Naomba Ushauri na Maelekezo: Jinsi ya Kusuluhisha Kesi ya Madai ya Kubumba

Foxhunters

Senior Member
Nov 25, 2019
123
67
Ndugu zangu, habari ya jioni. Ninaomba ushauri wa kisheria. Mimi nakabiliwa na kesi ya (madai) ya kubumba ambayo mdai alishinda kesi na mahakama ikaamuru mdaiwa (mimi) nilipe deni ndani ya siku 30, na hakukuwa na mjadala baada ya hukumu.

Siku 30 zilipita bila kulipa chochote kwa sababu sikuwa na hela ya kulipa.

Sasa nimeletewa barua ya kuitwa shaurini mahakamani kama mhukumiwa kuwa kwanini mahakama isichukue hatua dhidi yangu?

Naomba ushauri, namna gani nifanye ili nisiingie kwenye matatizo zaidi. Lengo langu ni kujichanganya ili nilipe deni husika. Shida iliyopo ni muda, nikipata miezi minne ninaweza kupata hela ninayodaiwa na kuilipa yote.

Nifanyeje juu ya shauri nililoitiwa mahakamani? Ushauri tafadhali, sina uzoefu na mambo haya ya kesi na mahakama.
 
Ungekuja wakati wa kesi ingekua poa Sana huenda pia ungepewa mbinu ungechomoka. Pia baada ya hukumu ungekuja ungepewa mbinu za Nini ukifanye ndani ya hizo siku 30 ambazo ndio muda wa kisheria kuonesha Nia ya kulipa au kukata rufaa.
 
Ndugu zangu, habari ya jioni. Ninaomba ushauri wa kisheria. Mimi nakabiliwa na kesi ya (madai) ya kubumba ambayo mdai alishinda kesi na mahakama ikaamuru mdaiwa (mimi) nilipe deni ndani ya siku 30, na hakukuwa na mjadala baada ya hukumu.

Siku 30 zilipita bila kulipa chochote kwa sababu sikuwa na hela ya kulipa.

Sasa nimeletewa barua ya kuitwa shaurini mahakamani kama mhukumiwa kuwa kwanini mahakama isichukue hatua dhidi yangu?

Naomba ushauri, namna gani nifanye ili nisiingie kwenye matatizo zaidi. Lengo langu ni kujichanganya ili nilipe deni husika. Shida iliyopo ni muda, nikipata miezi minne ninaweza kupata hela ninayodaiwa na kuilipa yote.

Nifanyeje juu ya shauri nililoitiwa mahakamani? Ushauri tafadhali, sina uzoefu na mambo haya ya kesi na mahakama.
Inamaana katika hiyo kesi yako, mdai amefungua maombi ya kukazia hukumu ya wewe kuwa mfungwa wa madai, ila inachohitajika hapo ni wewe kuhudhuria au kutii wito (summons) mahakamani katika siku uliyotajiwa. Na ukifika, utatoa sababu za kwa nini usiwe mfungwa wa madai. Basi, utatoa sababu mfano: ulikuwa unapitia kipindi kigumu cha uchumi na haukuweza kulipa kiasi chote cha deni katika muda uliopewa, ila uko tayari kumlipa kwa awamu katika kipindi cha miezi 4 (kama ulivyosema katika maelezo) na utalipa kiasi ................ hadi deni litakapokamilika.

Nimetoa maelezo ya jumla sababu sijui kesi yako vizuri wala sababu za wewe kutokulipa kwa wakati, na kiasi cha mkopo ulichochukua. Umekopa kutoka kwa taasisi au mtu binafsi na maamuzi ya hakimu/jaji katika kesi yako yalikuwaje.
 
