Mkogoti
TAPELI Mkubwa
- May 3, 2020
- 2,416
- 3,911
Habari zenu Wakuu!
Kwakweli Tabia yangu hii mimi ndo nimeipalilia mpaka imeota vizuri na jinsi ya kuiacha ndo mtihani.
Ni hivi Mimi ni mtu wa Aibu sana au haya yani naweza kulala ndani siku nzima harafu Usiku natoka naenda kutembea kwa marafiki zangu,
Tena wale marafiki niliowazoea sana tena wa mbali na mtaani kwangu sina rafiki ata mmoja zaidi ya wale ninaosalimiana nao basi imetoka! Yani msiba ata ukitokea ninapata wakati mgumu sana kwenda iyo yote naogopa flani hivi wasinione.
Napata shida sana sana ata nikiwepo pale nakuwa natetemeka muda wote nimekaa makini yani naweza kuwa nafanya kitu hapo kwa usahihi nisikosee, kwakweli hii hali ndugu zangu inanitesa sana, Nikiangalia Vijana wenzangu hapa mtaani wamechangamka sana, wanapiga kelele wanavyotaka wanajidai wanatembea barabara nzima ni zao.
Lakini kwangu ni uyonge tu mimi tena nachangua barabara za uchochoroni kuogopa nisionekane na watu wasinizoee yani nakaa kinyonge muda wote. Naomba kama kuna mshauri nifanyeje niepukane na hali hii🙏
Kwakweli Tabia yangu hii mimi ndo nimeipalilia mpaka imeota vizuri na jinsi ya kuiacha ndo mtihani.
Ni hivi Mimi ni mtu wa Aibu sana au haya yani naweza kulala ndani siku nzima harafu Usiku natoka naenda kutembea kwa marafiki zangu,
Tena wale marafiki niliowazoea sana tena wa mbali na mtaani kwangu sina rafiki ata mmoja zaidi ya wale ninaosalimiana nao basi imetoka! Yani msiba ata ukitokea ninapata wakati mgumu sana kwenda iyo yote naogopa flani hivi wasinione.
Napata shida sana sana ata nikiwepo pale nakuwa natetemeka muda wote nimekaa makini yani naweza kuwa nafanya kitu hapo kwa usahihi nisikosee, kwakweli hii hali ndugu zangu inanitesa sana, Nikiangalia Vijana wenzangu hapa mtaani wamechangamka sana, wanapiga kelele wanavyotaka wanajidai wanatembea barabara nzima ni zao.
Lakini kwangu ni uyonge tu mimi tena nachangua barabara za uchochoroni kuogopa nisionekane na watu wasinizoee yani nakaa kinyonge muda wote. Naomba kama kuna mshauri nifanyeje niepukane na hali hii🙏