Horse power itakupa nguvu zaidi kwenye tractor yako. Horse power inapozidi kuwa kubwa ndio nguvu ya tractor pia inazidi kuwa kubwa. Lenye 4wd linakua zito zaidi ila pia lina kua na faida ya kupita maeneo korofi zaidi, lenye 2wd ni jepesi linakimbia zaidi ila uwezekano wa kushindwa kupita maeneo korofi ni mkubwa ukilinganisha na la 4wd. Wingi wa horse power, na lenye 4 au 2 wd inategemea sana na aina ya mashamba unayolima yakoje au unaenda kufanyia kazi gani.
Kwa mfano, kama unaenda kufanyia kazi mashamba ya maeneo ya kibaigwa, tractor la hp 50 hadi 60 na ni 2wd linatosha kabisa maana udongo wa kule ni kichanga. Ila kama unaenda mashamba yenye mfinyanzi lenye 4wd utafanya kazi vizuri zaidi.
Pia kama unahitaji tractor kwa ajili ya kusombea mizigo na barabara ni nzuri lenye 2 wd na hp ya kuanzia 65 linaweza vuta mzigo wa gunia hadi 50 za mahindi vizuri tu.
Tractor karibia zote ni nzuri. Ila usijaribu kununua za kichina. Nina ushuhuda mzuri sana wa tractor aina tatu tofauti za kichina ambazo zinavutia kwa muonekano ila ni takataka kwenye uimara. Massey ferguson trekta yeboyebo kabisa na upatikanaji wa spare na mfundi kwa hili wala usiwe na hofu. New holland tractor imara spare na mafundi pia wapo. Farmtrack, spare zipo za kutosha na mafundi wa kutosha na inafanya kazi safi kabisa namiliki mbili hizo farmtrack so naongea kitu ninachokijua vizuri sana. Swaraj spare zipo kibao na mafundi kibao pia ila ni nyepesi, vinakimbia kama gari

. Taffe ni kama massey ferguson spare zinaingiliana. Matrekta hayo hapo juu yote ni mazuri sana tu na bei zinaanzia milioni 32 hivi kuendelea kutokana na ukubwa wa tractor.
Sasa kwenye hili kundi la ford, john deere, sonalika, kubota, fendt. Hizo ziache kabisa ni kama kumiliki rolls royce au range rover velar na nissan pathfinder, ni nzuri sana ila bei ya spare zake ni bei ghali sana na upatikanaji wa spare ni mgumu pia na mafundi wengi hawazijui hizo. Usidanganyike mtu kukuambia utaagiza online, sawa spare itafika je itachukua muda gani kufika na je mvua itakua inasubiri wewe utengeneze chombo chako ndo inyeshe? Sonalika na john deere nime experience tabu ya upatikanaji wa spare na wanaouza spare zake wanaringa sana.
Ukiwa na maswali usisite kuuliza. Pia utambue kumiliki tractor ni kama gari, sio kwa sababu inapiga kazi ngumu ndo usifanye service kwa wakati, litakuliza. Zingatia kila kitu na kwa wakati