GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Wanabodi, Kuomba msamaha sio ujinga bali ni kujitakasa mbele za Muumba.
Napenda kutumia nafasi hii kuomba msamaha kwa wote niliowakosea kwa kujibu hovyo au kutukana Katika thread zangu, Reply Back na Comments zangu.
Nimeomba radhi baada ya kujifunza jinsi kwa kipindi cha mwezi mmoja tangu Hayati Rais wetu afariki dunia na kabla hata nguo hazijaoza jinsi wanaobaki wanakusuta, wanakusema na kuongea ubaya wako wote wa uliyoyafanya hapa Duniani.
Hakika nimechukua mitazamo mipya sana na kuamua kuacha baadhi ya Propaganda pembeni ambazo zilikuwa zinakwaza na kuumiza Wengine huku nikijua sio sahihi nifanyacho kwa taaluma yangu na weledi wangu. Zaidi ya hapo wazazi wangu hawakunilea hivyo kuwa mtu wa kupiga Propaganda wakati maelfu wanaumia.
Nina mazuri yangu mengi hapa JF ambayo niliamua kutumia akili zangu na mchango wangu vizuri hayo nitayaendeleza kwa weledi na taaluma yangu.
Propaganda zote nilizozifanya hapa JF kwa miaka mitano za kusifia pale palipoharibika ninaomba msamaha kwa niliowakwaza.
Kwa Imani yangu Mimi huwezi kwenda mbele bila toba na kuyaorodhesha baadhi ya mambo niliyoyafanya kwa Propaganda huku nikijua ni uwongo.
Mosi, Kusifia ajira kwa vijana huku nikijua vijana wana hali ngumu.
Pili, Propaganda za mishahara kwa watumishi kuwa wasiongezwe bali iendane na Uchumi huku nikijua ni haki yao ya msingi.
Tatu, Kumjibu mtu vibaya kwa kugusa Personalities zake Baba yake, Mama yake au Familia yake badala ya kujibu hoja yake. Hili limeniumiza sana na ninaomba msamaha sana.
Mwisho, Tuishi kwa upendo na Amani, Tuongee yaliyo kweli daima kwa maslahi ya Taifa letu.
Tuishi vizuri ili watu wasimulie mema yetu lakini si kwa kusimulia maovu na ubaya wetu, Tuombe msamaha pale tunapokosea.
Napenda kutumia nafasi hii kuomba msamaha kwa wote niliowakosea kwa kujibu hovyo au kutukana Katika thread zangu, Reply Back na Comments zangu.
Nimeomba radhi baada ya kujifunza jinsi kwa kipindi cha mwezi mmoja tangu Hayati Rais wetu afariki dunia na kabla hata nguo hazijaoza jinsi wanaobaki wanakusuta, wanakusema na kuongea ubaya wako wote wa uliyoyafanya hapa Duniani.
Hakika nimechukua mitazamo mipya sana na kuamua kuacha baadhi ya Propaganda pembeni ambazo zilikuwa zinakwaza na kuumiza Wengine huku nikijua sio sahihi nifanyacho kwa taaluma yangu na weledi wangu. Zaidi ya hapo wazazi wangu hawakunilea hivyo kuwa mtu wa kupiga Propaganda wakati maelfu wanaumia.
Nina mazuri yangu mengi hapa JF ambayo niliamua kutumia akili zangu na mchango wangu vizuri hayo nitayaendeleza kwa weledi na taaluma yangu.
Propaganda zote nilizozifanya hapa JF kwa miaka mitano za kusifia pale palipoharibika ninaomba msamaha kwa niliowakwaza.
Kwa Imani yangu Mimi huwezi kwenda mbele bila toba na kuyaorodhesha baadhi ya mambo niliyoyafanya kwa Propaganda huku nikijua ni uwongo.
Mosi, Kusifia ajira kwa vijana huku nikijua vijana wana hali ngumu.
Pili, Propaganda za mishahara kwa watumishi kuwa wasiongezwe bali iendane na Uchumi huku nikijua ni haki yao ya msingi.
Tatu, Kumjibu mtu vibaya kwa kugusa Personalities zake Baba yake, Mama yake au Familia yake badala ya kujibu hoja yake. Hili limeniumiza sana na ninaomba msamaha sana.
Mwisho, Tuishi kwa upendo na Amani, Tuongee yaliyo kweli daima kwa maslahi ya Taifa letu.
Tuishi vizuri ili watu wasimulie mema yetu lakini si kwa kusimulia maovu na ubaya wetu, Tuombe msamaha pale tunapokosea.