Naomba Ushauri: Gari gani linamfaa mstaafu.

Kama ameshakamilisha yale mambo ya msingi mfano kusomesha, kujenga nyumba ya familia, kuweka vitega uchumi vya kula uzeen, nadhani ataweza kukabiliana na changamoto za kumiliki gari....
Pia anunue gari ambalo halijatumika kwenye mikono ya watanzania...hapo atakuwa na uhakika wa kuendesha miaka kama 5 bila kupata changamoto kubwa kubwa...yeye atakuwa anabadi oil ya engine na transmission, brake pads, bushes, plugs, matairi na mambo mengine ambayo ni ya kawaida sana kulingana na hali ya barabara zatu.....
Wastaafu wengi wanashikishwa magari mabovu, ndiyo yanaenda kusaidia kuchochea umasikini uzeeni.....kununua gari mkononi mwa mtanzania ni sawa na kucheza kamari...unaweza ukala au ukaliwa...
Nina mtumishi mwenzangu hapa kazini kauziwa IST namba C milioni 6, kwa kweli inamtesa...hiyo milioni 6angeongeza 2, angeweza kupata gari kule beforward ambaloangeendesha miaka 4 bila shida....
Gari isiyosumbua ni ile unayonunua kiwandani ya KM 0 haya Used kutoka Japani nayo ni mchezo wa kubahatisha tu. Kama hujawahi miliki gari ukiwa kazini au katika ujana wako usinunue gari baada ya kustaafu haina tofauti na kuoa mke wa pili uzeeni. Hata ukipigwa bao na traffic huna uzoefu wa kujieleza utajikuta unakamuliwa tu 30 kila kukicha. hujakwanguliwa na vichaa barabarani humo, hujakwangua magari ya wenzio bado matatizo yenyewe ya gari nk. Katika uzee usio na uzoefu gari litakupeekea stress sana
 
Gari isiyosumbua ni ile unayonunua kiwandani ya KM 0 haya Used kutoka Japani nayo ni mchezo wa kubahatisha tu. Kama hujawahi miliki gari ukiwa kazini au katika ujana wako usinunue gari baada ya kustaafu haina tofauti na kuoa mke wa pili uzeeni. Hata ukipigwa bao na traffic huna uzoefu wa kujieleza utajikuta unakamuliwa tu 30 kila kukicha. hujakwanguliwa na vichaa barabarani humo, hujakwangua magari ya wenzio bado matatizo yenyewe ya gari nk. Katika uzee usio na uzoefu gari litakupeekea stress sana
Mwenye uzi alishajieleza mstaafu atakuwa na dereva wake....
Used Japan usije ifananisha na used bongo...
Gari mpya kutoka kiwandani ikija bongo mwa bara bara zetu za kizalendo miaka michache tu mahudhurio ya garage yanaanza kama kawaida...rejea magari ya serikali ambayo yanakuja 0 km..
 
Kwa pesa hiyo mshauri aagize gari ambayo haizidi 10m kiasi kwamba hata akienda town wahuni wakaichukua anapitia yard na kununua/kuagiza nyingine hata kwa instalment muda huo huo. Siyo maswala ya kurudi nyumbani kwa miguu. Au gari ambayo ikizingua akaipeleka garage na kuambiwa kitu kikubwa anaitelekeza hukohuko kwa wakata spare kisha anapitia yard.
 
Hii ndiyo jamii forum.....
Kila mtu ana uhuru wa kutoa mawazo yake....

Na mimi natoa mawazo yangu....
Mstaafu kama ni wa kufa mapema atakufa mapema tu bila kujalisha ana gari au hana....inategemea life style aliyokuwa nayo tangu ujanani....

Ni kweli kuna baadhi ya watu wakiwa na gari wanajizembea, hawatembei tena kwa miguu....na hawafanyi kazi zozote za kuwatoa jasho

Binafsi mstaafu ambaye ni Mwalimu, Mwanajeshi au Polisi....hawa watu sina wasiwasi nao....huwa hawajiweki kizembe hata wakiwa na magari 10....miili yao ilishazoea kutembea sana, kusimama sana na kufanya kazi nyingine za mikono...

Mstaafu akiwa na kazi zake za kawaida za mikono za kika siku zinazomtoa kajasho kidogo, ni zoezi tosha....
Sioni tatizo akiwa na usafiri wa kwenda sokoniz kanisani, harusini siku amealikwa au safari nyingine binafsi......

Binafsi bado naunga mkono wazo la mstaafu kuwa na usafiri...cha msingi aendelee kufanya kazi zake za mikono mfano kufua, kudeki, kuosha vyombo, kuhudumia bustani zake za mboga mboga na matunda....hizo movements ni zoezi tosha...
Pia apunguze matumizi ya nyama nyekundu, na azidishe mboga mboga na matunda, apende ibada...
Hapo mstaafu atafurahia maisha..


Yani umemueleza vizuri sana sina la kuongeza.
 
Gari isiyosumbua ni ile unayonunua kiwandani ya KM 0 haya Used kutoka Japani nayo ni mchezo wa kubahatisha tu. Kama hujawahi miliki gari ukiwa kazini au katika ujana wako usinunue gari baada ya kustaafu haina tofauti na kuoa mke wa pili uzeeni. Hata ukipigwa bao na traffic huna uzoefu wa kujieleza utajikuta unakamuliwa tu 30 kila kukicha. hujakwanguliwa na vichaa barabarani humo, hujakwangua magari ya wenzio bado matatizo yenyewe ya gari nk. Katika uzee usio na uzoefu gari litakupeekea stress sana
Ukiwa na mawazo haya hata ukiwa kijana hutoweza kununua gari.
 
Ukiwa na mawazo haya hata ukiwa kijana hutoweza kununua gari.
Naona uelewa wako mgumu sana walimu wako walipata taabu sana kukufundisha. Mimi nakazia kuhusu kununua gari ungali kijana ili uweze kukabiliana na changamoto za gari ilihali u kijana mwenye nguvu na akili inayofanya kazi kwa haraka kuliko kuja kununulia uzeeni ambako akili na nguvu zimepungua ndo uanze kukabiliana na changamoto za magari. Wewe unakuja na mawazo yako 0 hapa
 
Naona uelewa wako mgumu sana walimu wako walipata taabu sana kukufundisha. Mimi nakazia kuhusu kununua gari ungali kijana ili uweze kukabiliana na changamoto za gari ilihali u kijana mwenye nguvu na akili inayofanya kazi kwa haraka kuliko kuja kununulia uzeeni ambako akili na nguvu zimepungua ndo uanze kukabiliana na changamoto za magari. Wewe unakuja na mawazo yako 0 hapa
Nashukuru kwa dharau zako mkuu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom