Naomba Ushauri Juu Ya Hali Hii Ya Wife

naombeni msininione binafsi,aa... ila kuishi na ndugu wa mume ni lawama maana waweza kujitoa kwa roho yako yote lakini hawaridhiki,mi niliishi na shem angu mwaka jana akiwa form two alikua jeuri,kiburi aambiwe kitu na kaka yake lakini sio mimi,nimeumwa mimi ye alikua likizo basi hata anisaidie chochote hamna anaenda kuzurura,lakini angekua mdogo wangu hapo angenisaidia,ila kiukweli tunamkaribisha shetani mana hamuwezi kujinafasi na mume wako
nachoshauri ni kuwasaidia wakiwa kwa wazazi wao au wapelekwe bording au hostel uwahudumie huko
 

Umemuoa wewe au mmemuoa ukoo mzima?
 
Huyo wa darasa la saba naweza kufahamu kuja kujiendeleza lakini huyo wa la pili mmmmh bora mrudishe. Kijijini hakuna shule jamani, pili ni mdogo atakosa mapenzi ya wazee. Tatu huyo mkeo kama keshaanza kunung'unika atakuja mtesa huyo mtoto.

He is too young for all that, msaada haukatazwi lakini mbo ya kuishi na extended family hizi za bongo pasua kichwa.
 
ahaaaaaaaaaaaa! Ticha ndo umetema vitu hizooooo design za kifisadi kama mtoto Nata??????????? Daaaaah! I cant believe this!!!!!!!!!!!

me nikahisi mtu kaiba PaSsWorD yake jman, Lol
 
Fuata ushauri wa mke wako kaka,achana na watoto wa ndugu zako. Familia ni BABA,MAMA NA WATOTO.Hata huyo mdogo wake anayesoma CHUO fukuza. Kama ni kusaidia watoto wa kaka yako wasaidie wakiwa huko huko kwao,sio unawaleta kwako. Chukua hiyo usisikilize kelele za watu.
Utapata shida sana mkeo akiondoka na ndo mwanzo wa kuharibika kwa ndoa na familia yako kwa ujumla.
 

swadaktaaaaaa.....
Mke ni rahisi kucontrol ndugu zake lakini ukitaka kucontrol nduhu za mume huchelewi kuiywa mchoyo,tania mbaya na mengine mengi.....tena watasambaziana maneno ukoo mzima..hayo ndo wanayoyakataa wanawake wengi...


Lakini miaka hii kukaa na watu chungu nzima ya nini? Ndugu wa mke na wa mume kama kuna uwezekano wa kuwasaidia huko waliko wasaidiwe huko huko... Au waende boarding la sivyo maneno maneno na mifarakano ndipo inapoanzia.
 

start with capital M in when u mention God the creator..................ujumbe mzuri!
 
Tatizo kubwa hapo ninaloweza kuliona ni mke wako kuogopa mzigo wa ulezi.

Kulea mtoto wa darasa la pili, na mwengine aliyepo katika umri ambao watoto wengi huwa wakaidi, si jambo dogo na inawezekana ikawa hilo linalomuogopesha japo kuwa hajachukua njia sahihi kufikisha ujumbe wake (kama hajakueleza hili)

Mkilizungumza suala hilo linaweza kukusaidia kidogo
 
Well said Gaijin,naomba kura yako miss chit chat
 
Last edited by a moderator:
Mmmmh, yaani kabisa nimesoma, nimeanza kazi
Nina wadogo zangu? BAdo wanahitaji shule eti niwaache kuwasaidia kisa kuogopa extended family sijui mume ana nini
Phheeeewwww! Niwaache ili baadae waje kuwa tegemezi?

Au niwaache afu kwenye ukoo niwe nimetoka alone???
Unaenda kwa nduguyo hana hata shati kisa ulishindwa kumsomesha na uwezo ulikuwa nao?

To hell!

Kuna watu fulani fulani wanafanikiwa karibu familia nzima sababu ya kusaidiana, sio kumsaidia mtu pesa bali kumpa njia ya kujipatia kipato.

Mfano, wahindi wa TZ hawatupani, hata wachaga baadhi yao unakuta kaka kamwajiri mdogo wake dukani. Nenda baada ya miaka miwili yule mdogo naye ana kibanda chake, hawa ni katika biashara.

Wanaoamini katika elimu pia, hauwezi kuwa na degree ukasema nimpunguzie kidogo ndugu yangu, awe na certificate afu mie niwe na advanced diploma, elimu haigawanyiki kihivyo, lazima akae darasani na asome.

SI kila jambo la kuiga, iga kwa akili na manufaa ya uwapendao
 
Mwanamke MJINGA ataivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe
 
Inavyoonesha Mkeo Hajakataa Kuwapa Msaada Hao Nduguzo,Tatizo Hawi Huru Iwapo Nduguzo Mtaishi Nao!
Kama Kuna Uwezekano Wa Kuwahudumia Nduguzo,Waki Mbali Na Nyumba Yako!..Basi Waondoe Nyumbani Na Endelea Kuwasomesha Wakiwa Mbali!
Msikilize Mkeo Banah!
 
anatikisa kiberiti huyo..we mwambie unakubaliana naye aende kwao halafu usiongee sana..najua ni ngumu ila kaza moyo mkuu. amini nakuambia hamalizi hata wiki atakutafuta mikono nyuma anataka kurudi. pole sana!
 