Inamaana katika hiyo kesi yako, mdai amefungua maombi ya kukazia hukumu ya wewe kuwa mfungwa wa madai, ila inachohitajika hapo ni wewe kuhudhuria au kutii wito (summons) mahakamani katika siku uliyotajiwa. Na ukifika, utatoa sababu za kwa nini usiwe mfungwa wa madai. Basi, utatoa sababu mfano: ulikuwa unapitia kipindi kigumu cha uchumi na haukuweza kulipa kiasi chote cha deni katika muda uliopewa, ila uko tayari kumlipa kwa awamu katika kipindi cha miezi 4 (kama ulivyosema katika maelezo) na utalipa kiasi ................ hadi deni litakapokamilika.

Nimetoa maelezo ya jumla sababu sijui kesi yako vizuri wala sababu za wewe kutokulipa kwa wakati, na kiasi cha mkopo ulichochukua. Umekopa kutoka kwa taasisi au mtu binafsi na maamuzi ya hakimu/jaji katika kesi yako yalikuwaje.
Asante kwa mwongozo kiongozi,maelezo yako yamenipa mwanga .
 
Ungekuja wakati wa kesi ingekua poa Sana huenda pia ungepewa mbinu ungechomoka. Pia baada ya hukumu ungekuja ungepewa mbinu za Nini ukifanye ndani ya hizo siku 30 ambazo ndio muda wa kisheria kuonesha Nia ya kulipa au kukata rufaa.
Ni kweli sikuja kwa wakati ,maana mimi siyo mzoefu kwenye haya mambo nilijiamini kwa kuwa kesi haikuwa halisi bali ya kubumba ili nihukumiwe. Lakini ndiyo hivyo mahakama ilimpa ushindi yeye.
 
Inamaana katika hiyo kesi yako, mdai amefungua maombi ya kukazia hukumu ya wewe kuwa mfungwa wa madai, ila inachohitajika hapo ni wewe kuhudhuria au kutii wito (summons) mahakamani katika siku uliyotajiwa. Na ukifika, utatoa sababu za kwa nini usiwe mfungwa wa madai. Basi, utatoa sababu mfano: ulikuwa unapitia kipindi kigumu cha uchumi na haukuweza kulipa kiasi chote cha deni katika muda uliopewa, ila uko tayari kumlipa kwa awamu katika kipindi cha miezi 4 (kama ulivyosema katika maelezo) na utalipa kiasi ................ hadi deni litakapokamilika.

Nimetoa maelezo ya jumla sababu sijui kesi yako vizuri wala sababu za wewe kutokulipa kwa wakati, na kiasi cha mkopo ulichochukua. Umekopa kutoka kwa taasisi au mtu binafsi na maamuzi ya hakimu/jaji katika kesi yako yalikuwaje.
Nikifanya hivi,hakutakuwa na matatizo kwa upande wangu tena .??? Pia naomba kufahamu mfungwa wa madai na anakuwaje?.mwisho wake unakuwaje
 
Nikifanya hivi,hakutakuwa na matatizo kwa upande wangu tena .??? Pia naomba kufahamu mfungwa wa madai na anakuwaje?.mwisho wake unakuwaje
Mfungwa wa madai ni kuwa huyo anayekudai itabidi aende akaonane na afisa wa gereza apewe gharama zote za kukutunza wewe ukiwa magereza,na chakula chako sio ugali na maharage,ni kile cha kawaida cha nyumbani,kama una matatizo ya kiafya labda huli ugali ni wali tu,lazima akulishe hivyo!!akishapewa hizo gharama za mwezi ,anaenda kulipia ndio upokelewe magereza.Na akishindwa tu kulipa unaachiwa,ila hizo pesa anazokulisha atakudai tena!!YAANI huwa ni ngumu sana ,hiyo hufanywa na mtu anayekudai pesa nyingi na uwezo unao wa kumlipa ila hutaki tu/au una ndugu wenye uwezo .Tofauti na hivyo ni kuzidi kijitia hasara tu.Nadhani kwa sasa gharama ya kumtunza mfungwa wa madai kwa siku inaweza fika 15,000 kwa siku,hapo ni chakula tu!!bado matibabu!!umfunge miezi 6 hapo kuna nini?na una mdai milioni 5!!ILA KUPANGA NI KUCHAGUA.mimi sio mwanasheria ila naongea tu kutokana na uzoefu nalo.
 
