Naomba mtizamo wako tafadhali....

Naomba mtizamo wako tafadhali....

kibali

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2011
Posts
504
Reaction score
425
Wakuu wa MMU heshima mbele sana,

Poleni na majukumu ya wiki nzima.Naombeni kujua mitizamo yenu juu ya hili... Ni mume/mchumba anaishi mtaa mmoja na baadhi ya wafanyakazi wenzie ambao ni wadada..i mean wanatumia route moja waendapo kazini. Je ni sawa wale wadada either kila mmoja kwa wakati wake kuwa wanapiga simu kuomba lift asubuhi au mchana ile mida ya lunch, au wakati mwingine kutoa order kabisa ya kusubiriwa ili waende wote? Tafadhali naomba kujua kama imekaa sawa au wivu wangu tu unanisumbua..lol😱hwell:

Week end njema kwenu.

Kibali
 
Kwa mm ninae jijua kuwa nina wivu mpaka naugua sio sawa hata kidogo.Hao waomba lift kwann wasisubirie tu hiyo lift itokee kama bahati.Binadamu wa siku hizi walivyo na tamaa sasa!!mara watake kumiliki jumla
 
hao wapige marufuku kabisa chelea chelea utakuta mwana si wako wanaanzaga hivo.:fear:
 
Kama una wivu dawa ni kujinyonga tu,uwezekano mkubwa sana ni kuwa hao ni wake wenzio.
 
Kwa mwanamke mwenye akili timamu, si sawa kumganda mume wa mtu kwa lift kila siku
Lazima mtaishia kitandani.

Na hata kwa wanamme, unamwombaje mdada tena mke wa mtu lift kila siku
Tena unawahi siti ya mbele nusura ubadili na gia
Akiachika, hope utamlinda.

Anyway, mtizamo wangu wa lift huwa naomba mara moja wakati kweli nahitaji, mara nyingi nakuwa na uhuru kupanda vifodi.
 
kama suala la lift huombwa mara moja tu na kilichobaki ni kutekeleza ... na mara nyingi linakuwa la njia moja ama kwenda ama kurudi na mara nyingi kuna muda maalumu ambao hukubalika na pande zote.. na muombaji shurti awahi na asubiri na si kusisitiza au kulazimisha
 
Wivu unatakiwa kuwa na mipaka...Msaada unatakiwa kuwa na mipaka pale mtu unapokuwa unaumia.
a) Mwambie asitoke nao kazini kuja nyumbani-labda kama huwa anapitia somewhere atoe excuse. Kuwapa lifti wakati wa kutoka ndio hatari zaidi, kwa sababu hawakawii kusugest wapitie somewhere kama friends halafu yakaenda kuwa mengine..
b) Kwenda nao kazini asubuhi awasaidie tu, kwa sababu hata ukiwazuia kazini watakutana na wata'interact' masaa yote ya kazi na siku zote za kazi ambapo ni muda mrefu sana ukilinganisha na huo wa kukaa kwenye gari na kwenda.
c) Nawashaurini wote kupenda siasa za mwalimu za ujamaa na kujitegemea! tuwasaidie watu na sisi tukisaidiwa sio ndo tunafanya ni wajibu- eti everyday we wapewa lifti tu!

d) Zingatia acbui : :A S thumbs_up: Jioni :A S thumbs_down:
Asubuhi watu wanakuwa wanawaza sana kazi, Jioni wamekaa kimapumziko na kistarehe zaidi....

e)Haya yote yana exceptions, kwa sababu vitu hutokea tu hata ukikaba mpaka kivuli bado haisaidii..so alow youself an occupation error, usije kufa kwa wivu bure.
 
Raha ya lift uipate kwa bahati yaani ukiwa hujategemea lakini hizo habari za kupeana lift kila siku hata ingekua mie kiroho kingenidunda..
Katika maisha kusaidiana ni kawaida lakini sio kila siku hiyo imekua too much sasa au walitoa mchango kidogo kwenye ununuzi wa gari??
Abiria chunga mzigo mazoea ya lift mwisho wa siku unakuja kugundua mmoja kati yao mke mwenzio,wengine wakipewa lift wanataka kupiga honi kabisa..
 
Sioni kosa kama una muamini mme wako, kama humuamini hapo sasa ni shida tupu.
 
Weee.... funguka bidada. Mwambie mme kuwa the way u feel kuhusu hilo. kwanini wampigie kila siku. nyakati za asubuhi ni sawa lakini sio kila siku bana. afu itokee tu kwa bahati co kama wameweka order kwny tax ama hilo sio gari la ofc. mwambie mmeo mara nyingine awe anatoka excuse kwua anapitia mahali flani au siku hiyo atachelewa kutoka home kama hao wadada wana akili timamu watasoma alama za nyakati......
 
