Naomba kujua nini tofauti tago pori na tango la kupanda

Mwanaweja

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
3,575
523
Jana nilikuwa nafuatilia kipindi kimoja redioni kinaitwa "Afya ya jamii" kuna Daktari mmoja alikuwa anaelezea jinsi ya kutibu magonjwa mbali mbali haswa yatokanayo na kuvunjika mifupa, kupasuka kwa mifupa, kusangika kwa vipingiri kama vya mmgongo, kuteguka kwa nyonga, na akasema dawa nzuri yakutumia ni tango pori. Lakini alisema sio tango la kupanda cha ajabu zaidi matango aliyokuwa anayaonyesha ni matango ambayo mimi najua sasa nikawa na shindwa kupata majibu ya haraka tango pori lipi na tango la kupanda ni lipi. Kwa uelewa wangu kuna matango machungu "Limbe" kwa wale ndugu zangu wa wasukuma tunayafahamu kuna matango pori "Limbe Lugulu" yaani matago pori ambayo huwa yanajiotea kwenye porini na matango ya kupanda "limbe" ni matango yale ya asili . Daktari aliyokuwa anaonyesha ni matango ya kupanda. Naomba ufafanuzi kwa yeyote mwenye ufahamu zaidi. Asante sana
 
Back
Top Bottom