.

Basi katika mizunguko ya kazi hapa na pale nilikutana na dada huyu ambaye ndiye nimezaa naye pasina kujua ni dada yangu. Tulikutana kwenye semina mkoani Kilimanjaro kama ilivyo kawaida ya wanaume nikamuaproach yule dada na akaingia line. Tukaanza kujihusisha kimapenzi kwa muda wa mwaka mzima mpaka alipopata ujauzito.

Ikanilazimu niukubali ule ujauzito na nikatafuta wazee wa mtaa ninaokaa na kwenda nyumbani kwa mwanamke ili kujitambulisha. Yule mama mkwe ambaye ni mama mdogo kihalali alipoona majina yangu matatu akapatwa na wasi wasi japo barua ilipokelewa.

Ikabidi akanitafuta kwa kuniuliza kiundani nilipojieleza ndipo akasema huyu uliyempa mimba ni dadayako tena wa damu.

Kwakweli niliishiwa nguvu akaanza kunisimulia kila kitu kuhusu baba yangu. Mpaka hapa ninapo andika mwanamke ameshajifungua na mtoto ana miezi 5.

Baba sijamwambia bado ila nataka nimpeleke huyu binti nyumban kwetu. Na hii siri naijua mimi na mama mkwe au mama mdogo.

Sijajua nifanyeje mama mwenyewe ameshindwa afanye nini, tunaogopa kuwashirikisha watu aibu.
 
Pole sana Mkuu-makosa anayo baba.Mpeleke dada nyumbani,na mtoto wenu uendelee na maisha.Huyo dada atapata mke mwingine.
 
du mbona kazi! nenda nalo taratibu hilo swala mkuu ili uchukuwe uwamuzi sahihi
 
Kosa sio.lako n.la baba ako though umezini kabla y ndoa lakin.wa kulaumiwa n.baba yako pole sana mkuu
 
17 Juni 2014
https://www.jamiiforums.com/mambo-ya-kikubwa/676383-nmemchoka-huyu-mwanamke-sna-hamu-naye.html
Nipo naye kwa mda wa miezi 4 ktk mahusiano ila kila nikifanya naye tendo anaishia kuridhika yeye tu wakat mm nabaki na hamu yangu.

21 Juni 2014
https://www.jamiiforums.com/mahusia...8194-nilishangazwa-sana-na-huyu-mwanamke.html
Ni muda wa mwaka mmoja tangu niachane naye.

Nilikuwa na dada mmoja ambaye alikuwa ni mpenzi wangu.

Kwa kipindi chote hicho nilichokuwa naye sikuwahi kumwingia kimwili kwasababu alikuwa anakataa sana kwa lengo la kusubiri mpaka ndoa.....

17 Julai 2014
https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/691414-nmezaa-na-dada-yangu-msaada.html
 
[h=3]Nilishangazwa sana na huyu mwanamke[/h] Started by 7 5 mm, 21st June 2014 09:25

MR. 7 5 mm!!..CAN YOU PLEASE GIVE ME THE TIMELINE OF THE RED BOLDED EVENTS....
 
Rudi nyumbani tafuta wazee walioona mengi wasiopokupa kurunzi watakuchimbia shimo la kutokea.
 
Hii bongo movie sijawahi kuiona ila mara ya mwisho niliicheki kwa wababe wa nollywood wazee wa Nigerian movie.
 
Haramu, haramu unaacha kuanzia pale ulipopata ukweli huu
 
Usinichekeshe mie, mtu kakupa penzi muda woote hadi kakuzalia mtoto leo unasema unamuonea kinyaa, huna haya wewe, kinyaa kinatoka wapi na wakti alikuwa mpenzi wako, bora hata ungesema unamuonea aibu, eti unamuona kinyaa, babako alimuona kinyaa na wewe umeshaanza kumuona kinyaa, thats why mmevuna mlichopanda

mmmmh! Mpaka sasa namwona kinyaa hata kumsogelea
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…