Kwa mm ninae jijua kuwa nina wivu mpaka naugua sio sawa hata kidogo.Hao waomba lift kwann wasisubirie tu hiyo lift itokee kama bahati.Binadamu wa siku hizi walivyo na tamaa sasa!!mara watake kumiliki jumla

Asante Hopecomfort, ulivyowaza ndivyo nilivyofikiria kuwa huwa lift inatokea kwa bahati, sasa hili ka kupiga simu kabisa kuomba lifti hapo ndiyo nilipata utata kwa kuzingatia ubinadamu wetu...
 
hao wapige marufuku kabisa chelea chelea utakuta mwana si wako wanaanzaga hivo.:fear:

sasa mpendwa wa kupiga marufuku ni waombaji au ni kuongea na muombaji ili aache hiyo kitu?embu fafanua hapo
 
Kwa mwanamke mwenye akili timamu, si sawa kumganda mume wa mtu kwa lift kila siku
Lazima mtaishia kitandani.

Na hata kwa wanamme, unamwombaje mdada tena mke wa mtu lift kila siku
Tena unawahi siti ya mbele nusura ubadili na gia
Akiachika, hope utamlinda.

Anyway, mtizamo wangu wa lift huwa naomba mara moja wakati kweli nahitaji, mara nyingi nakuwa na uhuru kupanda vifodi.


Asante Kongosho nilidhani hivyo pia,tena kwa mwanamke anayejiheshimu lazma awe na hofu ya kumpigia mume wa mtu kwa, lakini pale inapotokea mtu hana hata hofu asubuhi asubuhi anapiga simu kuomba lift hapo ndipo ninaposhangaa!
 
aisee hii ni bongo movie live...lift ni mbaya!na foleni hii ya daslamu wataongea nini mpaka posta kwa mfano?

hapo sasa! nway wanaweza wakaongea mambo mema tu lakini pale mazoea yanapojenga tabia lolote linaweza kuzaliwa!
 
kama suala la lift huombwa mara moja tu na kilichobaki ni kutekeleza ... na mara nyingi linakuwa la njia moja ama kwenda ama kurudi na mara nyingi kuna muda maalumu ambao hukubalika na pande zote.. na muombaji shurti awahi na asubiri na si kusisitiza au kulazimisha


BPM hapa sijakuelewa,kwa hiyo kinachotakiwa asiwe anapiga simu awe anawahi mahali anapoweza kukutana nae? je unadhani kuendekeza lift pia ni sawa? kwanini mtu asijiendee tu ikitokea iwe ni goodluck?
 
Wivu unatakiwa kuwa na mipaka...Msaada unatakiwa kuwa na mipaka pale mtu unapokuwa unaumia.
a) Mwambie asitoke nao kazini kuja nyumbani-labda kama huwa anapitia somewhere atoe excuse. Kuwapa lifti wakati wa kutoka ndio hatari zaidi, kwa sababu hawakawii kusugest wapitie somewhere kama friends halafu yakaenda kuwa mengine..
b) Kwenda nao kazini asubuhi awasaidie tu, kwa sababu hata ukiwazuia kazini watakutana na wata'interact' masaa yote ya kazi na siku zote za kazi ambapo ni muda mrefu sana ukilinganisha na huo wa kukaa kwenye gari na kwenda.
c) Nawashaurini wote kupenda siasa za mwalimu za ujamaa na kujitegemea! tuwasaidie watu na sisi tukisaidiwa sio ndo tunafanya ni wajibu- eti everyday we wapewa lifti tu!

d) Zingatia acbui : :A S thumbs_up: Jioni :A S thumbs_down:
Asubuhi watu wanakuwa wanawaza sana kazi, Jioni wamekaa kimapumziko na kistarehe zaidi....

e)Haya yote yana exceptions, kwa sababu vitu hutokea tu hata ukikaba mpaka kivuli bado haisaidii..so alow youself an occupation error, usije kufa kwa wivu bure.

Petcash rafiki,asante kwa mtizamo wako..lakini binafsi sikatai mtu kusaidiwa lakini unadhani ni sawa hata kama ni jioni wewe kama mume wa mtu uwe na mtu wako permanent wa kumpa lift hata kama mnakaa njia moja?je ni sawa kuwa unapokea simu za kuomba lift halafu huoni shida tena unafanya kuharakisha ili kumpick aliyekuomba lift?
 
Raha ya lift uipate kwa bahati yaani ukiwa hujategemea lakini hizo habari za kupeana lift kila siku hata ingekua mie kiroho kingenidunda..
Katika maisha kusaidiana ni kawaida lakini sio kila siku hiyo imekua too much sasa au walitoa mchango kidogo kwenye ununuzi wa gari??
Abiria chunga mzigo mazoea ya lift mwisho wa siku unakuja kugundua mmoja kati yao mke mwenzio,wengine wakipewa lift wanataka kupiga honi kabisa..

hapo kwenye red ndicho ninachokiamini, lakini inapokuwa ni utaratibu wa kuuliza kwa simu hapo ndipo ninaposhindwa kuelewa!
 
Sioni kosa kama una muamini mme wako, kama humuamini hapo sasa ni shida tupu.

Namuamini sana tu fazaa lakini hii tabia ya hizi simu ndiyo ilinishangaza kidogo nikadhani kuwa haipaswi kuwa hivyo.
 
Back
Top Bottom