Nimesoma maoni ya wengi, there's mixing feelings lakini ukweli utabaki kuwa kwa maisha yetu ya Kiafrika hatuwezi kukimbia extended family. Wengi wetu tumepitia kwenye mikono ya watu wengi na tumekaa kwa kaka, dada, shemeji, mjomba, nk kabla ya kuanza kujitegemea na kuwa na mafanikio tuliyonayo sasa. Itakuwa ni upumbavu kama wewe baada ya kufanikiwa hautaki kuangalia nyuma na kutoa msaada kama ambavyo na wewe ulivosaidiwa mpaka ukafanikiwa. Wazo la kuwasaidia huko waliko ni wazo zuri, lakini tuwe wakweli elimu ya leo kijijini ni mbovu sana, kwa hiyo kama mtu una nafasi na una nia ya kumsaidia ndugu yako ni bora uanze angali mdogo kw kumpeleka kwenye shule nzuri, provided uwezo unao. Hivi ndiyo tunavyoishi kiafrika. By the way, ni faraja sana kama mwisho wa siku hao uliowasadia wakafanikiwa na kuwa na maisha mazuri, jamani wema hauozi. Kuna familia wamezaliwa zaidi ya 10, lakini wote wamepata elimu nzuri na wana kazi za maana ukifuatilia utagundua kuwa wazazi hata hawakuwa na uwezo wowote wa kuwapa elimu watoto wote, lakini kwa kuwa mkubwa alipata elimu na akatambua umuhimu wa kuwavuta ndugu zake, mwisho wa siku wote wamafanikiwa na wanaishi maisha mazuri ya kuheshimiana na kusadiana kwa shida na raha.
Kwa ushauri kama una nafasi ya kuwasaidia, pls wasaidia kwa kadri ya uwezo wako na mke wako anapaswa ajue kuwa your doing for good.
 
Mtoto wa darasa la pili anakunyima uhuru mama mwenye nyumba??


Nikupe mfano: Nimezaliwa na kukulia Tandale kwa mfuga mbwa, nimetoka kwa manati na kuolewa.
Mdogo wangu yuko darasa la pili, nahitaji asome, kwa sasa naishi Arusha, je unadhani mazingira ya kwa mfugwa mbwa yanafaa sana?? Risk zikoje??


Unamsaidia mtu akiwa mbali kama mazingira ya huko yanaruhusu kusaidika, hata pale mazingira hayaruhusu umwache tu?? Haiingii akilini

Ee Mungu, nisaidie kuwaelewa wanadamu

Inavyoonesha Mkeo Hajakataa Kuwapa Msaada Hao Nduguzo,Tatizo Hawi Huru Iwapo Nduguzo Mtaishi Nao!
Kama Kuna Uwezekano Wa Kuwahudumia Nduguzo,Waki Mbali Na Nyumba Yako!..Basi Waondoe Nyumbani Na Endelea Kuwasomesha Wakiwa Mbali!
Msikilize Mkeo Banah!
 
baadhi ya wanawake ni kama watoto, anapima kina cha maji.

Ila angalia pia kakulia mazingira gani, kama kwao alizoea kuishi wao wa familia yao tu, basi lazima aone mzigo kuishi na nduguzo.

hilo neno pia ,mazingira aliyokulia labda yamechangia yeye kuwa hivyo pia ya kutozoea kuishi na familia kubwa ya nduguzo
 
Jamani nawashukuruni nyote, kwa michango yenu ya mawazo kwa sababu nimepata upeo sasa, kiasi kwamba kuna uwezekano wa kuamua kusaidia au ukaacha au ukasaidia mtu akiwa mbali au karibu lakini pia ukamfuata Mke na kutowasikiliza ndugu au ukawa na msimamo wako binafsi bila kujali wengine watasema nini provided uko katika right way. Mawazo yangu yaliyobakia kichwani hayatofautiani kabisa na yale ya akina na Micha, Kongosho, jamiif na wengineo wengi.
Nawashukuru sana na kwakuwa nilijisikia kama mtu aliyekosa wa kuongea naye kama rafiki wa karibu wa kuweza kunishauri vizuri hadi nilipo leta habari hii hapa, nahisi kama mzigo uliokuwepo ndani ya nafsi yangu nimeutua kwani hii ni true story na imetokea juzi Jumatano nikawa kama nimepoteza ramani vile! Nitatoa feedback kwenu iwapo itatokea vinginevyo.

ILA NAHISI KWA MAISHA YA WATANZANIA WALIO WENGI BADO TUNAISHI KATIKA HALI YA EXTENDED FAMILY, HATA KAMA HATUKAI NA NDUGU KARIBU LAKINI BADO WANATUNYOOSHEA MIKONO KUANZIA SHIDA NDOGO NDOGO KAMA MSOSI (KILIMO KINAPOPATA MATATIZO mfano. UKAME/MAFURIKO), ELIMU, MAKAZI, n.k.
SASA KAMA NTAPATA NAFASI YA KUONANA NAYE HAMUONI KUWA NI VEMA KUMUONYESHA HIZI KOMENTS MAANA WENGINE WAMEWEKA VITU KAMA CASE STUDIES ZA MAISHA HALISI AMBAO WAO WAMEYAPITIA ILI NAYE AWEZE KUELEWA MAONI YENU NI YAPI JUU YA HILI?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…