masara
JF-Expert Member
- Jul 20, 2016
- 1,738
- 2,279
Za asubuhi,
Niende kwenye mada moja kwa moja na sababu yai mimi kuleta uzi huu.
Sababu kubwa ni kisa cha rafiki yangu mmoja ambaye ni dereva wa hiace au daladala hapa Mwanza na bosi wake ambaye pia ni mfanyakazi wa serikali misugwi.. huyu bosi wake anaitwa Mage...mwenye gari namba DQD.. yenye maneno.(I LOVE YOU.... NA GOD IS.....) inasemekana kabla ya kuja Mwanza alikuwa kati ya moshi au Arusha ila mkubwa mmoja wa serikali alikuta madudu kwenye kitengo chake hivyo akatimuliwa na kuletwa Mwanza.
Kama kawaida ya daladala huwa inaamsha alfajiri sana, rafiki yangu alienda kuchukuwa gari ili aingie kazini ila kwa bahati mbaya alipata ajali ya kugogwa na kupelekea gari kuharibika lakini jambo zuri ni kwamba hakudhulika na yule aliye mgonga alikubali kutengeneza gari na gari hadi sasa iko barabarani inapiga kazi kama kawaida lakini bila dereva aliyepatwa na ajali.
Cha kusangaza wengi nikwamba mwanzo pale polisi ilionekana kama bosi anataka hasa gari yake itengenezwe na hana mambo mengi ila ghafla baada ya gari kutengemaa bosi analazimisha kesi iende mahakamani ili aliyemgonga amlipe fidia ya malipo yake... na hapo ndio kisa cha dereva kinaanzia
Kama ilivyokawaida ya mabosi wengi wa magari huwa wanataka leseni ya dereva kukakaa nayo na hivyo na rafiki yangu katika mazingira yasiyoelezeka sana bosi aliweza kupata leseni ya dereva kabla hata ajali.
na baada ya ajali kutokea dereva kasimamia gari ila baada ya gari kuwa katika hali yake bosi amemgeuzia kibao na kumwambia alipe kiasi fulani cha pesa ndio ampe leseni yake, deni hilo limepatika ni kwa sababu jana yake kabla ya ajali walipigwa adhabu ya faini na trafik hivyo kabla ya kulipa ndio ajali ikatokea kwa sababu hiyo bosi aliamua kulipa faini hiyo na kujaza mafuta yaliyotumika kwenye mizunguko ya ajali. mwisho dereva kadhulumiwa mishahara yake na kupewa deni ambalo lilipatikana kwa sababu ya kazi za gari ya bosi.
Devera baada ya kuona hivyo akaona aende kitengo cha kazi lakini kwa sababu walikuwa na makubaliao na mdomo kesi yake inakuwa haina nguvu, dereva amejaribu kwenda polisi ili kuona kama itaweza kushinikiza apewe japo leseni yake, ukweli kwa hatua za awali polisi walikamata gari ya bosi ila waliiachia kwa maelekezo kuwa dereva apewe lesen yake na walipowasiliana na bosi wa gari alisema dereva afate na hana tatizo.
Lakini cha kushangaza dereva alipofata leseni bosi alimfokea dereva na kumwambia polisi hana mamlaka ya kushika gari maana hawajamchngia hata mia na zaidi akadai kuwa na akiendelea kufatilia leseni yeye anawatu wa kuweza hata kuifungia ili asiweze kutengeneza nyingine yaani iwe WANTED au akiitwa polisi atakataa kuwa hana leseni ya dereva kwa vile hakuna ushaidi wa makabidhiano na hawana mikataba, kwa kifupi huyo bosi anafanya kama kumkomoa maana anasema ni bora apoteze kazi ya serikali kuliko kutoa leseni.... sasa wote hatujui huyu dada anachuki gani...
Changamoto iliyopo ni kwamba polisi anayemshughulikia huyu dereva kiukweli yuko busy sana hivyo upatikanaji wake ili kurudisha majibu umekuwa ni mdogo hiyo ndio sababu.
Mimi maoni yangu ni kwamba, serikali iweke shinikizo kubwa kuwa mabosi wasichukue hata kopi ya leseni ya dereva na badala yake wawe na mikatamba ambayo itamtambua mdhamini badala ya leseni ili tatizo likijitokeza mdhani awajibike na sio kushikilia leseni.
