T 2021 SSH
Member
- Apr 26, 2021
- 20
- 42
Habari zunu ndg zangu,
Nimekuwa nikifanya kazi TBA mkoani Geita, hapa wanajenga jengo la TANESCO mkoa wa Geita.
Hapa tunafanya kazi kama day worker, tunalipwa kwa wiki, ila toka mwezi wa pili tumefanya kazi bila malipo yoyote(ikimbukwe tumetoka mbali tumeweka kambi hivyo tulijikuta tunaendelea tu kufanya kazi kwa kukosa nauli)
Hawataki kutulipa pesa yetu, wameamua kutuzungusha tu, tuna familia tunaendeshaje maisha miezi miwili hatuna pesa?
Tumeenda mara kadhaa ofisi ya mkuu wa mkoa Geita bila mafanikio (hatukuwa tunakutana na RC), tukaamua kwenda ofisi ya mkuu wa wilaya, hapo pia hatujakutana na DC ila tulifanikiwa kukutana na DAS akatusikiliza.
Aliwapigia simu viongozi wa TBA na wakandarasi wakaja ofisini kwake akawasikiliza na akawasisitiza watulipe pesa yetu ndani ya siku mbili ilikuwa ni jumatano ya tarehe 21 ila mpaka leo kimya.
Jamani tunaomba mtusaidie namba ya Waziri wa Ujenzi au Waziri wa Kazi na Ajira(vijana) watusaidie kupata stahiki zetu kama kuna wawakilishi wa TANESCO na TBA humu msisahau kuwatagi pia waone uonevu tunaofanyiwa TBA Geita.
Ahsanteni!
Nimekuwa nikifanya kazi TBA mkoani Geita, hapa wanajenga jengo la TANESCO mkoa wa Geita.
Hapa tunafanya kazi kama day worker, tunalipwa kwa wiki, ila toka mwezi wa pili tumefanya kazi bila malipo yoyote(ikimbukwe tumetoka mbali tumeweka kambi hivyo tulijikuta tunaendelea tu kufanya kazi kwa kukosa nauli)
Hawataki kutulipa pesa yetu, wameamua kutuzungusha tu, tuna familia tunaendeshaje maisha miezi miwili hatuna pesa?
Tumeenda mara kadhaa ofisi ya mkuu wa mkoa Geita bila mafanikio (hatukuwa tunakutana na RC), tukaamua kwenda ofisi ya mkuu wa wilaya, hapo pia hatujakutana na DC ila tulifanikiwa kukutana na DAS akatusikiliza.
Aliwapigia simu viongozi wa TBA na wakandarasi wakaja ofisini kwake akawasikiliza na akawasisitiza watulipe pesa yetu ndani ya siku mbili ilikuwa ni jumatano ya tarehe 21 ila mpaka leo kimya.
Jamani tunaomba mtusaidie namba ya Waziri wa Ujenzi au Waziri wa Kazi na Ajira(vijana) watusaidie kupata stahiki zetu kama kuna wawakilishi wa TANESCO na TBA humu msisahau kuwatagi pia waone uonevu tunaofanyiwa TBA Geita.
Ahsanteni!