Naomba orodha ya viwanda vilivyoanza kujengwa

Naomba orodha ya viwanda vilivyoanza kujengwa

singojr

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2014
Posts
5,314
Reaction score
6,896
Niende moja kwa moja kwenye swali la msingi tumeambiwa tuko kwenye Tanzania ya viwanda mi naomba tu list au hata picha tu ya kiwanda kilicho kwenye hatua ya ujenzi au hata tu eneo lililofyekwa ili kiwanda kijengwe. Maana huu wimbo wa Tanzania ya viwanda nimeshindwa kuuimba.
 
Mh jaman mbona hata ww kiwanda unacho hebu jichunguze vzr
Mimi nnavifahamu walau viwanda vitatu vilivyopo katika hatua za mwisho kabla ya kufunguliwa... Kimoja kipo Kibaha Maili Moja ni cha kutengeza sabuni aina ya Kleesoft, shampoo za aina mbalimbali na 'detergents'; kingine kipo kilomita tano kabla ya kufika Chalinze kutokea Dar es Salaam ni cha kutengeneza tiles na kingine kipo eneo la Mboga, Chalinze. Hini ni cha kusindika matunda.

Kwa ujumla vyote vitakapoanza kazi vitatoa ajira za moja kwa moja takriban 10,000
 
Niende moja kwa moja kwenye swali la msingi tumeambiwa tuko kwenye Tanzania ya viwanda mi naomba tu list au hata picha tu ya kiwanda kilicho kwenye hatua ya ujenzi au hata tu eneo lililofyekwa ili kiwanda kijengwe. Maana huu wimbo wa Tanzania ya viwanda nimeshindwa kuuimba.
Usipende sana kuamini maneno ya wanasiasa
 
Mbona comment za wadau zinazidi kunivuruga ina maana kumbe sio tu mimi sijaona viwanda ishu ni hakuna viwanda
 
Viwanda vipo vingi ukiwa na vyereani vyako vinne ni viwanda [emoji3][emoji3][emoji21] Tanzania ya vi Wonder
 
Back
Top Bottom