Mimi nina miaka 57 ni mstaafu . Kwanza niseme lugha aliyotumia ni ya kawaida kabisa nawashangaa wanaomshangaa . Napenda kukushauri siri ya kuweza kumudu maisha ya kustaafu ujaliwe na familia nzuri inayokuzunguka kuanzia mke , watoto na extended family wasiwe pasua kichwa . Hata ulipwe kiasi gani huwezi kufungua biashara yoyote ikafanikiwa kama hujapata mtu wa kuweza kuisimamia . Unatoka mjini kwenda shamba kujiunga na mkeo sawa . Nyumba ni kitegauchumi chako umeziacha na wapangaji nani anakupokelea kodi ? Sasa hivi wanakuheshimu uko karibu wanakulipa kodi . Ukiwa kijijini kama unafikiri watakurushia kwa M-pesa sahau . Jiandae na trip za kuja mjini kuja kudai kodi zako , kumwondoa mpangaji mkorofi , kufanya matengenezo na kutafuta mpagaji mpya . Waliomshauri agenge guest house ndio wamempotosha kabisa . Nitaomba uniajiri mimi mapokezi niwe napiga hela ya short time .