Naomba msaada, nakabwa na wachawi usiku

Naomba msaada, nakabwa na wachawi usiku

Kabla ya kulala hakikisha unasali na kumwomba Mungu ulinzi kwa Jina la Yesu Kristo. Hiyo ni funga kazi kwa kila kitu katika maisha yako! Nina uhakika asilimia 100. Wakija usiku ita Yeeesu! Kwisha habari yao. Pia kabla ya kulala jifunike pamoja na nyumba yako kwa Damu ya Yesu. Wakija wataona maajabu yote humu ulimwenguni. Usipoteze muda wala mia yako kwa mganga, Yesu ni yote katika yote.
 
Habari zenu wadau, mimi naomba kujuzwa njia ya kujikinga na hawa wachawi wanaonitesa usiku, yaani unakabwa hadi ukishtuka unaona kichwa hakiko sawa, nimechoka sana na hawa wanga.
Naomba msaada niepukane na hili janga jamani.
wambie waje kwangu nina hamu sana
 
Uzuri ww ndo unaelewa unavyoteseka!

Hakuna kitakachokusaidia zaidi ya Yesu blv mi!
 
Mkubwa Mshana njoo huku msaada Kitabu cha Yoshua bin Sira (31:27-29) kinasema: ”Kwa wanadamu mvinyo ni kama maji ya uzima, ukinywa kwa kiasi. Je, anao uzima gani mtu asiye na mvinyo? Nayo imeumbwa ili kuwafurahisha wanadamu. Mvinyo ni furaha ya moyo na changamko ya roho, ikinywewa kwa wakati wake na ya kutosha. Lakini kunywa mno ni uchungu wa roho, na fedheha, na ugomvi.”ako ni muhimu sana hapa.
Unamchanganya!
 
Unalala vibaya tu wewe!!
Hakunaga kitu kama kukabwa usingizini!
Nakushauri pia usiamini mambo ya uchawi hutaishi kwa amani na furaha!!
 
MPE yesu maisha yako , kingine hapo umeshashinda maana mambo ya kiroho yakidhihirika katika ulimwengu wa nyama ujue wamekushindwa , ila na wewe kazana kumjua yesu na agano lake LA damu ,
 
Acha ujinga huo, hakuna wachawi wala kukabwa, njia ni moja tu
Usipende kulala huku ukiwa umeshiba sana, lala masaa matatu baada ya kula hutaona hizo ndoto.
Asipokuelewa nitashangaa
 
Sasa umelala alafu umekabwa, umejuaje kama umekabwa ukiwa usingizini, unaonekana una msongo wa mawazo, jitahidi kunywa maji ya kutosha, sali na usipende kukaa ndani peke yako muda mrefu, uchawi utafanya kazi kwako ikiwa utauamini. Usimuhisi jirani yako vibaya.
 
Sali rosari daily before bed
Ila wahuni wanakwambia piga gambe na cha arusha na ikishindikana lala macho..
 
Back
Top Bottom