1. ADB debugging, ndio option naitumia sana, kwa ajili ku connect simu ya android na windows pc. Hii inaipa ruhusa pc kufanya mambo kadhaa kama ku disable apps, kuinstall apps, na mengine mengi (ambayo hayawezekani kwa urahisi kuyafanya ukitumia simu) kwenye simu moja kwa moja kwa kupitia waya wa usb.
2. Unlocking Bootloader (OEM Unlock) kwa ajili ya ku root au kuflash custom recovery kama twrp au custom roms.
3. Advanced options / Settings
Kuna options zingine hazipo kwa matumizi ya kawaida kama kubadili transition animation scale na animation duration scale, pia kuna option za kubadili dpi n.k
4. Kudhibiti ufanyaji wa kazi wa apps, hii kama simu ina memory ndogo inafaa sana. Mfano app zinazokula ram sana zinaweza kuondolewa pale mtumiaji anapoifunga inasaidia ku free memory japo itachelewesha app kufunguka itakapotumika tena maana android iwa ina cache activity za app ili ifunguke fasta. Pia unaweza kudhibiti app zinafanya kazi nyuma ya pazia mfano whatsapp inakuwa inafanya kazi ata ukiwa umeifunga hii inakula memory.
5. Wataongezea na wengine