Naomba kwa lugha nyepesi mnieleweshe linux kernel ndio kitu gani?

Naomba kwa lugha nyepesi mnieleweshe linux kernel ndio kitu gani?

Kichwa Ndio Mtu

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2014
Posts
3,079
Reaction score
1,719
Wadau,salam

Mim sio mjuzi wa mambo ya it na computer ila huwa napenda kujifunza hayo mambo kwa ajili ya kupanua uelewa wangu tu.

Sasa kila nikipitia kuhusu operating system hasa hizi open source naambiwa "based on linux kernel",nikitafta maana yake naambiwa tena"unix like" nachoka kabisa.

Ningependa nijue hiyo linux kernel ni nini hadi os zote ziwe based kwake,kingine je hakuna os inayoweza kutengenezwa bila kua "based" kwake?,je closed os zinakua "based" kwenye nini?

Natanguliza shukrani.
 
Sasa kila nikipitia kuhusu operating system hasa hizi open source naambiwa "based on linux kernel",nikitafta maana yake naambiwa tena"unix like" nachoka kabisa.


Hiyo unix-like isikuchanganye !
Kwasabu Linux yenyewe ni clone !

Yaani ni clone ya UNIX ! Na unix ni copyrighted name !
Ukiangalia ReadMe file ya Linux Kernel imesema hivi !

''Linux is a Unix clone written from scratch by Linus Torvalds with assistance from a loosely-knit team of hackers across the Net. It aims towards POSIX (portable operating system interface) compliance.''


Kernel ni central operating system ! Inayo run katika Privileged mode na ina interfere apps ktk user mode na physical hardware yenyewe !

Kuna aina kama tatu za Kernel

MICRO KERNEL

MONOLITHIC KERNEL

HYBRID KERNEL

Lakini Linux Kernel katika aina za kernel yenyewe ni monolithic !

Na ni inatofautiana na hiyo Microkernel !

Hizi windows 7 na OS X zote ni hybrid !

Nazani nimekufungua kidogo !

Ningependa nijue hiyo linux kernel ni nini hadi os zote ziwe based kwake, kingine je hakuna os inayoweza kutengenezwa bila kua "based" kwake?,je closed os zinakua "based" kwenye nini?

Natanguliza shukrani.


Kwenye red hapo sio kweli !
 
kaka umewahi kula tunda damu au embe au tunda lolote lenye kokwa? ile kokwa ndani ndio kama kernel. ni centre ya operating system.

kabla hatujaangalia kazi ya kernel hebu tujiulize swali inakuwaje hadi computer au simu inaonesha vitu kwenye kioo? nikibonyeza herufi kwenye keyboard inatokea kwenye kioo inajuaje hii computer?

basi hapo ndo tunaijua kazi ya kernel yenyewe inakuwa katikati kuchukua request za application zako kama microsoft word au ukicheza game nakuzipeleka kwenye ram au processor kwenye usb port. kwa lugha rahisi kernel ni ile inayokaa katikati baina ya hardware na application zako.

Kernel_Layout.svg


linux kernel ndio inayotumika sana sababu ni open source na bure, kutengeneza kernel ni gharama kubwa sana hivyo kampuni ndogo nyingi haziwezi kuafford na kuamua kutumia kernel ya linux. pia sababu ni open source na inatumiwa na wengi inamaana support itakuwa kubwa na itakua rahisi kupata solution pale ukikwama.

ishu ni tofauti kwa makampuni makubwa wao wana kernel zao wenyewe, mfano kama microsoft kernel yake inaitwa windows nt na ndio inatumika kwenye windows na windows phone.
 
Jaman mi naomba msaada jinsi ya kupost maada humu jamvini
Fungua jukwaa unalokusudia kubandika mada yako(sio maada)scroll mpaka chini upande wa kushoto utaona kifungo cha kuweka mada mpya.
 
Ahsanteni. Siku ya leo nameingiza kitu ktk CPU yangu kichwani
 
Back
Top Bottom