Nikifanya hivi,hakutakuwa na matatizo kwa upande wangu tena .??? Pia naomba kufahamu mfungwa wa madai na anakuwaje?.mwisho wake unakuwaje
white wizard ametoa ufafanuzi mzuri sana,kwa ufupi ni kuwa matatizo bado yapo kwakuwa unadaiwa ,hivyo kinachotakiwa kufanyika ni wewe kuanza kutafuta pesa ili ikiwezekana siku utakayoenda mahakamani uanze kutoa hicho kiasi cha pesa na kuahidi kulipa kiasi kilichobakia ndani ya miezi minne na kufuata taratibu zingine.Japo sijui ni kiasi gani unachodaiwa na imepita muda gani bila kulipa,kwa maelezo na msaada zaidi karibu PM ukiwa na nakala ya maamuzi(hukumu)kutoka mahakama husika.
 
Mfungwa wa madai ni kuwa huyo anayekudai itabidi aende akaonane na afisa wa gereza apewe gharama zote za kukutunza wewe ukiwa magereza,na chakula chako sio ugali na maharage,ni kile cha kawaida cha nyumbani,kama una matatizo ya kiafya labda huli ugali ni wali tu,lazima akulishe hivyo!!akishapewa hizo gharama za mwezi ,anaenda kulipia ndio upokelewe magereza.Na akishindwa tu kulipa unaachiwa,ila hizo pesa anazokulisha atakudai tena!!YAANI huwa ni ngumu sana ,hiyo hufanywa na mtu anayekudai pesa nyingi na uwezo unao wa kumlipa ila hutaki tu/au una ndugu wenye uwezo .Tofauti na hivyo ni kuzidi kijitia hasara tu.Nadhani kwa sasa gharama ya kumtunza mfungwa wa madai kwa siku inaweza fika 15,000 kwa siku,hapo ni chakula tu!!bado matibabu!!umfunge miezi 6 hapo kuna nini?na una mdai milioni 5!!ILA KUPANGA NI KUCHAGUA.mimi sio mwanasheria ila naongea tu kutokana na uzoefu nalo.
Asante kwa mchango wako .
 
white wizard ametoa ufafanuzi mzuri sana,kwa ufupi ni kuwa matatizo bado yapo kwakuwa unadaiwa ,hivyo kinachotakiwa kufanyika ni wewe kuanza kutafuta pesa ili ikiwezekana siku utakayoenda mahakamani uanze kutoa hicho kiasi cha pesa na kuahidi kulipa kiasi kilichobakia ndani ya miezi minne na kufuata taratibu zingine.Japo sijui ni kiasi gani unachodaiwa na imepita muda gani bila kulipa,kwa maelezo na msaada zaidi karibu PM ukiwa na nakala ya maamuzi(hukumu)kutoka mahakama husika.
Nitakuchek kiongozi
 
Mfungwa wa madai ni kuwa huyo anayekudai itabidi aende akaonane na afisa wa gereza apewe gharama zote za kukutunza wewe ukiwa magereza,na chakula chako sio ugali na maharage,ni kile cha kawaida cha nyumbani,kama una matatizo ya kiafya labda huli ugali ni wali tu,lazima akulishe hivyo!!akishapewa hizo gharama za mwezi ,anaenda kulipia ndio upokelewe magereza.Na akishindwa tu kulipa unaachiwa,ila hizo pesa anazokulisha atakudai tena!!YAANI huwa ni ngumu sana ,hiyo hufanywa na mtu anayekudai pesa nyingi na uwezo unao wa kumlipa ila hutaki tu/au una ndugu wenye uwezo .Tofauti na hivyo ni kuzidi kijitia hasara tu.Nadhani kwa sasa gharama ya kumtunza mfungwa wa madai kwa siku inaweza fika 15,000 kwa siku,hapo ni chakula tu!!bado matibabu!!umfunge miezi 6 hapo kuna nini?na una mdai milioni 5!!ILA KUPANGA NI KUCHAGUA.mimi sio mwanasheria ila naongea tu kutokana na uzoefu nalo.
Sijawahi sikia hii kitu kwa kweli... Nipe uzoefu wa hili mkuu nami niongezee maarifa
 