Niende kwenye mada moja kwa moja na sababu yai mimi kuleta uzi huu.
Sababu kubwa ni kisa cha rafiki yangu mmoja ambaye ni dereva wa hiace au daladala hapa Mwanza na bosi wake ambaye pia ni mfanyakazi wa serikali misugwi.. huyu bosi wake anaitwa Mage...mwenye gari namba DQD.. yenye maneno.(I LOVE YOU.... NA GOD IS.....) inasemekana kabla ya kuja Mwanza alikuwa kati ya moshi au Arusha ila mkubwa mmoja wa serikali alikuta madudu kwenye kitengo chake hivyo akatimuliwa na kuletwa Mwanza.
Kama kawaida ya daladala huwa inaamsha alfajiri sana, rafiki yangu alienda kuchukuwa gari ili aingie kazini ila kwa bahati mbaya alipata ajali ya kugogwa na kupelekea gari kuharibika lakini jambo zuri ni kwamba hakudhulika na yule aliye mgonga alikubali kutengeneza gari na gari hadi sasa iko barabarani inapiga kazi kama kawaida lakini bila dereva aliyepatwa na ajali.
Cha kusangaza wengi nikwamba mwanzo pale polisi ilionekana kama bosi anataka hasa gari yake itengenezwe na hana mambo mengi ila ghafla baada ya gari kutengemaa bosi analazimisha kesi iende mahakamani ili aliyemgonga amlipe fidia ya malipo yake... na hapo ndio kisa cha dereva kinaanzia
Kama ilivyokawaida ya mabosi wengi wa magari huwa wanataka leseni ya dereva kukakaa nayo na hivyo na rafiki yangu katika mazingira yasiyoelezeka sana bosi aliweza kupata leseni ya dereva kabla hata ajali.
na baada ya ajali kutokea dereva kasimamia gari ila baada ya gari kuwa katika hali yake bosi amemgeuzia kibao na kumwambia alipe kiasi fulani cha pesa ndio ampe leseni yake, deni hilo limepatika ni kwa sababu jana yake kabla ya ajali walipigwa adhabu ya faini na trafik hivyo kabla ya kulipa ndio ajali ikatokea kwa sababu hiyo bosi aliamua kulipa faini hiyo na kujaza mafuta yaliyotumika kwenye mizunguko ya ajali. mwisho dereva kadhulumiwa mishahara yake na kupewa deni ambalo lilipatikana kwa sababu ya kazi za gari ya bosi.
Devera baada ya kuona hivyo akaona aende kitengo cha kazi lakini kwa sababu walikuwa na makubaliao na mdomo kesi yake inakuwa haina nguvu, dereva amejaribu kwenda polisi ili kuona kama itaweza kushinikiza apewe japo leseni yake, ukweli kwa hatua za awali polisi walikamata gari ya bosi ila waliiachia kwa maelekezo kuwa dereva apewe lesen yake na walipowasiliana na bosi wa gari alisema dereva afate na hana tatizo.
Lakini cha kushangaza dereva alipofata leseni bosi alimfokea dereva na kumwambia polisi hana mamlaka ya kushika gari maana hawajamchngia hata mia na zaidi akadai kuwa na akiendelea kufatilia leseni yeye anawatu wa kuweza hata kuifungia ili asiweze kutengeneza nyingine yaani iwe WANTED au akiitwa polisi atakataa kuwa hana leseni ya dereva kwa vile hakuna ushaidi wa makabidhiano na hawana mikataba, kwa kifupi huyo bosi anafanya kama kumkomoa maana anasema ni bora apoteze kazi ya serikali kuliko kutoa leseni.... sasa wote hatujui huyu dada anachuki gani...
Changamoto iliyopo ni kwamba polisi anayemshughulikia huyu dereva kiukweli yuko busy sana hivyo upatikanaji wake ili kurudisha majibu umekuwa ni mdogo hiyo ndio sababu.
Mimi maoni yangu ni kwamba, serikali iweke shinikizo kubwa kuwa mabosi wasichukue hata kopi ya leseni ya dereva na badala yake wawe na mikatamba ambayo itamtambua mdhamini badala ya leseni ili tatizo likijitokeza mdhani awajibike na sio kushikilia leseni.