Naomba mbinu bora ya kumuachisha mwanangu kunyonya

Naomba mbinu bora ya kumuachisha mwanangu kunyonya

masai dada

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
16,703
Reaction score
16,378
Ana miaka 2 sasa kasoro siku kadhaa, ila kila nachojaribu kufanya naona namuumiza analia sana nikisema nimkazie siku hiyo asiguse nyonyo.

Ananikondesha sasa hivi maana spidi ya kunyonya imekuwa kubwa.

Nipeni mbinu rafiki za kumuachisha ziwa mwanangu bila kumuumiza.
 
Ana miaka 2 sasa kasoro siku kadhaa
Ila kila nachojaribu kufanya naona namuumiza analia sana nikisema nimkazie siku hiyo asiguse nyonyo.
Ananikondesha sasa hivi maana spidi ya kunyonya imekua kubwa.
Nipeni mbinu rafiki za kumuachisha ziwa mwanangu bila kumuumiza
Unaweza kuendelea kumnyonyesha mpaka aache mwenyewe.

Sio mbaya sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swali; Hivi weye mamako angekunyima nyonyo ungekuwa hapa JF kweli?? Hakuna dhuluma mbaya ka kuangalia kwa macho unachokitamani halafu hupewi ruhusa kujisevia mwenyewe.
Usimdhulumu chalii wa watu, Mwache anyonye weye ongeza ugali ule zaidi na maji na mamboga mengi ila maziwa yatiririke hadi akinai. Kiutaalam watoto walionyonya vya kutosha 3yrs huwa na akili sana
 
Swali; Hivi weye mamako angekunyima nyonyo ungekuwa hapa JF kweli?? Hakuna dhuluma mbaya ka kuangalia kwa macho unachokitamani halafu hupewi ruhusa kujisevia mwenyewe.
Usimdhulumu chalii wa watu, Mwache anyonye weye ongeza ugali ule zaidi na maji na mamboga mengi ila maziwa yatiririke hadi akinai. Kiutaalam watoto walionyonya vya kutosha 3yrs huwa na akili sana


Kweli kbs mkuu naunga mkono hiyp hoja! Mie niliachisha mwanangu nikashindwa kbs!yaan Dk akasema anyonye tu!hv had leo ananyonya!n ni kipanga balaa darasani..ana uelewa mkubwa sana
 
Swali; Hivi weye mamako angekunyima nyonyo ungekuwa hapa JF kweli?? Hakuna dhuluma mbaya ka kuangalia kwa macho unachokitamani halafu hupewi ruhusa kujisevia mwenyewe.
Usimdhulumu chalii wa watu, Mwache anyonye weye ongeza ugali ule zaidi na maji na mamboga mengi ila maziwa yatiririke hadi akinai. Kiutaalam watoto walionyonya vya kutosha 3yrs huwa na akili sana
Kabisa nyonyo ya mama humfanya mtoto awe na akili pia awe na afya bora, chamsingi mtoto amuongezee menu, kwa umri aliofikia na sio kumdhurumu.
 
Hahaha duuh huo ni mtihani,first born wangu alinyonya hafi miaka miwili na miezi mitatu, kila mbinu aligoma nikamwanzisha day care akawa anashida asubuhi hadi saa sita, it nilikua nimeshamwambia mwalimu kwamba dogo ananyonya sana a mbinu zote za kumwachisha zimegima, mwalinu akamwita akamwambia watoto wanaonyobya hawaruhusiwa kwenda shule, duuh siku hiyo ninetoka kazini akniambia taki tena nyonyo mimi ataka chule tu

Second born wa kiume ndo alinyonya hadi miaka miwili na nusu, kilambinu iligoma, nikabeba mimba nyingine, wakazi huo nilikua natapika sana na nilikua weak kwa hiyo ikifia wakati nikalazwa hospitali wiki nzima, niliporudi alikua kadhasahau nyonyo

Wa tatu yeye alinyinya mwaka na nusu halafu nikabeba mimba nyingine, kirho safi akaendelea na amziwa ya kopi sema amegoma kuacha kunywa amziwa kwenye chuchu mpka aleo n ana miaka mitatu na nusu, n hawezi kulala bila kujibembeleza na chuchu, kwa siku anamaliza chuchu hata tani, shuleni ana kopo lake na yakiisha wanamkorogea wanajaza kwenye chuchu yake

Huyu last born ndio balaa, kwa sasa menibatiza jina ananiita nyonyo, akiniona tu anaita nyonyoooo

Ana miaka 2 sasa kasoro siku kadhaa
Ila kila nachojaribu kufanya naona namuumiza analia sana nikisema nimkazie siku hiyo asiguse nyonyo.
Ananikondesha sasa hivi maana spidi ya kunyonya imekua kubwa.
Nipeni mbinu rafiki za kumuachisha ziwa mwanangu bila kumuumiza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtende,


🤣🤣🤣 tupo wengi!lakin mm najisikia raha sana( akiona nyonyo inaonekana analeta kitenge ananifunika) . sijui kwnn napenda kunyonyesha aisee!kitu nimefaulu na sichoki ni kumnyonyesha mtotot aisee!niliwah soma kwenye pregnacy magazine mtoto anayenyonya kwaukamilifu haptw na magonjwa ovyo ovyo basi ikawa ndalilo😅! Mie mvivu kubeba mtoto aisee!na kubeba mimb🤦!
 
Unaweza kwenda nae kwa bibi au aunt yake wewe utaondoka akabaki kwa wiki1 au 2. Mkikutana atakua kasahau nyonyo. Kipindi cha kumwachisha huwa kigumu sana kwa mtoto....ni sawa na kumnyima mnywaji kunywa beer, jitahidi anywe maziwa, juices na maji ya kutosha kupunguza kiu
 
Unaweza kwenda nae kwa bibi au aunt yake wewe utaondoka akabaki kwa wiki1 au 2. Mkikutana atakua kasahau nyonyo. Kipindi cha kumwachisha huwa kigumu sana kwa mtoto....ni sawa na kumnyima mnywaji kunywa beer, jitahidi anywe maziwa, juices na maji ya kutosha kupunguza kiu


Lakini watoto wengine hawaachi hata usafiri sijui y!
 
Back
Top Bottom