Mfungwa wa madai ni kuwa huyo anayekudai itabidi aende akaonane na afisa wa gereza apewe gharama zote za kukutunza wewe ukiwa magereza,na chakula chako sio ugali na maharage,ni kile cha kawaida cha nyumbani,kama una matatizo ya kiafya labda huli ugali ni wali tu,lazima akulishe hivyo!!akishapewa hizo gharama za mwezi ,anaenda kulipia ndio upokelewe magereza.Na akishindwa tu kulipa unaachiwa,ila hizo pesa anazokulisha atakudai tena!!YAANI huwa ni ngumu sana ,hiyo hufanywa na mtu anayekudai pesa nyingi na uwezo unao wa kumlipa ila hutaki tu/au una ndugu wenye uwezo .Tofauti na hivyo ni kuzidi kijitia hasara tu.Nadhani kwa sasa gharama ya kumtunza mfungwa wa madai kwa siku inaweza fika 15,000 kwa siku,hapo ni chakula tu!!bado matibabu!!umfunge miezi 6 hapo kuna nini?na una mdai milioni 5!!ILA KUPANGA NI KUCHAGUA.mimi sio mwanasheria ila naongea tu kutokana na uzoefu nalo.
Sijawahi sikia hii kitu kwa kweli... Nipe uzoefu wa hili mkuu nami niongezee maarifa
 
Sijawahi sikia hii kitu kwa kweli... Nipe uzoefu wa hili mkuu nami niongezee maarifa
Mimi kuna mzee tulikuwa tunamdai pesa nyingi,kulipa hataki ila uwezo anao,na watoto wake wako vizuri!!hukumu ikatoka kuwa alipe pesa, akasema sitaki kulipa fanyeni mnalotaka hakimu akasema vipi nmnaweza kumgharamikia jela,angalau kwa miezi sita kwanza tuone?tukasema powa,akatupa barua tukaenda nayo magereza,tukapewa utaratibu(gharama) zote,tukaenda kulipia,Akaenda kukamatwa tukampeleka!!mbona ndani ya siku tatu tu,watoto wake walitutafuta tuyamalize!!tukaenda mahakamani tena tukakubaliana jinsi ya kuilipa pesa,tukaenda kumtoa ila gharama zote tulizokuwa tumemlipia waliturudishia papo hapo kwanza,wao watadai magereza huko.Tunashukuru pesa yote ililipwa.
TAHADHARI.Kabla ya kufanya hivyo angalia kwanza kiwango cha deni na uwezo wa mdaiwa!!usije ukajikuta unazidisha hasara juu ya hasara.
 
Mimi kuna mzee tulikuwa tunamdai pesa nyingi,kulipa hataki ila uwezo anao,na watoto wake wako vizuri!!hukumu ikatoka kuwa alipe pesa, akasema sitaki kulipa fanyeni mnalotaka hakimu akasema vipi nmnaweza kumgharamikia jela,angalau kwa miezi sita kwanza tuone?tukasema powa,akatupa barua tukaenda nayo magereza,tukapewa utaratibu(gharama) zote,tukaenda kulipia,Akaenda kukamatwa tukampeleka!!mbona ndani ya siku tatu tu,watoto wake walitutafuta tuyamalize!!tukaenda mahakamani tena tukakubaliana jinsi ya kuilipa pesa,tukaenda kumtoa ila gharama zote tulizokuwa tumemlipia waliturudishia papo hapo kwanza,wao watadai magereza huko.Tunashukuru pesa yote ililipwa.
TAHADHARI.Kabla ya kufanya hivyo angalia kwanza kiwango cha deni na uwezo wa mdaiwa!!usije ukajikuta unazidisha hasara juu ya hasara.
Shukrani mzee, nmeongeza kitu kwenye ndonga yangu.
 
Back
Top Bottom