Naomba mwenye anwani za Taasisi ya kijani kibichi

AbouZakariya

JF-Expert Member
Mar 19, 2013
1,615
2,337
Habari wakuu,

Jamani jana mida ya asubuhi kati ya saa 1:30 na saa 2:00 asubuhi kupitia radio TBC nilisikia watu wakihojiwa, hao jamaa walikuwa wakihamasisha ufugaji wa mende pamoja na ukulima wa strawbery na mchaichai. Nilivutiwa na maelezo yao, lakini sikuwahi kusikia wakitaja namba zao za simu ama mahala ilipo hiyo taasisi.

Kwa hiyo wadau nimekuja kwenu, kwa mwenye kujua mawasiliano yao au mahala zilipo ofisi zao kwa hapa DSM anijuze.

Natanguliza shukrani.
 
Kwanini PM, mbona tbc walikuwa public?

Mkuu:
Una haki kuuliza kwa nini, sababu kubwa kwangu ni kuwa, anuani kamili ya ofisi sina lakini nina namba za simu binafsi za wahusika, inawezekana wanapenda/hawapendi namba zao za simu kujulikana kwa umma. Hata hivyo Ofisi zao zipo Kimara Temboni elekea kwenye Bar ya Hoja mita 50 kulia jirani na nyumba ya Mzee Mwanache. Samahani sana Mkuu.
 
Duh nilidhani kijani kibichi mmea wa anko bob male nikajua ushatambuliwa hadi sa hivi una taasisi yake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom