Naomba ushauri: Ameniambia "Baba wa nini?"

Masai wa Town

JF-Expert Member
Joined
Apr 9, 2017
Posts
6,553
Reaction score
23,914
Nilikuwa nataka nikajitambulishe kwa wazazi wa huyu binti sasa katika kumhoji napaswa kupeleka zawadi gani? Nikaona ananiorodheshea zawadi za mama yake tu.

Nikamuulize zawadi za baba je? Akajibu "baba wa nini wewe? Wewe fuata maelekezo ninayokupa"

Nimeshindwa kuelewa maana alisema baba yake yupo hai
 
Labda babake alishafariki...

Labda ni deadbeat dad na hajawahi kuwa kwenye maisha yake...

Labda hamfahamu tangu azaliwe...

Labda....

Muulize vizuri akwambie.

Changamoto nyingi za mabinti hutokana na mahusiano yao na baba zao hasa utotoni. Binti aliyetelekezwa na babake (abandonment) au aliyekuwa abused na babake (kingono, kihisia, kimwili...) ana uwezekano mkubwa sana wa kuwa na changamoto nyingi za kisaikolojia huko ukubwani mf. Kutokujiamini, kutokujithamini, hasira zisizo na sababu, utumiaji wa vileo kupindukia, kutafuta kupendwa na kufurahisha wengine kwa gharama yo yote ile, kutojali hata umfanyie nini, kutoamini katika mapenzi ya kweli, kuwa narcissist, kuwa mchafu, kutafuta sana attention; na mengineyo mengi.

Hili ni jambo la muhimu sana. Mwambie akwambie ukweli.
 
Daaaah umeusema ukweli mchungu!!!!
 
Hafai huyo "fuata maelekezo niliyokupa"
Kwani yeye ni luteni, mbona commanding language.... Piga chini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…