Naomba Ushauri na Msaada wa Mawazo

Naomba Ushauri na Msaada wa Mawazo

Passpp

Member
Joined
Apr 1, 2025
Posts
86
Reaction score
243
Naomba Ushauri na Msaada wa Mawazo

Wakuu, nimeamua kuandika hapa kwa unyenyekevu kabisa. Kuna changamoto ninayopitia kwa sasa na nimeona ni bora kushirikisha wenzangu kuliko kukaa nayo kimya.

Sihitaji lazima pesa; kama kuna mtu anaweza kunisaidia kwa ushauri, connection ya kazi, fursa yoyote halali au msaada wa aina nyingine, nitashukuru sana.

Kwa wale wanaoweza kunielekeza au kunishauri, niko tayari kusikiliza. 🙏
 
unataka ushauri kwenye nini zaidi?
Kwa sasa nahitaji ushauri upande wa kifedha. Sina hela, nahitaji kama TSh 30,000 tu kwa dharura. Nikifanikiwa kupata nitakurejeshea, naomba unisaidie ushauri wa namna ya kukabiliana na hali hii.
 
Miaka 30, elimu yangu ni Diploma ya Animal Husbandry (4M4), na kwa sasa najishughulisha na shughuli zinazohusiana na ufugaji huku nikisubiri nafasi ya ajira.
unaweza kufanya kazi zipi, na ungependa mshahara wako uanzie kiasi gani?
 
Kazi yoyote naweza kufanya, niko tayari kujifunza na kuanza. Mshahara tunaweza kuongea, ila kwa sasa nikisaidiwa TSh 30,000 nitashukuru sana. Na shida sana
unazingua, uzi wako umesema unahitaji connection ya kazi au mawazo, na umesema si lazima pesa sa unaulizwa upewe hiy kazi unaanza tena kuomba pesa hivi unazani kutoa elf 30 tu ni jambo rahisi kijana.?
 
unazingua, uzi wako umesema unahitaji connection ya kazi au mawazo, na umesema si lazima pesa sa unaulizwa upewe hiy kazi unaanza tena kuomba pesa hivi unazani kutoa elf 30 tu ni jambo rahisi kijana.?
Uko sahihi mkuu, nimekupata. Sikukusudia kuonekana kama nimegeuza ombi la connection kuwa ombi la pesa. Kipaumbele changu ni kupata kazi; hiyo TSh 30,000 ni changamoto ya muda tu. Asante kwa kunikumbusha.
 
Kwa sasa nahitaji ushauri upande wa kifedha. Sina hela, nahitaji kama TSh 30,000 tu kwa dharura. Nikifanikiwa kupata nitakurejeshea, naomba unisaidie ushauri wa namna ya kukabiliana na hali hii.
Wewe kama Tsh 30,000 inakushinda kupata, Utawezaje kuirejesha baada ya kukopeshwa?

Kijana uko sawa kweli?
 
Miaka 30, elimu yangu ni Diploma ya Animal Husbandry (4M4), na kwa sasa najishughulisha na shughuli zinazohusiana na ufugaji huku nikisubiri nafasi ya ajira.
Uko sehemu gani ?
Nikupe idea ya kupata pesa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom