Naomba msaada wa tractor kuanzia 50 hp

Naomba msaada wa tractor kuanzia 50 hp

Swaraji ni teknolojia ya muhindi but kakopy block na gia box kutoka kwa massey furgason ....nina uzoefu mkubwa na matreka hili ni trekta langu la pili kumiliki baada ya ford

sent from toyota Allex

Ni vizuri.
Kwa hiyo wewe ungemshauri mtu anunue tractor lipi kati ya ukilinganisha gharama zauendeshaji na uzalizhaji wa hasa uwezo wa kulima na kubeba mizigo?:
1: Massey furgason
2:FIAT
3:FORD
4:Farmtract
5: New holland
6: Ursus
7: SWARAJ
8: Johndeer
9: Kubota
 
Kwa mimi na ujuzi wangu trektor bora amabayo haina kokoro

1.FORD

2. BERALAUS

3.MAHINDRA


Hizo ni chaguo number moja na ninajua uzuri wake zaidi na ubora wake ...kwa kuwa nimezitumia na nimezimiliki expt hiyo mahindra ...but kuna mahali nimeiona ifanya vizuri haisumbui pump wala planger zake ,

Ugonjwa ...wa trector nyingi ni fuel pump zinasumbua balaa.....utalifurahia miez mitatu ya mwazo baada ya hapo utatamani uanze modification

Umri wangu ni mdogo but matrekta na ujuzi nayo sana
I

sent from toyota Allex
 
Soma utafiti uliofanywa wa matrekata ya holland kama URUSS NA NEW HOLLAND

Taasisi iliingia mkataba wa kufanya majaribio ya matrekta ya Kampuni ya URSUS S. A ya Poland Oktoba 4, 2016 na kuanza majaribio ya matrekta hayo kuanzia Desemba, 2016 baada ya matrekta hayo kuingizwa nchini.

Matokeo ya jumla ya matrekta hayo kutoka Poland yameonyesha matokeo mazuri ya kulima (ekari 0.97 hadi 1.75 kwa saa) na matumizi ya mafua (lita 5.7 hadi 5.9 kwa saa). Matrekta mengi huwa yanakuwa na viwango kama hivi. “Tulifanya pia vipimo vya uhimili (durability test). Kwa upande huo tumegundua mapungufu kadha wa kadha ikiwemo:-

“i. Mfumo dhaifu wa umeme unaosababisha vifaa mbalimbali kama vile taa kuharibika mara kwa mara. ii. Udhaifu wa matairi ya mbele uliopelekea rimu za matairi hayo kuvunjika mapema na pancha za mara kwa mara.

iii. Mifumo dhaifu ya uinuaji jembe (three point linkage) uliosababisha baadhi ya vifaa vyake kuvunjika mara kwa mara.

iv. Mfumo dhaifu wa kuvuta mafuta (throttle), kutoa moshi (exhaust) na kuchuja hewa (air cleaner) iliyokuwa ikiharibika mara kwa mara.

v. Baadhi ya sehemu zilizoharibika kama vile “front axle support” na “rim” zinaonyesha udhaifu wa baadhi ya vipuri vilivyotengenezwa kwa kumiminwa (casting). Hivyo, upo uwezekano wa sehemu mbalimbali zilizotengenezwa kwa kumiminwa kuwa dhaifu.

vi. Udhaifu mwingine umeelezwa zaidi kwenye ripoti zetu tulizoambatanisha,” inasema sehemu ya barua hiyo.

INSHORT HAYADUMU

sent from toyota Allex
 
Soma ushuhuda wa wakulima
Wakulima waeleza matatizo

Wakulima kutoka Iringa, Babati, Morogoro na maeneo mbalimbali ya nchi waliozungumza na JAMHURI, wamesema kuwa matrekta hayo ya URSUS yanawasumbua kwa kiasi kikubwa na wanapata shaka iwapo yataweza kufanya kazi kwa miaka miwili na zaidi.

Martine Qamary Ori wa Babati, Manyara, ameliambia JAMHURI kuwa betri mbovu, rimu zimevunjika, breki, wiring, taa zinazimika, cable ya accelerator (chapuzi) imekatika, gearbox inavujisha mafuta.

Athumani Hemed Kazikubwa – Kilindi, amesema pini ya kati ya kwenye kifua cha trekta inachomoka, wakati trekta linalima wanarudishia.

Ibrahim George Voniatis wa Ndanda, Mtwara, anasema kuhusu tairi za mbele: “Inakuwa kama vile unatembelea ‘tyubu’, yaani miba kidogo tu, tunakuta umepata pancha, hilo ndilo tatizo kubwa ambalo naliona.” Amenunua tairi za mbele mpya kwa Sh 400,000 na akaongeza: “Wiring ilikuwa inasumbua ile ya mwanzo ya 4wheel, honi switch inakataa, switch ya taa, switch… tairi hizi ni za Ulaya, hazifai hapa kwetu.”

Peter William Hhayuma, Mwenyekiti wa URSUS Tractors Family, katika maeneo ya Hanang, Karatu, Babati, Mbulu na Itigi, umoja ambao una wanachama 50, anasema: “Hili tatizo la rimu linachangiwa na adjustment ya jembe wakati unalima.

“NDC kwa sababu ni wageni na hiki chombo hawakuwa na wataalamu wa kuendesha haya matrekta, lakini mafundi wa vijijini kwa sababu ni wazoefu wamebaini, kuwa kisu cha nyuma kimenyooka, wamekipindisha kwa kukata shafti, unaipindisha ili iweze kuvuta, usipofanya hivyo unailazimisha kwenda kwenye system (mfumo) ambayo siyo.

“Oil kuvuja, kuna matatizo ya uvujaji na hilo linachangiwa katika hali ya ufungaji, zinakuja kuungwa hapo Dar es Salaam, kuna uzembe katika hatua za ufungaji ninavyoona mimi… ni kwamba chombo chako unapochukua, hata kama ungechukua gari mpya ukaamua kuanza nayo kwa kudhani kuwa ni mpya unakwenda mbele lazima itakuletea shida.

“Kununua nati, bolti… la kwangu, uvujaji ulikuwa kwenye tela nyuma, ilikuwa kumbe kuna seal kule nyuma imekufa, lakini kwa sababu ilikuwa kwenye ‘guarantee’ waliruhusu tuitengeneze.”

Wakulima wanalipa asilimia 10 ya bei ya kununulia trekta hiyo iliyopata msamaha wa kodi na kukabidhiwa trekta, hivyo 75HP inauzwa wastani wa Sh milioni 56 na ya 50HP inauzwa Sh milioni 45. “Mrejesho wake ni miaka 4, unarejesha bila riba, na mwaka wa 5 ndipo unalipa 10%. Kwa kweli huu ni ukombozi kwa mkulima, maana benki nyingine mpaka upeleke hati.

“Katika mpango huu unapeleka barua ya kijiji, kata au mkurugenzi wako anayekufahamu unakopeshwa trekta… kwa hiyo inarahisishia wakulima, baada ya kuona kwamba hili jambo ni zuri, watu tumeamua kuanzisha umoja na kama kuna tatizo mawasiliano yetu mtu anapiga simu unawajulisha huko NDC.

“Yalikuwa na tatizo la matumizi ya mafuta, kwenye system ya mafuta suala la injector kwenye chombo kilichopo kwenye guarantee huwezi kugusa, akatushauri fundi wetu kwamba tufanye adjustment, huyu kijana sasa hivi NDC wamempeleka Mwanza, Mafinga kurekebisha matatizo ya matrekta haya.”



sent from toyota Allex
 
Swaraji ni teknolojia ya muhindi but kakopy block na gia box kutoka kwa massey furgason ....nina uzoefu mkubwa na matreka hili ni trekta langu la pili kumiliki baada ya ford

sent from toyota Allex
Habari, nina tractor Belarus, inanisumbua sana spare, namba yangu 0788475371 naomba tuwasiliane kama una access na spare zake.
 
Kwa mimi na ujuzi wangu trektor bora amabayo haina kokoro

1.FORD

2. BERALAUS

3.MAHINDRA


Hizo ni chaguo number moja na ninajua uzuri wake zaidi na ubora wake ...kwa kuwa nimezitumia na nimezimiliki expt hiyo mahindra ...but kuna mahali nimeiona ifanya vizuri haisumbui pump wala planger zake ,

Ugonjwa ...wa trector nyingi ni fuel pump zinasumbua balaa.....utalifurahia miez mitatu ya mwazo baada ya hapo utatamani uanze modification

Umri wangu ni mdogo but matrekta na ujuzi nayo sana
I

sent from toyota Allex
Mkuu naomba msaada kujua unapopata spare za tractor ya belarus. Nahangaika sana kupata spare hapa Tanzania. Kuna mzungu mmoja awali alikuwa anauza pale moro lkn naona siku hizi ameacha.
 
Ni reviews nzuri sana zina Saidia wakulima na wajasiriamali.. Nipo harakati za mwishoni kuingiza Massey furgason pcs 5 za hp 80 na hp 90 recondition ikiwa na planter na jembe lake
 
Ni reviews nzuri sana zina Saidia wakulima na wajasiriamali.. Nipo harakati za mwishoni kuingiza Massey furgason pcs 5 za hp 80 na hp 90 recondition ikiwa na planter na jembe lake
Usisahau na harrow ili planter ifanye kazi kwa ufasaha
 
DUH Nimesoma thread zote bado sijapata jibu kamili (kwa kulima udongo wa mfinyanzi heka 5 kwa siku na kukokota mizigo ya ujenzi) ni tractor ipi na size gani iliyo BORA ? ? ?
 
DUH Nimesoma thread zote bado sijapata jibu kamili (kwa kulima udongo wa mfinyanzi heka 5 kwa siku na kukokota mizigo ya ujenzi) ni tractor ipi na size gani iliyo BORA ? ? ?
Huwa nalima udongo mfinyanzi kwa trekta mara nyingi tu. Trekta yoyote yenye hp kuanzia 75 kuendelea inafaa. Ikiwa na 4wd uhakika wa kutokwama kizembe unaongezeka. Udongo mfinyanzi ukikosa maji kwa muda mrefu ni mguma sana hata kulima unasumbua na ukipata maji mengi unateleza sana na unanata sana ambayo inasababisha usumbue kwenye kulima. Timing ni muhimu, mimi huwa nasubiri inyeshe mvua ambayo nina uhakika imelowanisha udongo vya kutosha then naingia na trekta kulima
 
DUH Nimesoma thread zote bado sijapata jibu kamili (kwa kulima udongo wa mfinyanzi heka 5 kwa siku na kukokota mizigo ya ujenzi) ni tractor ipi na size gani iliyo BORA ? ? ?
Kuokota mizigo ya ujenzi, tutaangalia vitu vifuatavyo
1:uzito wa mizigo na uwezo wa trailer. Unaweza kuta uzito wa mizigo ni tani 7 na trailer lako linabeba tani 4. Hapo ujue utaharibu chasis ya trailer. Zingatia hilo
2: barabara utakayokua unapita. Kama ni barabara ya lami au vumbi iliyo nzuri wakati wote. Trekta la 2wd hp kuanzia 60 kuendelea linafaa. Ila kama barabara iba miinuko mikali na mvua ikinyesha inachafuka sana, trekta la 4wd na hp 75 na kuendelea ndo litafaa
3:dereva mzoefu nalo ni muhimu sana
Aina karibia zote za trekta zinafaa iwe tu na uwezo wa kufanya kazi husika kwa kufuata vigezo vya kazi na uwezo wa trekta.
New holland
Farmtrac
Massey
Fiat
Swaraj
Ford
John deere
 
Hizo ulizozitaja Massey Ferguson na New Holland zote ni takataka kwa sababu zote zinatengenezwa uturuki na pakistani. Achana nazo.

Kamata kitu cha FARMTRAC. Hizo ndiyo trekta za uhakika kwa ardhi yoyote ya Tanzania, zinalima mpaka ekari 45 kwa masaa 12. Zinabeba mzigo mkubwa na mzito sana na shambani hata udongo wa matope zinalima kwa spidi ya Ferrari.
Nakushauri nenda pale SUMA JKT kama FARMTRAC moja uanze kunuka pesa,
Ukikosa FARMTRACK kamata URSUS.
ulipotaja Ursus tu nikajua wewe ni chenga
 
Mwenye spare hii ya new holland 4WD Hp 75
IMG_20211029_162448_401.jpg
 
Back
Top Bottom