Naomba ushauri kuhusu nyumba yangu Bagamoyo

Naomba ushauri kuhusu nyumba yangu Bagamoyo

Eliud Bunju

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2017
Posts
375
Reaction score
707
Nimehamishiwa Chalinze kutoka Bagamoyo, lakini tayari nmejenga ila Bado sijamaliza finishing lkn familia yangu mke na mtoto mmoja wanaishi hapo na Mimi nachoka kurudi Bagamoyo kwenda na kurudi. Sitaki kupanga Chalinze maana najua utamu wa kuishi nyumbani kwako.

Nyumba tayari nimeweka umeme na maji, Bado finishing Tu tiles na rangi Pamoja na gypsum bodi.

Namshukuu Mungu Chalinze nimepata kiwanja kingine, nimeanza kutamani nipauze kule bagamoyo halafu pesa nitakayopata ninunue kiwanja bagamoyo nije huku Chalinze nijenge nyumba nyingine upya katika kiwanja hiki cha Chalinze kiwanja kiko sehemu nzuri sana kuna nguzo ya umeme na maji yapo karibu sana.

Naombeni ushauri wenu wakuu. Niuze kule Bagamoyo au nikomae nimalizie nipangishe. Nije kupanga huku Chalinze?
 
Nimehamishiwa Chalinze kutoka Bagamoyo, lakini tayari nmejenga ila Bado sijamaliza finishing lkn familia yangu mke na mtoto mmoja wanaishi hapo na Mimi nachoka kurudi Bagamoyo kwenda na kurudi. Sitaki kupanga Chalinze maana najua utamu wa kuishi nyumbani kwako...
Hizo akili za kujenga sehemu ambazo hazina value mnazitowa wapi?
 
Piga bei vyote, nyumba na kiwanja, mbona kuna nyumba nyingi za kupanga?

Hapa duniani tunapita tu, sasa sijui unanunua nyumba za kazi gani!
 
MAlizia hiyo na ukaanze kulee halafu pangisha huko bagamoyo , halafu jenga kule tena maana sio gharama
 
Yani unajenga nyumba sehemu ukitaka kupangisha nyumba nzima kodi laki moja, sasa hizo ni akili?
Hivi unajua laki moja kwa mwaka ni sh. Ngapi ni ml 1 na laki mbili na unajua kwa miezi sita ni laki 6 kuliko huna kabisa kunasiku umekwama hiyo akiba ndio ipo hiyo ni hela mzee baba hata akiopoa atapata mteja wa laki nanusu
 
Hivi unajua laki moja kwa mwaka ni sh. Ngapi ni ml 1 na laki mbili na unajua kwa miezi sita ni laki 6 kuliko huna kabisa kunasiku umekwama hiyo akiba ndio ipo hiyo ni hela mzee baba hata akiopoa atapata mteja wa laki nanusu
Na ajue ardhi inakuwa na thamani kila kukicha na Nyumba haiozi,,mipango ya muda marefu,,ya Kati na mifupi unaijua kwenye ardhi na mijengo,,, hata hapo anapo paona ni mjini lilikuwa Pori kabla
 
Daah. Nimehamia huku Mwanza nimeacha nyumba yangu niliyokuwa naijenga Dar, roho inaumaaa.
 
Huu ni ushauri wangu kwako na Hata vijana wengine

Ni mara 100 ukanunua mashamba ama viwanja maeneo potential kuliko kukimbilia kujenga nyumba ya kuishi.

Ukinunua maeneo / mashamba , unakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuishi vzr hapo baadae kuliko kukimbilia kujenga nyumba.
 
Chalinze Bagamoyo mbona si mbali? Jenga nyingine taratibu baada ya kumalizia hiyo ya bagamoyo. Au nunua gari kama huna, siku nyingine unadrive tu vuuhm.
Nikwel pia nimefikilia kutafuta usafiri.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Huu ni ushauri wangu kwako na Hata vijana wengine

Ni mara 100 ukanunua mashamba ama viwanja maeneo potential kuliko kukimbilia kujenga nyumba ya kuishi.

Ukinunua maeneo / mashamba , unakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuishi vzr hapo baadae kuliko kukimbilia kujenga nyumba.
Watakuambia ukifa watoto watapata shida.
 
Back
Top Bottom